Facebook Comments Box

Friday, October 24, 2014

KUELEKEA EL CLASICO ANGALIA PREVIEW HII



HATIMAYE DIAMOND ASALIMISHA SARE ZA JESHI

Kushoto ni Ney wamitego, Diamond Platnum, na Dancer wa Diamond wakiwa katika jukwaa la Fiesta hivi karibuni wakiwa wamevalia mavazi ya Jeshi.

MSANII wa muziki wa kizazi kipya, Naseeb Abdul 'Diamond', amekiri kuhojiwa na polisi baada ya kukutwa na hatia ya kuvaa mavazi yanayoaminika kuwa ni sare ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).

Hata hivyo msanii huyo alidai kwamba mavazi hayo hayakuwa sare za jeshi hilo na kwamba yeye aliyanunua alipokuwa Ujerumani ingawa baada ya kuhojiwa aliyasalimisha.

Diamond alipanda jukwaani Jumamosi iliyopita katika onyesho la Fiesta jijini Dar es Salaam akiwa na mavazi hayo jambo ambalo liliibua mjadala kwa watu walio wengi.

Diamond alikiri kupata ujumbe uliomtaka kufika Kituo cha Oysterbay, Dar es Salaam na madansa wake akiwa na nguo hizo,
"Awali Meneja wangu alishikiliwa kwa muda na mimi nikatakiwa kufika na zile nguo nikiwa na madansa wangu ambao pia walizivaa, nilifanya hivyo na kuziacha nguo baada ya taratibu zote za kisheria kukamilika," alisema.

"Nisingeweza kukaidi amri ya dola, nilifika na yale mavazi na nikahojiwa kwa saa kadhaa. Nikaeleza kwamba yalikuwa yakifanana tu na ya jeshi na hayakuwa sare rasmi za jeshi, kikubwa nilihitaji kumaliza tatizo," alisema.



Q.CHILLAH AELEZEA NANI MKALI KATI YA DIAMOND NA ALI KIBA

Msanii wa Bongo Fleva Q. Chillah

Mapya yanazidi kuibuka kuhusu ushindani wa Diamond na Ali Kiba ambapoushindani huo ulianzia katika hitimisho la tamasha la Fiesta lililofanyika katika viwanja vya Leaders Club Dar. 

Mashabiki wa wasanii hawa wawili wanavutana huku kila mmoja akisema mwenzake ana kipaji na anamfunika mwenzake. Inasemekana kuwa kuna baadhi ya mashabiki walikodiwa kwa ajili ya kumzomea Diamond wakati akitoa burudani siku ya Fiesta na hilo lilithibitishwa na Babu Tale ambaye ni meneja wa Diamond.

kwa sasa katika mziki wa Bongo Flava kumekuwa na fitina nyingi wakati mwingine wasanii kwa wasanii wanachonganishwa na mwisho wa siku unakuwa ugomvi, kwa mfano sasa hivi bifu la Ali Kiba na Diamond.

Q Chief : "Yote wanayopitia ni changamoto ambazo pengine hawakuwahi kuzania kwamba watapitia. Mimi nimepitia situation ambazo zimenijenga kuwa "sugu" na "Legendary" ndiyo maana ya kuwa mkongwe unapitia situation ambazo watu wengine wanakulazimisha ufike huko. 

Hata kama upo level fulani wanakushusha kwa kufikiria kwamba wanaweza kukushusha. Unapandishwa na watu, unapandishwa na mwenyezi Mungu, unashushwa na watu, unashushwa na mwenyezi Mungu. 

Mfano niliangalia Fiesta kwenye TV sikwenda kwa sababu nilikuwa na mambo yangu Studio, hakuna kitu kigeni nlichokiona, nimeona msanii wa marekani anafunikwa na msanii wa Tanzania ambaye ni Ali Kiba. 

Nmeona Ali Kiba ambaye amekaa kimya kwa miaka mitatu bila Airtime na watu wamemzungumzia vibaya, vizuri na nini wamemkubali tena. Ikiwa ni mtu yule yule ambaye wamemkataa na wakumuweka mtu mwingine juu. 

Hakuna kitu kisichowezekana, matokeo uliyoyaona juzi ndio matokeo yanayotokea na yataendelea kutokea. Hakuna Mungu wa hii kazi, hakunaga mfalme wa hii kazi ila kuna masultan wa Hii Kazi.



SOMA MAGAZETI YA LEO IJUMAA TAREHE 24 SEPTEMBA 2014 HAPA




 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU