Facebook Comments Box

Wednesday, April 23, 2014

JE, HUU NDIO MWISHO WA WENGER ARSENAL?


Baada ya Manchester United kumfungashia virago kocha wao fununu,tetesi,masikio na macho yote yamehamia  kwa washika bunduki wa London

Wengi wanasema kuwa huu ndio mwisho wa enzi za mzee huyo hapo kilabuni

Baada ya Moyes kuachia ngazi,kocha
anayetajwa sana kurithi mikoba yake ni
boss wa timu ya taifa ya Uholanzi Luis
van Gal. 
Lakini Van
Gal amehusishwa kuhamia Arsenal na
gazeti moja maarufu la kwao uholanzi
liitwalo Vuetbal international state kwa
kutaja sababu kadhaa.

1:Wenger amebakiza wiki 6 tu katika
mkataba wake wa sasa na hajaongeza
bado.

2:Arsenal imemuajiri aliyekuwa msaidizi
wa Van Gal walipokuwa Bayern
Munich. Adries Jonker kama Director
of academy. (Mkurugenzi wa vipaji) hili likitafsiriwa kama
matayarisho ya ujio wa Van Gal.

3:Kama hilo halitoshi,Arsenal pia
imeshawaajiri makocha wadachi wa
vijana wa miaka chini ya 18 na 16 wanaoitwa Jans de kaart
na Luis van Hoon. Kitu
kinachotafsiriwa kwamba ni maandalizi
ya kumnyakua kocha mkuu mdachi.




WANASAYANSI WAGUNDUA MIWANI INAYOGUNDUA MIHEMKO YA MTU.

Mwanasayansi nchini Japan anaitwa Osawa amegundua miwani ambayo imeitwa miwani ya kipelelezi "AgencyGlass"

Wakati akifanya mahojiano na shirika la habari la AFP amesema kuwa "nilikuwa nataka kutengeneza kitu ambacho kitaeleza tabia halisi za kijamii za binaadamu"


organic light-emitting diode (OLED) ambayo imewekwa kwenye miwani hiyo inaunganishwa na kifaa cha kugundua mihemko "emotion" ambacho kimewekwa nyuma kidogo ya miwani hiyo

Mwanasayansi huyo ambae anafanya kazi katika chuo kikuu cha Tsukuba anasem. miwani hiyo itasaidia kugundua wasafiri wakorofi au wanafunzi wakorofi na sehemu ya kazi ambapo mahusiano sio  mazuri

Miwani hiyo ina uzito wa gram 100 na inauzwa  kwa dollar za kimarekani 290.





AKUTWA NA VIPANDE 12 VYA DHAHABU TUMBONI.

Madaktari nchini India wamepatwa na mchangao baada ya kukuta vipande 12 vya dhahabu katika tumbo la mgonjwa ambae alikuja na maumivu ya tumbo.

Dr  C.S. Ramachandran anasema kuwa mgonjwa huyo alikuja na maumivu ya tumbo na akasema kuwa alimeza mfuniko wa chupa

Dr C.S Ramachandran alikataa kuweka wazi jina la mgonjwa ila vipande hivyo vya dhahabu wamevikabidhi polisi

Nae afisa wa polisi anasema vipande hivyo vitakuwa vimeibiwa na wanafanya uchunguzi.

Kila kipande cha dhahabu kilicho kutwa tumboni lilikuwa na uzito wa gram 33.



 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU