Facebook Comments Box

Thursday, February 7, 2013

HII NDIO HALI MBAYA INAYO WAKABILI WATALII WALIOTAKA KUWEKA HISTORIA YA DUNIA MLIMA KILIMANJARO


???????????????????????????????
Picha ikionesha heliKopta  ikiwa inapeleka chakula na maji kwa waanga walioshindwa kushuka kwa kutumia miamvuli maalum katika mlima kilimanjaro
Marubani waliopanda mlima Kilimanjaro kwa ajili ya kuruka kutoka kileleni kwa kutumia miamvuli maalum wanaendelea kusota baada ya hali mbaya ya hewa kuwazuia kutekeleza azma yao.
Wakiwa wametimiza siku 11 sasa tangu waanze safari yao mlimani, inaripotiwa kuwa hivi sasa wameanza kuishiwa akiba ya chakula na helikopta iliyosheheni maji na shehena nyingine ya vyakula imeruka kwenda kileleni siku ya Jumatano ili kuvidondosha kwa wahanga hao.
Marubani hao zaidi ya 100 walikuwa wanatarajiwa kuruka kutoka kilele cha Mlima Kilimanjaro kwa kutumia miamvuli maalum (Paragliding)na kutua eneo la Kibosho siku ya Jumanne, lakini hadi leo hii (Alhamisi) bado wako mlimani.
Mkuu wa Hifadhi ya Mlima Kilimanjaro Erastus Lufungulo amesema hali ya hewa mlimani hapo bado inaendelea kuchafuka kwa upepo mkali na mawingu mazito.
Marubani hao wa kimataifa, wanatoka nchi mbalimbali duniani, walitarajiwa kuwa binadamu wa kwanza kabisa kuruka kutoka kilele hicho kirefu zaidi barani Afrika.
Helikopta maalum ilitumwa mara kadhaa kuzunguka mlimani kwa siku mbili mfululizo ili kujaribu kuona marubani hao 100 wakiwemo wanawake 30 watakuwa wamefika wapi. Na siku ya jumanne usiku, watu 15 waliokuwa kwenye timu hiyo walirudishwa chini na kukimbizwa hospitali baada ya kuugua.
“Ni kweli zoezi limeshindikana hadi sasa ila hatuna wasiwasi na usalama wa watalii hao kwani tumekwisha kujiandaa kwa huduma zote za uokoaji,” alisema Afisa Habari wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Paschal Shelutete.
Shelutete amesema hii ni mara ya kwanza kabisa tukio hili la kuruka kutoka kilele cha Kilimanjaro kwa kutumia miamvuli kufanyika nchini na kwamba likifanikiwa litajumuishwa kuwa miongoni mwa vivutio vipya vya utalii.
Marubani hao walianza kupanda mlima tarehe 27 Januari na ilitarajiwa kuwa wangeruka kutoka kilele cha Uhuru siku ya tarehe 5, wakielea kutumia miamvuli hiyo maalum, ikiwa ni tukio la kwanza kabisa kufanyika nchini.
Mratibu wa taasisi ya ‘Wings of Kilimanjaro,’ ya Australia, inayoratibu zoezi hilo, Bi Paula McRae amesema zoezi hilo pia litasaidia kuchangia fedha kiasi cha dola millioni moja za kimarekani kwa ajili ya kusaidia jamii zinazounguka mlima huo mrefu zaidi barani Afrika.
DSCF7475
Picha ikionysha mwanamama aliyekuwa katika hali mbaya na kuamua kulala chini huku akimhofia mumewe alipanda mlima mara baada ya kupata taarika kuwa hali ya mlima huo bado ni tete
DSCF7473
Hapa ni baada ya heliKopta kurudi chini ambapo kamera ilifungwa na baadae kuleta hali halisi ya mlima huo …..hapa ndugu jamaa na marafiki wa marubani wakiwa wanaangalia video ya tukio hilo
DSCF7476
DSCF7470
Kikosi kazi cha waandishi wa habari walioweka kambi maalum kuwasubiri watalii kushuka kutoka mlima Kilimanjaro kwa kutimia miamvuli,zoezi ambalo halikuzaa matunda(picha zote na jamiiblog.co.tz)


UGANDA LAUNCHES MANDATORY HIV TESTING

By Francis Kagolo and agencies    

All people who seek treatment in public health centres across the country will undergo mandatory HIV testing under a new plan to increase access to HIV prevention and treatment, the health ministry has announced.


 Under the multimillion dollar programme codenamed 'provider-initiated testing', HIV counseling and testing will be incorporated in the routine medical care, according to Dr. Alex Ario, acting manager of the AIDS Control Programme.

The UN World Health Organization issued guidelines for healthcare provider-initiated counseling and testing in 2007.

In Uganda, mandatory testing was first piloted on expectant mothers attending antenatal care and general patients at regional referral hospitals in 2009.

 However, Ario explained that the system would be rolled out to cover Health Center IVs and IIIs across the country this year. Some private health facilities that receive supplies from the Government will also implement the programme at zero cost to patients.

  "Mandatory HIV testing will now form the many tests conducted when a patient is admitted. It will be part and parcel of our routine medical care practice to let more people know their status to augment HIV prevention and treatment campaigns," said Ario.

 Ario, however, explained that even when the tests are done, patients will not be compelled to know their results.

"Mandatory testing is advantageous to us health workers as well as the patients. It will promote better management of ailments. But this does not mean that patients will not be counseled," he said.

"If a patient is unwilling to know his HIV status on the first visit to the health center, we shall wait when he returns and is ready to receive the results."
Uganda employs a number of testing strategies, including: routine HIV testing for pregnant women; client-initiated counseling and testing; home-based HIV testing; couples HIV testing; mobile HIV testing; and moonlight (night-time) testing for high-risk groups such as sex workers.
According to government statistics, HIV testing is available in 80% of county-level health centres but only 22% of sub-county-level health centres. |

The number of people tested for HIV annually has gone up from 1.1 million in 2008 to 5.5 million in 2011.

The new strategy is part of efforts to lower Uganda's HIV prevalence, which climbed from 6.4 percent to 7.3 percent between 2006 and 2011.

Studies have shown that beyond the benefits of having HIV-positive people identified and referred for treatment, provider-initiated counseling and testing May also result in less risky sexual behaviour, reducing levels of HIV transmission.

"There are so many benefits of knowing their HIV status. Those who are HIV-negative will be careful and avoid engaging in risky behaviours. They will carry out preventive options such as partner notification, abstinence and safer sex," Ario told IRIN/PlusNews.

"Those who are HIV-positive will be enrolled in antiretroviral treatment and have increased opportunities for social support to live normally."

Anti-HIV activists welcomed the start of the new programme, but warned that the government must improve the health system in order to cope with the likely increase in treatment numbers.

"It's a good initiative. It will enable people to guard and take care of themselves. But our health system is struggling. It has not measured up. We have serious shortages of health workers in the health facilities," Florence Buluba, the executive director of the National Community of Women Living with AIDS (NACWOLA), told IRIN.

"The government first needs to address the challenges the health sector is facing before rolling out the programme."


USHAHIDI WA MILOVAN KUJA TANZANIA NA KIASI ANACHO IDAI SIMBA

Milovan kulia akisalimiana na Liewig
Profesa Milovan baada ya kuibuka Taifa

SIMBA SC imesema kwamba haina mpango wa kumrejesha Kocha Mserbia, Profesa Milovan Crikovick na haihusiki na ujio wake hapa nchini.
Msemaji wa klabu ya Simba, Ezekiel Kamwaga amesema leo kwamba, klabu hiyo haihusiki na ujio na Milovan hapa.
Alipoulizwa kuhusu kama ana madai dhidi ya klabu, Kamwaga alikiri lakini akasema hajawataarifu kama anakuja kwa ajili ya madai yake.
"Kulipwa lazima alipwe, lakini hawezi kuja tu ghafla na kutaka alipwe, lazima taratibu zifuatwe,"alisema.
  KITONGONI BLOG inatambua Milovan anawadai Simba SC dola za Kimarekani 24,000 ambazo ni mishahara ya miezi mitatu kabla ya kutupiwa virago Novemba mwaka jana.
Milovan, aliyetimuliwa Simba SC baada ya mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu, jana aliibuka Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam wakati wa mchezo wa kirafiki wa kimataifa kati ya Tanzania na Cameroon na kuteka hadhira.
Profesa Milovan aliwapungia mkono mashabiki wa Simba ambao walimjibu kwa shangwe zito na baadaye Milovan, aliwasalimia baadhi ya wadau na kwenda kuketi kushuhudia mchezo huo. Wakati wa mapumziko, alikwenda kusalimiana na kocha aliyerithi nafasi yake, Mfaransa Patrick Liewig. 
Tayari zilianza kuibuka hisia kwamba, Mserbia huyo anarejeshwa kazini kwa kuwa kocha wa sasa, Mfaransa Patrick Liewig ameingia kwenye mgogoro na wachezaji 'mafaza' wa Simba SC.

BOBAN NA NGASSA KUWEKWA KITI MOTO NA UONGOZI LEO

Mrisho Ngassa

Na Mahmoud Zubeiry
WACHEZAJI wawili tegemeo wa Simba SC, Mrisho Khalfan Ngassa na Haruna Moshi Shaaban, watakuwa na kikao leo saa 5:00 na uongozi wa Simba, kufuatia kesi iliyowasilishwa dhidi yao kwa uongozi na Kocha Mfaransa, Patrick Liewig.
Habari za uhakika, kutoka ndani ya Simba SC, zimesema kwamba, Liewig amewasilisha malalamiko ya kinidhamu dhidi ya wachezaji hao na kuomba uongozi ukutane na wachezaji hao kuzungumza nao, ili wabadilike.
  imefahamika kuwa Simba SC haiko tayari kuwachukuliwa hatua zozote kali wachezaji hao kwa wakati huu, zaidi ya kuzungumza nao na kuwapa mwongozo.
Kikosi cha Simba SC kimeondoka leo asubuhi kwenda Arusha tayari kwa mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara dhidi ya JKT Oljoro Jumamosi kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, lakini Haruna maarufu kama Boban na Ngassa wamebaki kwa ajili ya kikao hicho.
Habari zimesema, wachezaji hao watapanda ndege baada ya kikao hicho kwenda kuungana na wenzao Arusha kwa ajili ya mchezo huo. 
Kumekuwa na habari kwamba wachezaji hao wamesimamishwa kwa utovu wa nidhamu, lakini ukweli ni kwamba hawajasimamishwa na wala uongozi hauna dhamira ya kufanya hivyo kwa kuwa hawana kosa kubwa, zaidi ya kutofautiana na kocha.
Katika kikao cha leo, uongozi utawatajia wachezaji hao kesi iliyowasilishwa dhidi ya na kocha Liewig na kisha kusikiliza utetezi wao, na baada ya hapo watatafuta suluhu.
  inafahamika Simba haiko tayari kuvuruga timu yake kwa sasa zaidi ya kujipanga sawasawa, ili kuhakikisha wanajiimarisha kwenye mbio za kutetea ubingwa wao wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.


SUNZU HATOKUWEPO MECHI YA SIMBA NA JKT OLJORO

UONGOZI wa Klabu ya Simba umethibitisha  kuwa mshambuliaji wa timu hiyo, Felix Sunzu hatokuwamo kwenye msafara wa timu hiyo utakaoelekea Arusha kesho kwa ajili mechi ya ligi dhidi ya JKT Oljoro.
Akizungumza jijini Dar es Salaam msemaji wa Simba, Ezekiel Kamwaga alimesema kuwa Sunzu ameondolewa katika kikosi  kitakachoivaa JKT Oljoro kutokana na kuwa majeruhi.
"Kama tulivyopanga awali kikosi chetu  kitaondoka kesho kuelekea Arusha kikiwa na wachezaji 20.
"Mpaka wakati huu mchezaji ambaye ninaweza kukuthibitishia kwamba hatokuwa miongoni mwa wale watakaosafiri ni Felix Sunzu ambaye bado anasumbuliwa na majeraha,".alisema Kamwaga.
Kamwaga alisema kuwa, orodha kamili ya wachezaji 20 watakaosafiri kuelekea Arusha ilitarajiwa kutangazwa mapema baada ya kumalizika kwa pambano kati ya Timu ya Taifa(Taifa Stars) na Cameroon leo jioni.
"Nani na nani watakuwamo katika kikosi kitakachosafiri itajulikana leo jionibaada ya mechi kati ya Taifa Stars na Cameroon kama unavyojua tuna wachezaji kwenye timu ya Taifa. Hatuwezi kujua kuna nini kitatokea baada ya mchezo,".alisema Kamwaga.
Pambano baina ya Simba na JKT  litapigwa Jumamosi hii kwenye Dimba la Sheikh Amri Abeid jijini Arusha.
Katika pambano la mzunguko wa kwanza  lililopigwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, Wekundu wa Msimbazi, Simba ilichomoza na ushindi wa mabao 4-1


DR SLAA AUNGURUMA KUTETEA WABUNGE WAKE




VIJANA KIGOMA WAMALIZA MAFUNZO YA JKT


Mkuu wa mkoa kigoma Issa Machibya (Mwenye suti)  akikagua mafunzo kwa vitendo ya vijana wanaomaliza mafunzo ya kujitolewa ya JKT katika kambi ya JKT Kanembwa wilayani Kibondo mkoani Kigoma
Baadhi ya vijana wanaomaliza mafunzo ya kujitolea katika kambi ya JKT Kanembwa wilaya ya Kakonko mkoani Kigoma wakisikiliza hotuba iliyokuwa ikitolewa na mkuu wa mkoa kigoma Issa Machibya (hayupo pichani) wakati wa hafla ya kufunga mafunzo hayo



 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU