Facebook Comments Box

Thursday, January 1, 2015

NAULI ZA TRENI ZAPANDA BAADA YA KUWASILI MABEHEWA PAMOJA NA VICHWA VIPYA

Mabehewa Mapya yakishushwa bandarini baada ya kuwasili nchini tayari kwa safari.
Moja wapo ya behewa jipya kama linavyoonekana kwa ndani hapo ni kitanda katika behewa la kulala.
Moja wapo ya behewa jipya kama linavyoonekana kwa ndani sehemu ya kukaa abiria
Moja wapo ya behewa la zamani katika muonekano wa ndani abiria wakiwa wamekaa tayari kwa safari.
Treni ya Zamani ikiwa ndo inaanza safari yake ya kwenda Kigoma, Tabora na Mwanza.

Mamlaka ya huduma za usafiri wa nchi kavu na majini SUMATRA imekutana na wadau wa usafiri wa reli mjini Dar es salaam, lengo likiwa ni kupokea na kujadili mapendekezo ya nauli ya huduma mpya ya usafiri huo, unaotarajiwa kuanza katikati ya mwezi Januari 2015, baada ya shirika la reli TRA kupokea mabehewa mapya na vichwa ambapo itafanya safari zake kutoka Dar es salaam, Mwanza na Kigoma.

Usafiri huo mpya utakuwa katika madaraja matatu(3) ambapo behewa la daraja la pili likiwemo lenye vitanda litakuwa na vyumba 6 kila behewa ambapo kila chumba kitakuwa na abiria 6 na kufanya jumla ya abiria katika behewa moja kuwa 36.

Aidha daraja la pili lingine litakuwa na mabehewa yenye viti ambavyo vitachukuwa abiria 60 na daraja la tatu litakuwa na mabehewa yenye uwezo wa kuchukuwa abiria 80 kila behewa wakiwa wamekaa.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano huo Mkurugenzi Mkuu wa (SUMATRA) Giriad Gewe, amesema mapendekezo hayo yatazingatia vigezo muhimu ambavyo vitalinda maslahi ya pande zote mbili (Mtoa huduma na Mtumiaji).

Zikiwemo gharama za uwendeshaji na viwango vya ushindani na kuahidi kuwa baada ya siku 14 SUMATRA itakuwa na maamuzi ambayo yameridhiwa.

Nae Mkuu wa Masoko wa TRL Bwana Charles Ndege amesema kuanzishwa kwa huduma kutaimarisha uwezo katika utendaji wa shirika hilo kwa kuongeza utoaji wa huduma hadi kufikia mara tatu kwa wiki ikilinganishwa na awali ambapo imekuwa ikitoa huduma mara mbili kwa wiki.

Aidha huduma hiyo itaendana na wakati kwa kuwapunguzia safari ndefu wasafiri hususan wafanya biashara kwa kuwa na vituo 14 kwa safari nzima badala ya 54 vya awali.

Bwana Ndege amesema Nauli ya kutoka Dar es salaam mpaka Mwanza itakuwa ni 76,400/= kwa daraja la pili kulala, na Shilingi 44,400/= kwa daraja la pili kukaa, huku shilingi 38,100/= kwa daraja la tatu kukaa.

Treni hiyo ambayo haitaruhusu abiria kusimama itakuwa na uwezo wa kubeba abiria wapatao 800 daraja la tatu, 360 daraja la pili kukaa na abiria 200 wa daraja la pili kulala na itakuwa na behewa moja kwa ajili ya maakuli na viburudisho.

Baadhi ya wadau wameelezea kutoridhishwa na viwango hivyo vya nauli kwa madai kwamba vipo juu na kuboresha huduma ya mabehewa na vichwa haitakuwa na maana endapo miundo mbinu yake bado itakuwa ni ya zamani na isiyokuwa na uhakika kwa usafiri.

Afisa elimu wa SUMATRA Bwana Nicolas Kinyariri alitoa maoni kwa niaba ya SUMATRA kuwa: 
  1. Nauli zilizo wasilishwa hazija zingatia hali halisi ya usafiri wa Tanzania ya leo na Tanzania ya kesho,Nauli za Treni za abiria zinapaswa kuwa nafuu sana zikilinganishwa na usafiri wa mabasi.
  2. Baraza linashauriwa kwamba TRL waendelee na nauli zilizopo ambazo zinaweza kuhimili ushindani na nauli za mabasi japo kwa miezi siat (6) kushawishi abiria kuwa huduma zimebadilika
Nae Mkurugenzi Mkuu wa SUMATRA Bwana Giriad Gewe amesema nauli hizo zinaweza kubadilika kutokana na maoni ya wadau hivyo amepongeza ujio mpya wa TRL kwani utaweza kuleta mabadiliko katika sekta ya usafirishaji ikiwemo kupunguza ajali za barabarani zinazo sababishwa na mabasi.




SIMBA NA MTIBWA, YANGA NA VILLA, AZAM NA KCC-KOMBE LA MAPINDUZI

 Uwanja wa Aman Zanzibar baada ya kuwekewa nyasi bandia

Timu za Yanga, Simba,Azam,Mtibwa Sugar kutoka Tanzania Bara na KCC, na Sport Club Villa zote kutoka Uganda, zitakuwa katika mshikemshike wa kombe la mapinduzi kuanzia leo Tarehe 01-01-2015 katika uwanja wa Aman-Zanzibar.

Timu za Zanzibar zitakazoshiriki michuano hiyo KMKM, Mtende Ranger, Shaba,Polisi,JKU na Mafunzo kutoka Zanzibar. Ameyataja makundi na timu zake.

 Alhamis 1 Januari 2015 

Jioni Saa 9:00      JKU vs MAFUNZO.  --         KUNDI.      C

Jioni Saa.11:00.   POLISI VS SHABA.              KUNDI .     A

Usiku Saa 2:15.     SIMBA VS MTIBWA.          KUNDI       C


Ijumaa 2 Jan 2015 
Jioni saa 10:00  KMKM VS MTENDE           KUNDI           B

Usiku Saa 2:00 KCC VS AZAM.                        KUNDI          B


Jumamosi 3Jan 2015.
Jioni Saa 10:00 JKU VS MTIBWA                  KUNDI       C

Usiku Saa 2:00 YANGA VS SC.VILLA             KUNDI      A

Jumapili  4 Jan 2015                        

Jioni saa 9:00 KCC VS MTENDE                        KUNDI    B

Jioni saa 11:00 KMK VS AZAM.                          KUNDI    B

Usiku saa 2:15. MAFUNZO VS SIMBA                KUNDI    C


Jumatatu 5 Jan 2015                  

Jioni saa 10;00 SC VILLA VS SHABA               KUNDI    A

Usiku saa 2:00 YANGA VS POLISI                     KUNDI    A


Jumanne 6 Jan 2015

Jioni saa 9:00 AZAM VS MTENDE                   KUNDI     B

Jioni saa 11: 00  MTIBWA VS MAFUNZO        KUNDI     C

Usiku saa 2:15. SIMBA VS JKU                           KUNDI    C


Jumatano 7 Jan 2015

Jioni saa 9;00  POLISI VS SC VILLA                KUNDI      A

Jioni saa 11:00  KCC VS KMKM                         KUNDI     B

Usiku saa 2:15. YANGA VS SHABA                  KUNDI      A


Alhamisin 8 Jan 2015.

Jioni saa 10:00  WINNER B VS RUNNERS  A.

Usiku saa 2:00 WINNER  A VS BEST LOOSER 1


Ijumaa 9 Jan 2015

Jioni saa 11:00 WINNER C VS BEST LOOSER 2

Usiku saa 2;00 RUNNERS  B VS RUNNERS C.


Jumapili 11 Jan 2015.
SEMIFINAL 1 
Jioni saa 10:00. WINNER 1 VS WINNER 2

SEMIFANAL 2

Usiku saa 2:00  WINNER  3 VS WINNER 4


Tarehe 13/1/2015 itakuwa fainali ya michuano hiyo itakayofanyika usiku katika uwanja wa amaan Zanzibar. kuhitimisha michuano hiyo.

 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU