Facebook Comments Box

Tuesday, May 20, 2014

BALOZI AFA AKIWA NA KIMADA

Balozi wa Togo nchini Nigeria amefariki akiwa na kimada. Balozi huyo inasemekana walikuwa wametoka klabu ya usiku na binti huyo na bahati mbaya ndio wakadumbukia baharini na mauti yakawafika.
Wapasha habari wanasema walikuta wawili hao wakiwa wamesema ndani ya maji






MUUGUZI MWENYE HIV AFUNGWA JELA UGANDA

Nchini Uganda mahakama imempata na hatia muuguzi mwenye HIV,
aliyeshitakiwa kwa kumdunga mtoto mchanga sindano, ambayo
awali ilimchoma yeye mwenyewe.
Muunguzi huyo, Rosemary Namubiru, mwenye umri wa miaka 64,
mwathiriwa wa virusi vya HIV, amefungwa miaka mitatu jela, kwa
kile hakimu amekiita, 'uzembe wa weledi'.
Hukumu hio imetolewa wiki moja baada ya bunge la Uganda
kupitisha muswada, unaomtia hatiani mtu yeyote ambaye kusudi
anamuambukiza mtu mwengine virusi vya ukimwi.
Mtoto huyo hata hivyo hakuambukizwa virusi vya HIV na
wanaharakati wamekosoa mahakama kwa kumfunga jela
mwanamke huyo.
Babake mtoto huyo hata hivyo alielezea kufurahishwa na uamuzi wa
mahakama.
Baba huyo, Daniel Mushabe, amesema kuwa anatumai kesi hiyo
itampa motisha Rais Museveni kuidhinisha mswada uliopitishwa na
wabunge wa kuwachukulia hatua za kisheria watu
wanaowaambukiza wengine HIV kusudi.
Adhabu ya kosa hilo ni faini ya dola 1,900 au miaka kumi jela.
Sheria hiyo ikiwa itapitishwa itawaadhibu wanaotenda uhalifu huo
kwa maksudi.
Wananchi bila shaka walionyesha kuudhiwa na kitendo cha muuguzi
huyo ingawa wanaharakati wamemtetea mama muuguzi.
Hakimu aliyetoa hukumu alisema kuwa Namubiru alikosa
kuonekana kama aiyesikitishwa na kosa lake.
Namubiru, muuguzi mwenye uzoefu wa kazi wa miaka 30, alisisitiza
kwamba hana hatia na kuwa mtoto huyo hakuambukizwa HIV.
Namubiru aliamua kumdunga sindano mtoto huyo kutafuta mshipa
lakini kapata ugumu na hivyo kujidunga mwenye kwa bahati mbaya
lakini amesisitiza kuwa hakuwa na nia yoyote ya kumuambukiza
mtoto huyo virusi vya HIV.
CHANZO: BBC SWAHILI


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU