Facebook Comments Box

Friday, September 7, 2012

MWANAJESHI ALIEANDIKA KITABU CHA MAUAJI YA OSAMA NDIO HUYU

.
Wizara ya usalama ya Marekani (Pentagon) imetishia kumpeleka mahakamani mwanajeshi alieandika kitabu kuhusu jinsi yeye na wenzake walivyomuua gaidi Osama Bin Laden aliekua kiongozi wa Al Qaeda.
Mwanajeshi huyo aliekua kwenye kundi la wanajeshi wenye ujuzi wa hali ya juu alikua mtu wa pili kuingia chumbani alipokuepo Osama ambapo kwenye kitabu alichoandika anaeleza kwamba Osama hakua na silaha yoyote walivoingia chumbani kwake, taarifa ambayo inatofautiana na iliyotolewa na Pentagon.
Kanuni zinazoongoza oparesheni kama iliyomuua Osama zinawanyima wanajeshi waliohusika kutoa siri au kutangaza chochote ndio maana anaonekana kavunja makubaliano.
Sasa hivi vyombo vya habari vimeanza kuhusisha hicho kitabu na kampeni za urais jambo ambalo mwanajeshi huyo amelikataa na kusisitiza kwamba amekiandika hicho kitabu ili kuweka hadharani ukweli bila kulenga chama chochote cha siasa wala mgombea.
Matt Bissonnette(36) ambae hafurahii uongozi wa rais Obama, alikua hataki kutambuliwa kwenye vyombo vya habari lakini tayari jina lake limeshajulikana na limesambaa hivyo ilimlazimu kujificha.

MAANDAMANO YA WAISLAM DAR ES SALAAM



Wananchi wakiandamana karibu na maeneo ya ofisi za mkuu wa mkoa wa Dar es salaam. Wakielekea wizara ya mambo ya ndani wakishinikiza waislam wote walioshikiliwa kwa ajili ya kukataa sensa waachiwe. Wizara ya mambo ya ndani imetoa tamko waislam wote walioshikiliwa kwa ajili ya kukataa sensa waachiwe huru. Waslam hao wameondoka \Wizara ya mambo ya ndani na kuelekea msikiti wa kichangani ili kuwasiliana na wailam tanzania nzima kujua kama wote wameachiwa.

JIVUNZE KUFUNGA TAI

Watu wengi wamekuwa wakipenda kuvaa tai ila hawajui jinsi ya kufunga tai. Tumeamua leo kuweka picha hii inayokuonesha namna mbalimbali za ufungaji wa tai

KITUKO NA KATUNI YETU YA LEO





JESHI LA POLISI MSILIFUMBIE MACHO HILI

 Pamoja na kampeni ya jeshi la Polisi la Tanzania ya utii wa sheria bila shurti kumekuwa na uvunjwaji wa makusudi wa sheria kama basi hili litokalo Korogwe mjini kwenda Korogwe vijijini (magamba kwalukonge) likiwa limepakia abiria mpaka kwenye sehemu ya mizigo. Jeshi la polisi msilifumbie macho hili.








 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU