Facebook Comments Box

Wednesday, January 30, 2013

KIWANDA CHA CHEMICOTEX KIMEWAKA MOTO




Kiwanda cha ChemiCotex kilichopo huko Africana njia ya Tegeta jijini Dar es Salaam kimeungua moto jioni ya leo tar 30/01/2013.






IGP MWEMA APATA AJALI MBAYA MOROGORO


                                               IGP SAID MWEMA


Jinamizi la ajali  limeendelea  kuwaandama viongozi  wa  juu  serikali na vyama baada ya  juzi waziri mkuu mstaafu Edward Lowassa kunusurika kifo katika ajali  iliyotokea eneo la Bwawani mkoani Morogoro  ,Mkuu wa jeshi la polisi nchini (IGP )  Said Mwema leo amenusurika  kifo  baada ya gari lake alilokuwa akisafiria  kupinduka.
Ajali  hiyo  imetokea  majira ya mchana katika  eneo Mkundi Manispaa ya Morogoro wakati kiongozi huyo akitokea  jijini Dar es Salaam kwenda mkoani Dodoma.
Hata  hivyo katika ajali  hiyo hakuna madhara makubwa kwa  binadamu zaidi ya gari  kuharibika  kiasi na msafara  wa  IGP kuendelea na safari  ya Dodoma kwa  kutumia usafiri mwingine .


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU