Facebook Comments Box

Tuesday, October 28, 2014

AJALI KONA YA JETI: LORI LAIANGUKIA HIACE


Kumetokea ajali mbaya mida hii maeneo ya Jeti Lumo mwisho wa lami ambapo gari kubwa la mizigo limeangua daladala iliyokuwa kituoni.


Ajali hiyo imetokea wakati gari hilo semi-trailer ikikata kona pale mwisho wa lami ambapo kontena lilianguka na kutua juu ya bodi ya daladala.


Mtoa taarifa wangu amesema hali ni mbaya na bado hajajua idadi ya vifo na majeruhi ujumla.Pia gari imepondeka sana jambo ambalo linaashiria hatari zaidi.


Kuna gari la kunyanyua makontena limeshafika pale lakini limeshindwa kutoa msaada wa uhakika kutokana na kuzidiwa uzito na kontena ambapo likijaribu kunyanyua kontena ushuka.

Hamna mtu yoyote aliepoteza maisha maana Hiace hiyo ilikuwa imepaki kusubiri muda wake wa kupakia abiria.



ABUBAKAR SALUM "SURE BOY" ACHAGULIWA MCHEZAJI BORA WA OKTOBA



Bodi ya ligi kuu soka Tanzania bara TPL Bord imemtangaza mchezaji  wa Azam FC Salum Abubakar  ‘Sure  Boy’ kuwa mchezaji bora wa mwezi oktoba katika ligi kuu soka Tanzania Bara.

Akizungumza leo Jijini Dar es Salaam kwa niaba ya Bodi ya ligi, Mkurugenzi wa Masindano wa TFF Boniface Wambura amesema mchezaji uyo amechaguliwa baada ya kuwasinda kwa vigezo wachezaji wenzake katika michezo ya mwezi  uu wa oktoba.
Mwezi  uliopita  mchezaji  wa Mbeya City Antony Matogolo aliibuka  mchezaji bora wa  mwezi  septemba na kuambulia  kitita cha shilingi milioni moja.


NAHODHA NA GOLIKIPA WA AFRIKA KUSINI AUAWA NCHINI HUMO



Nahodha na golikipa wa timu ya Taifa la Afrika kusini Senzo Meyiwa enzi za uhai wake.

Nahodha na golikipa wa timu ya Taifa la Afrika kusini Senzo Meyiwa amefariki dunia baada ya kupigwa risasi. Jeshi la polisi la nchi hiyo limesema. Tukio hilo limeripotiwa kutokea katika nyumba ya mpenzi wake iliyopo katika mji wa Vosloorus kusini mwa Johannesburg.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 aliichezea klabu ya Orlando Pirates na alicheza mechi nne zilizopita za timu yake ya taifa katika mechi za kufuzu za fainali ya mataifa ya Afrika.

Jumamosi alikuwepo katika tukio la timu yake pindi waliposonga mbele katika nusu fainali ya ligi ya Afrika kusini.
Katika maelezo yake Jeshi la polisi la afrika kusini limesema kwamba Meyiwa ameripotiwa kufariki wakati akiwasili hospitalini.

Chanzo: BBC

 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU