Facebook Comments Box

Thursday, April 17, 2014

MABADILIKO YA UELEKEO WA BARABARA KATIKATI YA JIJI LA DAR ES SALAAM

MABADILIKO YA UELEKEO WA BARABARA KATIKATI YA JIJI LA DAR ES SALAAM KUANZIA SIKU YA  TAREHE 28/04/2014. TRAFFIC CIRCULATION AT CBD
1. Kipande cha Mtaa wa Samora kuanzia Mnara wa Askari (Askari Monument) hadi Clock Tower, kutakuwa na mabadiliko ambayo magari yatakuwa yanaelekea Clock Tower badala ya Askari Monument.
2. Barabara ya Sokoine kuanzia Station hadi Makutano ya Mtaa wa Maktaba Posta Ya Zamani Magari yatakuwa yanaelekea Uelekeo mmoja wa Station Posta ya Zamani tofauti na ilivyo sasa Posta ya Zamani kwenda Station.
3. Barabara ya Kivukoni  Kuanzia Posta ya Zamani hadi Ferry itakuwa barabara ya mielekeo miwili (Two Ways).
4. Barabara ya Samora kuanzia Mnara wa Askari hadi Ocean Road Hospitali itakuwa ni barabara ya mielekeo miwili.
5. Daladala Zote zitakazotokea barabara za  Makataba zitakunja kulia pembeni ya Jengo la NBC na hadi Makutano ya Mkwepu na kukunja kushito kuingia Sokoine pale Posta ya Zamani na baadaye kukunja kushoto kuingia Makataba na kurudi Posta Mpya .
Key:
1. RANGI YA NJANO - Njia ya Uelekeo Mmoja {One Way}.
2. RANGI YA BLUE MPAUKO - Njia ya Mielekeo Miwili {Two Way}
3. RANGI YA KIJANI - Mitaa ya Kutembea kwa Miguu Magari marufuku {Walking Streets}
4. RANGI NYEKUNDU - Barabara za kupita Daladala
5. RANGI YA BLUU ILIYOIVA - Barabara za DART
6. DUARA ZA NJANO - Mzunguuko {Roundabout}
7. MSALABA WA KIJANI - Makutano yenye Taa za kuongozea Magari {Singnalized Intersection}
Kwa Maelezo zaidi Wasiliana na Ofisi za DART
UBUNGO PLAZA GHOROFA YA KWANZA.
AU.
OFISI YA MHANDISI WA MANISPAA YA ILALA
MABALA NA SHOPRITE SUPEEMARKET JIRANK NA KAMATA
Ni muhimu kwa waendesha magari wote kujua habari hii muhimu !!!!
Hasa mimi ninaesoma sasa
Mtaarifu mwingine juu ya mabadiliko haya kuondoa usumbufu ifikapo siku ya Jumatatu 28/04/2014.


NMB WATOA MSAADA KWA HOSPITALI YA MWANANYAMALA.

Nmb imekabidhi msaada wa vifaa vya hospitali vyenye thamani ya milion 5 akipokea msaada huo Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mwananyamala Dkt. Kariamel Wandi ameishukuru Nmb,misaada hii imewasilishwa na Meneja wa NMB kanda ya Dar es salam Ndg,Salie Mlay.


WAMILIKI WA TV IMAAN KUANZISHA GAZETI LAO.

Mweyekiti wa The Islamic Foundation Brother Aref Nahdi akiwa na
Mkurugenzi wa habari Tanzania Mr Mwambene, kujadili maombi
ya kibali cha GAZETI IMAAN.
Taasisi hio imeshafanya maombi Rasmi ya Gazeti la Imaan Hivyo
inasubiri Majibu ya kupewa leseni, Dua na Michango yenu ni muhimu
sana.
Kwa sasa taasisi hiyo inamiliki Tv Imaan ambayo inapatikana katika satellite dish pamoja na king'amuzi cha startimes katika miji mikubwa yote Tanzania.
Vilevile wanamiliki Radio Imaan ambayo inasikika katika eneo kubwa la Tanzania na baadhi ya maeneo ya nchi jirani.

Tv Imaan
Radio Imaan
Gazeti Imaan.......Inshallah.



 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU