Facebook Comments Box

Wednesday, September 10, 2014

COUTINHO HATIHATI KUIKOSA AZAM MECHI YA NGAO YA HISANI


kitongoni loyola:
Timu ya Yanga ya Jijini Dar es Salaam imegawana point na Polisi ya Dar es Salaam pia pale zilipotoka suluhu bin suluhu katika mtanange wa kirafiki uliofanyika leo asubuhi katika uwanja wa shule ya sekondari Loyola ambao ndiyo uwanja wa mazoezi wa timu ya Yanga.

Mpambano huo uliokuwa mzuri na wa kasi kutokana na timu zote mbili kutumia sana viungo ambapo kwa upande wa wenyeji Yanga Mrisho Ngassa na Coutinho waling'ara sana.

 Coutinho

katika dakika ya 14 tu ya mchezo, mshambuliaji wa timu ya Polisi alikosa goli la wazi akiwa ana kwa ana na mlinda mlango wa Yanga Juma Kaseja ambaye aliucheza mpira huo kwa mguu.

Mpira huo uliingia dosari katika dakika ya 20 ya mchezo wakati Coutinho alipoumia na kutolewa nje na kuzua hofu kubwa kwa Viongozi, wachezaji pamoja na mashabiki wa timu hiyo kuona kuwa anaweza kukosa mchezo wa ufunguzi wa Ligi kuu ya Vodacom kati ya Yanga na Azam ambao unataraji kufanyika tarehe 14 septemba, 2014 siku ya jumapili.

Kwani hata kuondoka kwake hapo uwanjani mchezaji huyo alipewa msaada mkubwa na Daktari wa timu yake aliyekuwa amemshikilia begani na kuacha maswali mengi hasa kuhusu mchezo huo.



SAMSUNG YAZINDUA SIMU MPYA NI "SAMSUNG GALAXY NOTE EDGE" HEBU IONE HAPA

Haya tena wale wapenzi wa teknolojia,Samsung wamezindua flagship yao kutoka familia ya Galaxy note amabayo inakwenda kwa jina la Samsung Galaxy Note edge.

Simu hii ina kioo kilichojikunja tofauti na flat screen tulizozoea, kwa sasa hii ndio highest end phone kutoka Samsung.



Note Edge ina sifa zifuatazo:

Inaelekea kufanana kiasi Note 4. Yenyewe ina metallic design, It has the same soft-touch back, blissfully without the fake stitching. Ina kamera yenye 16-megapixel, heart-rate monitor, processor, memory, software, Multi Window feature, kila kitu kama ndugu yake note 4.



Kwa sasa hii ndio simu kutoka samsung yenye nguvu kuliko simu zote.

Ina Quad HD, 2560 x 1440 display kama kwenye Note 4, Ila hii kioo chake ni kidogo kidooogo ambayo ni inchi 5.6 tofauti na 5.7 ya note 4.


WAKAZI WA BAGAMOYO NA MAENEO YA JIRANI KUKWEPA FOLENI BAADA YA KIVUKO CHA MV DAR ES SALAAM KUKAMILIKA



Kivuko kipya cha Mv Dar es salaam ambacho kinataraji kutoa huduma zake kati ya Dar es salaam na Wilaya ya Bagamoyo Mkoani Pwani tayari kimekamilika.

Taarifa za kivuko hicho zilitolewa jana na Waziri wa Ujenzi Dkt. John Pombe Magufuli kuwa kivuko kimekamilika nchini Denmark na kimeisha shushwa kwenye maji tayari kuanza safari ya kuja Dar es salaam ili kazi ianze ambapo kinatarajiwa kufika kati ya wiki tatu au nne hivi. 

Kivuko hicho kitakuwa na kasi kuliko kivuko chochote Afrika Mashariki.




 



SOMA MAGAZETI YA LEO JUMATANO TAREHE 10/09/2014 HAPA

1_2f86a.jpg
2_5bc9d.jpg
3_725a3.jpg
4_35de4.jpg
5_102d4.jpg
6_64d98.jpg


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU