Facebook Comments Box

Friday, February 22, 2013

MBUNGE WA CHADEMA AINGIZWA MJINI KWA KUIBIWA MILION SITA BENK

SAKATA la wizi wa fedha katika akaunti za wateja wa benki, sasa limeingia katika sura mpya baada ya Mbunge wa Biharamulo Magharibi, Dk Gervas Mbasa (Chadema) naye kuibuka na kudai kuwa ameibiwa Sh6 milioni kutoka kwenye akaunti yake. Akizungumzia wizi huo, mbunge huyo alisema fedha zake ziliibwa kwa nyakati tofauti kati ya Desemba 20 mwaka jana na Januari 3, mwaka huu. 
Alisema kitendo hicho kilifanywa na mtu mmoja aliyempigia simu na mtu mmoja aliyejitambulisha kuwa ni mfanyakazi wa Makao Makuu ya Kampuni ya Airtel na kwamba alikuwa katika zoezi la kuhakiki namba zote za zamani.
“Alinieleza kwamba kwa niaba ya Airtel yupo katika zoezi la kuhakiki namba zote zilizosajiliwa zamani na yangu ilikuwa ni ya miaka 10 na akaniuliza namba ya mwisho kuwasiliana na mtu kupitia simu yangu. Nilimtajia namba ya mke wangu na baada ya maelezo hayo aliniomba nisizime simu yangu wakati wakiwa wanashughulika na kuisajili na kwamba muda wowote nitapatiwa maelekezo,” alieleza mbunge huyo.


JCB AFUNGA PINGU ZA MAISHA NA MZUNGU

JCB afunga ndoa na girlfriend wake wa kitambo,Diana
Jorgensen 
ambae kwa sasa wanamtoto mmoja pamoja, huko jijini Arusha


 
Jcb akipitia makaratasi huku mke wake akicheza na pete na maua na mwanae
 
 


Baada ya kufunga ndoa, kinachofata huwa ni picha na hapa ni akiwa na ndugu jamaa na marafiki


PSPF WAONESHA NYUMBA ZAO ZA MKOPO ZILIZOPO BUYUNI - CHANIKA




Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSPF) umekamilisha awamu ya kwanza ya ujenzi wa nyumba 641 katika mikoa mitano ambazo zilianza kuuzwa tangu Novemba mwaka 2012. Mradi huo unalenga kutatua tatizo la makazi kwa wanachama wake na jamii kwa ujumla.

Mikoa iliyojengwa nyumba hizo na idadi ya nyumba katika mabano ni Dar es salaam – Buyuni (491), Morogoro – Lukobe (25), Shinyanga – Ibadakuli (50), Tabora – Usule (25) na Mkoa wa Mtwara – Mang’amba (50).

Aidha kwa Mujibu wa maelezo ya Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa PSPF, Bwana Adam Mayingu amewaambia wanandishi wa habari na viongozi mbalimbali waliotembelea eneo la mradi huo Mkoa wa Dar es Salaam kuwa Shirika lake limejenga nyumba za aina nne ambazo ni za nyumba viwili, Vyumba vitatu, Nyumba za vyumba vitatu kimoja ikiwa ni Master na Nyumba ya vymba vine kimoja kikiwa ni Master.

Gharama ya ununuzi wa nyumba hizo ambazo zinauzwa kwa wanachama wa Mfuko huo ni kati ya Shilingi Milioni 64 hadi milioni 94 gharama zikijumlishwa na Kodi ya ongezejo la Thamani.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSPF) Adam Mayingu (katikati) akiwaonesha maofisa wa Jeshi la Polisi moja ya nyumba 491 zilizopo katika mradi wa ujenzi wa nyumba za gharama nafuu ambazo zitkopeshwa kwa wanachgama wa mfuko huo. Nyumba hizo zipo katika eneo la Kigezi Kata ya Majohe wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSPF) Adam Mayingu (kushoto) akifafanua jambo wakati wa ziara hiyo ya kuakagua makazi hayo. Kulia ni  Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala, Hery Mohamed Kessy Nyumba hizo zipo katika eneo la Kigezi Kata ya Majohe wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam.
 Wadau mbalimbali wakitembelea nyumba hizo hii leo.

 Ziara ikiendelea katika nyumba hizo zipatazo 491




MALKIA WA NYUKI AMLIPA ALIYEKUWA KOCHA WA TIMU YA SIMBA MILOVAN CIRKOVIC


Ushahidi wa cheki aliyopewa Milovan Cirkovic na Malkia wa Nyuki kulipa deni alilokuwa akiidai Simba.


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU