Facebook Comments Box

Thursday, August 22, 2013

SERIKALI YA WASIMAMISHA KAZI NA KUWAVUA MADARAKA MAAFISA WA JESHI LA POLISI

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Waziri Nchimbi amesema hatua hiyo ni katika kuendeleza vita ya kuhakikisha kuwa jeshi la polisi linakuwa na nidhamu, linatekeleza wajibu wake wa kutenda haki na kuwalinda raia na mali zao.

Waziri Nchimbi aliwataja waliovuliwa madaraka kuwa ni Mkuu wa kikosi cha kutuliza ghasia mkoani Arusha Mrakibu wa Polisi Ramadhan Giro, Mkuu wa Upelelezi wilaya ya Mvomero mkoani Morogoro Inspekta Jamal Ramadhan, Mkuu wa Kituo cha Polisi cha Dumila Inspekta Juma Mpamba na mkuu wa upelelezi wa wilaya ya Kasulu ASP Daniel Bendarugaho na kumsimamisha kazi Inspekta Isaack Manoni.

Alifafanua kuwa Mrakibu wa Polisi Ramadhan Giro alivuliwa madaraka kwa kushindwa kusimamia kikamilifu askari na maafisa walio chini yake ambao walikamatwa wakisafirisha bangi yenye uzito wa kilogramu 540 kwa kutumia gari la polisi. Alisema askari hao wawili waliokamatwa wakisafirisha bangi, walikuwa wakifanya kazi kwenye kituo cha Ngarananyuki na baada ya kukiri kosa walifukuzwa kazi mwezi Mei mwaka huu.

Alisema kwa upande wa Inspekta Jamal Ramadhan amevuliwa madaraka yake kwa kutochukua hatua stahiki baada ya kupata taarifa za mfanyabiashara wa Mvomero Samson Mwita kubambikiwa fuvu la kichwa cha binadamu na askari polisi watatu wakishirikiana na matapeli wawili. “Katika tukio hilo Inspekta Isaack Manoni amesimamishwa kazi na atashtakiwa kijeshi kutokana na tuhuma za kumtorosha mtuhumiwa, Cpl. Edward aliyekuwa dereva wa gari la Polisi lililokamatwa na bangi kitendo ambacho kimelifedhehesha jeshi la polisi” alisema Waziri Nchimbi.

Alibainisha kuwa Inspekta Juma Mpamba amevuliwa madaraka hayo kwa kuonesha udhaifu katika utendaji wake wa kazi kwa kutosimamia kikamilifu askari walio chini yake kitendo kilichosababisha askari kujipangia kazi nje ya utaratibu na kumbambikiza mfanyabiasha huyo kesi kwa lengo la kujinufaisha kinyume na maadili ya kazi. Aliongeza kuwa askari waliohusika na tukio hilo wamefukuzwa kazi na kushtakiwa. Waziri Nchimbi alisema ASP Daniel Bendarugaho amevuliwa madaraka kwa kutokuwa makini katika kufanya na kusimamia upelelezi wa kesi ya mauaji ya marehemu Gasper Mussa Sigwavumba aliyeuawa baada ya kupigwa na askari polisi wawili Desemba mwaka jana.

Alisema upelelezi mbovu uliofanywa chini ya usimamizi wa Mkuu huyo wa upelelezi ulisababisha kesi hiyo kuondolewa mahakamani. Aliongeza kuwa upelelezi wa kesi hiyo utaanza upya ili haki itendeke.


KITUO CHA MABASI YA KUTOKA DAR KWENDA MIKOANI KUJENGWA MBEZI LUIS NA BASIHAYA: JIJI







TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI:

Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam itajenga vituo vya mabasi yaendayo mikoani na nchi za jirani katika maeneo ya Mbezi Luis na Boko-Basihaya. Ujenzi wa vituo hivyo ni utekelezaji wa mipango ya Jiji ya kuimarisha huduma za usafiri Dar es Salaam.

Kituo cha Mbezi Luis kitahudumia wasafiri wa Kanda ya Kati na Nyanda za Juu wakati Kituo cha Boko Basihaya kitatoa huduma kwa wasafiri wa Kanda ya Kaskazini. Kwa Kanda ya Kusini Halmashauri ya Jiji itajenga Kituo cha Mabasi Kongowe.

Kituo kitakachoanza kujengwa ni Mbezi Luis ambacho kitajengwa sambamba na Boko Basihaya. Kituo Kikuu cha Mabasi Ubungo kimepangwa kutoa huduma ya usafiri wa mabasi yaendayo haraka kwa wasafiri wote watakaokuwa wakitumia vituo hivyo vya mabasi yaendayo mikoani. Ujenzi wa vituo vya Mbezi Luis na
 Boko Basihaya, kutokana na upembuzi yakinifu wa awali, unakadiriwa kugharimu kiasi cha shilingi bilioni 40 kwa kila kituo.

Ujenzi wa vituo hivyo unahitaji upembuzi yakinifu wa kina kwa lengo la kupata gharama halisi za utekelezaji wake, kubaini vyanzo vya fedha na kuangalia uwezekano wa kuzishirikisha taasisi mbalimbali za fedha na wawekezaji wanaoonyesha nia ya kushirikiana na Halmashauri ya Jiji katika ujenzi wa vituo hivyo ambavyo vitakapokamilika vitakuwa pia ni chanzo cha ajira kwa wananchi.

Katika kipindi hiki cha maandalizi ya ujenzi wa vituo hivyo, bado Kituo Kikuu cha Mabasi Ubungo (UBT) kitaendelea kutoa huduma kwa wasafiri waendao mikoani na nchi za jirani. Halmashauri ya Jiji inapenda wananchi wafahamu kwamba UBT,

 kama ilivyopangwa na Serikali, itakuwa ni kituo kitakachotoa huduma ya usafiri wa Mabasi Yaendayo Haraka(Dar Rapid Transit-DART) baada ya kukamilika kwa ujenzi wa miundombinu yake. Pamoja na hilo Halmashauri ya Jiji pia itajenga “shopping malls” na hoteli katika kituo hicho cha UBT

Kukamilika kwa ujenzi wa vituo hivyo vya mabasi ni mafanikio makubwa katika jitihada za serikali za kuimarisha huduma za usafiri katika Jiji la Dar es Salaam. Wadau wa maendeleo katika sekta hii, wananchi na taasisi mbalimbali wanategemewa kuendelea kutoa mapendekezo yao ya kuimarisha huduma za usafiri Dar es Salaam.

DIAMOND PLATNUMS AELEZEA KASHFA YAKE YA MADAWA YA KULEVYA TAZAMA ALICHO KISEMA



Msanii Wa Muziki wa Bongofleva mwenye jina kubwa mjini na mwenye Mkwanja mkubwa hapa nchini Naseeb Abdulmaliki “Diamond Platnumz” amejitokeza na kukanusha kuwa hahusiki na biashara ya madawa ya kulevya.
 
Kwa muda mrefu sasa kumekuwa na taarifa za Diamond kujihusisha na biashara hiyo hasa kutokana na ukaribu wake na wafanyabiashara wakubwa wa dawa za kulevya wenye maskani yao nchini Afrika Kusini.

 
Taarifa zaidi zinasema ni wafanyabiashara hao waliohusika kwa karibu kuusafirisha mwili wa marehemu Albert Mangwair, aliyefia huko huko Afrika Kusini ambaye taarifa za kifo chake ziligubikwa na matumizi ya madawa ya kulevya.

Akikanusha taarifa hizo Diamond amesema “Ni kweli mimi nina pesa za kutosha kuniwezesha kuishi maisha ninayotaka lakini sijawahi kujihusisha na biashara hiyo.

"Kufanya kazi kwa bidii kunalipa na kazi yangu inaonekana na ndiyo inayoniwezesha kuwa na fedha ambazo leo watu wameanza kuzitilia shaka. Sielewi nia ya watu hawa ni nini?”

Taarifa za Diamond kuhusishwa na mtandao huu zimeanza kushika kasi kufuatia miongoni mwa watu wake wa karibu kuonekana wakiwa karibu sana na akina Agnes Gerald “Masogange” (25) na Melisa Edward (24) kwenye uwanja wa kimataifa wa ndege wa Mwalimu JK Nyerere wa Dar es Salaam kabla hawajapanda ndege kuelekea Afrika Kusini ambako walikamatwa.


RAISI JAKAYA KIKWETE AFANYA MABADILIKO YA MAKATIBU WAKUU WA WIZARA MBALIMBALI


Katibu Mkuu Kiongozi, Mhe. Balozi Ombeni Y. Sefue akiongea  na Waandishi wa Habari waliojikusanya jioni hii kuhusu Uteuzi wa Makatibu Wakuu na Manaibu Katibu Wakuu Wapya, jijini Dar es Salaam. Pembeni kushoto ni Bw. Salvatore Rweyemamu, Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu.

Baadhi ya walioteuliwa:
Dr Florence Turuka - Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu
Bi Joyce Mapunjo -Katibu Mkuu wizara ya Afrika Mashariki
Bw Sihaba Mkinga -Katibu Mkuu -Habari, Michezo na Utamaduni
Bi Sofia Kaduma -Katibu Mkuu Kilimo na Ushirika
Dr Deo Mtasiwa -Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu akishughulikia Afya

Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardh Nyumba na Maendeleo ya Makazi Bw Patrick Rutabanzibwa Amestaafu kwa hiari.
Wafuatao wameondolewa Ukatibu Mkuu na badala yake watapangiwa kazi nyingine:

1. Seth Kamuhanda
2. Kijakazi Mtengwa
3. Omary Chambo

Bw Peniel Lyimo aliyekuwa Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu amehamishiwa Ofisi ya Rais kuwa Naibu Mtendaji Mkuu Kitengo cha PDU akishughulikia maswala ya Kilimo

  Orodha kamili ya walioteuliwa ni:
Jumanne Sagini amekuwa Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu- Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) awali alikuwa Naibu Katibu Ofisi wa Waziri Mkuu - TAMISEMI. Dk. Servacius Likwalile amekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Fedha,awali alikuwa Naibu Katibu.
Dk. Patrick Makungu- Katibu Mkuu wa Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, awali alikuwa Naibu Katibu Mkuu katika wizara hiyo.

Alphayo Kitanda- Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi ,Nyumba na Maendeleo ya Makazi, awali alikuwa Naibu Katibu Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI. Dk. Shaaban Mwinjaka - Katibu Mkuu Wizara ya Uchukuzi,awali alikuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Masoko, Dk.Uledi Mussa-Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Masoko, awali alikuwa Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki. 

Profesa Sifuni Mchome- Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, awali alikuwa Katibu Mtendaji Mkuu wa Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania. Charles Pallangyo - Katibu Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, awali alikuwa Naibu Katibu Mkuu, Anna Maembe -Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto, awali alikuwa Naibu Katibu Mkuu wizara hiyo, Sihaba Nkinga- Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, awali alikuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara hiyo, Sophia Kaduma- Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika, awali alikuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo.

Naibu makatibu wakuu wapya walioteuliwa ni:
Angelina Madete- Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira, Regina Kikuli -Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Zuberi Sumataba -Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI anayeshughulikia suala la elimu, Edwin Kiliba -Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu - TAMISEMI.

Dk. Yamungu Kayandabila -Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika, Profesa Adolf Mkenda -Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha anayeshughulikia sera, Dorothy Mwanyika -Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha anayeshughulikia Fedha za Nje na Madeni. Rose Shelukindo -Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, 

Dk. Selassie Mayunga -Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi ,Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Monica Mwamunyange -Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Uchukuzi, Consolata Mgimba -Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi. Profesa Elisante ole Gabriel Laizer -Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Armantius Msole -Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki.
Waliopewa uhamisho kuwa ni:
John Mngondo amehamishiwa  Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia ametoka Wizara ya Uchukuzi, Selestine Gesimba - Wizara ya Maliasili na Utalii anatoka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Injinia Ngosi Mwihava anahamia Wizara ya Nishati na Madini kutokea Ofisi ya Makamu wa Rais.

Maria Bilia -Wizara ya Viwanda na Biashara kutoka Wizara ya Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Nuru Milao anahamia Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii.
Hiyo ndio orodha yote ya walioteiuliwa, kuhamishwa na kuacha kazi.


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU