Facebook Comments Box

Friday, August 31, 2012

USAJILI SIKU YA MWISHO NA WALIO KAMILISHA USAJILI


Hatimaye Dimitar Berbatov amehamia rasmi Fulham kutoka Manchester United kwa ada ya £5million

Mchezaji wa kimataifa wa Brazil Douglas Maicon amesajiliwa kutoka Inter Milan kwenda Manchester City

Charlie Adam amejiunga na Stoke City City akitokea Liverpool kwa ada ya £4MILLION



Andy Carroll amejiunga na West Ham kwa mkopo wa mwaka mzima

Rafael Van Der Vaart amejiunga na Schalke akitokea Tottenham Hotspur

Pablo Hernandez amejiunga na Swansea City akitokea Valencia ya Spain

Scott Sinclair amekamilisha uhamisho wake kutoka Swansea na kuhamia kwa mabingwa wa England Man City

Nicklas Bendtner amehama Arsenal na kwenda kujiunga na Juventus ya Italia


NI KWELI MICHAEL ESSIEN ANAENDA ARSENAL?

Kuna uvumi umezagaa ndani ya jiji la London kuwa Michael Essien anahitajika Arsenal kwa mkopo. Yamebaki masaa kadhaa ili kumalizika muda wa usajili. Tusubiri hadi mwisho tuone jembe hili litaenda kwa washika bunduki.

HATIMAE TFF WATOA RATIBA YA LIGI

LIGI KUU TANZANIA BARA 2012/2013
Michuano ya Ligi Kuu kuwania ubingwa wa Tanzania Bara kwa msimu wa 2012/2013 itaanza Septemba 15 mwaka huu kwa timu zote 14 kujitupa kwenye viwanja tofauti.
Mechi za ufunguzi zitakuwa kati ya Simba vs African Lyon (Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam), Polisi Morogoro vs Mtibwa Sugar (Jamhuri, Morogoro), Tanzania Prisons vs Yanga (Sokoine, Mbeya), Mgambo JKT vs Coastal Union (Mkwakwani, Tanga), JKT Ruvu vs Ruvu Shooting (Azam Complex, Dar es Salaam), Kagera Sugar vs Azam (Kaitaba, Bukoba) na Toto Africans vs Oljoro JKT (Kirumba, Mwanza).
Mzunguko wa kwanza (first round) utamalizika Novemba 11 mwaka huu ambapo kwenye mzunguko huo mechi ya watani wa jadi Yanga na Simba itachezwa Oktoba 3 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Ligi hiyo itamalizika Mei 18 mwakani kwa mechi kati ya Toto Africans vs Ruvu Shooting (Kirumba), Mgambo JKT vs African Lyon (Mkwakwani), JKT Ruvu vs Mtibwa Sugar (Azam Complex), Tanzania Prisons vs Kagera Sugar (Sokoine), Simba vs Yanga (Uwanja wa Taifa), Oljoro JKT vs Azam (Sheikh Amri Abeid Kaluta) na Polisi Morogoro vs Coastal Union (Jamhuri).
Endapo Simba na Azam hazitafanikiwa kuvuka hatua mojawapo ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika na Kombe la Shirikisho, ratiba hiyo itafanyiwa marekebisho.

WACHEZAJI 17 WAPINGWA KWENYE USAJILI
Klabu mbalimbali zimewasilisha pingamizi Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kupinga usajili wa wachezaji 17 walioombewa usajili katika timu za Ligi Kuu.
Toto Africans ya Mwanza imewawekea pingamizi wachezaji Enyinna Darlinton aliyeombewa usajili Kagera Sugar, na Mohamed Soud anayekwenda Coastal Union kwa maelezo kuwa bado ina mikataba na wachezaji hao.
 Pia Flamingo ya Arusha inapinga usajili wa wachezaji wake Kelvin Friday Iddy katika timu za Azam na Salim Walii (Polisi Mara) kwa vile taratibu za kuwahamisha bado hazijafanywa. Nayo Kagera Sugar inapinga usajili wa beki David Charles Luhende kwenda Yanga kwa vile ada ya uhamisho haijalipwa.
Super Falcon ya Chanjamjawiri, Chakechake, Pemba inapinga wachezaji wake wanne; Edward Christopher Shija, Samir Said Luhava (Simba), Robert Joseph Mkhotya (African Lyon) na Sultan Juma Shija (Coastal Union) kusajiliwa katika timu hizo kwa maelezo taratibu halali za uhamisho hazikufuatwa.
Mchezaji Othman Hassan aliyeombewa usajili Coastal Union anapingwa na Oljoro JKT kwa vile bado ana mkataba na timu hiyo unaomalizika Mei 24, 2013. Nayo Rollingstone Multipurpose Ateclass Foundation ya Arusha inapinga usajili wa Kigi Makassy kutoka Yanga kwenda Simba hadi itakapolipwa fidia ya kumlea mchezaji huyo kwa vile bado hajafikisha umri wa miaka 23.
 Azam inapinga usajili wa Ramadhan Chombo ‘Redondo’ kwenda Simba kwa maelezo bado ina mkataba naye unaomalizika Juni 11 mwakani. Nayo Simba inapinga Kelvin Yondani kusajiliwa Yanga kwa maelezo kuwa ina mkataba naye uliosainiwa Desemba 23 mwaka jana.
 Vilevile Simba imewasilisha malalamiko ya mchezo usio wa kiungwana katika usajili wa Mbuyu Twite aliyeko Yanga kwa maelezo alisaini mkataba na klabu yao Agosti Mosi mwaka huu mbele yao, viongozi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Rwanda (FERWAFA) na APR ambapo alilipwa dola 30,000 na nyingine 2,000 ikiwa ni fedha ya kujikimu na nauli yake ya kujiunga na klabu hiyo.
 Nayo Yanga inapinga Simba kuwaacha wachezaji Dan Mrwanda, Haruna Shamte, Kanu Mbiyavanga na Lino Masombo kwa maelezo walishapatiwa leseni za kucheza Ligi ya Tanzania walizozitumia kwenye mashindano ya Kombe la Kagame. Pia inapinga Ramadhan Chombo ‘Redondo’ kujiunga Simba kwa vile ana leseni ya kuchezea Azam kwa msimu wa 2012/2013.
Pingamizi lingine la Yanga kwa Simba ni kuwa imezidisha idadi ya wachezaji wa kigeni wanaotakiwa kusajiliwa kwa maelezo inao wanane wakati wanaoruhusiwa ni watano. Imewataja wachezaji hao kuwa ni Lino Masombo, Felix Sunzu, Emmanuel Okwi, Mussa Mude, Kanu Mbiyavanga, Pascal Ochieng, Komalmbil Keita na Daniel Akuffor.
Kamati ya Sheria, Maadili na Hadhi za Wachezaji ya TFF chini ya Mwenyekiti wake Alex Mgongolwa inatarajia kukutana Jumapili (Septemba 2 mwaka huu) kupitia pingamizi hizo pamoja na usajili wa wachezaji kwa ujumla kwa 2012/2013.


Thursday, August 30, 2012

ANGALIA MAKUNDI YA UEFA HAPA

Angalia makundi ya UEFA (klabu bingwa barani ulaya) hapa.




 
GROUP A
GROUP B
GROUP C
GROUP D
Porto  Arsenal  AC Milan Real Madrid
Dynamo Kiev  Schalke  Zenit St Petersburg  Manchester City
Paris Saint-Germain  Olympiakos Anderlecht Ajax
Dinamo Zagreb  Montpellier  Malaga Borussia Dortmund
GROUP E
GROUP F
GROUP G
GROUP H
Chelsea Bayern Munich Barcelona Manchester United
Shakhtar Donetsk Valencia Benfica Braga
Juventus Lille Spartak Moscow Galatasaray
Nordsjaelland BATE Borisov Celtic  Cluj


KIBONZO CHA LEO C.RONALDO HAKAMATIKI

Kibonzo kikionesha barcelona wakipata shida na C.Ronaldo



MBUYU TWITE ATUA DAR

Mbuyu Twite akiongozwa na viongozi wa Yanga kuelekea kwenye gari
Hawa ni washabiki wa Yanga waliofika kumpokea Mbuyu Twite


Mbuyu Twite akiwa amevaa Jezi namba 4 Iliyoandikwa Rage akihojiwa na waandishi wa habari

Mmoja wa washabiki wa Yanga akiwa na jezi namba 4 iliyo andikwa Rage
Wakati huo huo kocha wa Yanga Tom amefanya kikao na waandishi wa habari na kukanusha habari iliyo andikwa katika website ya super sports kuwa hafurahii mazingira ya kazi nani ya ya klabu hiyo ya Yanga.
Amesema anavutiwa na mazingira yake ya kazi na ushirikiano anaopata kwa viongozi wa mabingwa hao wa klabu bingwa Afrika mashariki na kati.

KIZUNGU CHA OYSTER-BAY.




HAWA NGURUME AFARIKI DUNIA

Marehemu Hawa Ngurume akitoa maelezo ya ugonjwa wake kwa mwandishi wa habari

Aliyewahi kuwa Mkuu wa Wilaya ya Mbalali, Bagamoyo na Kinondoni na Mkoani Iringa Hawa Ngurume. Amefariki leo Asubuhi. Mama huyo alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa figo.
Ugonjwa huo ulimsumbua kwa muda ambapo ilifanya atibiwe katika Hospitali mbalimbali ikiwemo Hospitali ya Taifa Muhimbili na Hospitali nyingi za binafsi.
Marehemu atakumbukwa kwa uchapa kazi na uongozi wake mzuri na usikivu na uunganishaji wa wananchi na uhamasishaji wa maendeleo.
Sote ni wa Mungu na kwake tutarejea.

MAGAZETI YA LEO AGOSTI 30















TUSIPO LIKEMEA HILI TUTARAJIE AJALI MBAYA UBUNGO




MH KIKWETE NDANI YA BBC SWAHILI TV




ANGALIA MAGOLI YA MADRID WALIPO ICHAPA BARCELONA NA KUCHUKUA KOMBE


Real Madrid 2-1 Barcelona - Highlights by simaotvgolo12

MESSI NA C.RONALDO HAWAKUPEANA MIKONO BAADA YA MECHI




Wednesday, August 29, 2012

MBUYU TWITE KUWASILI KESHO

Mchezaji alieleta mtafaruku mkubwa katika usajili wake atawasili kesho majira ya saa tisa alasiri. Msemaji wa Young Africans Sports Club Luis Sendeu ameomba washabiki na wapenzi waote wa yanga kujitokeza kumpokea mchezaji huyo. Sendeu pia amehabarisha kuwa suala la Mbuyu kukamatwa wao wanaona ni kama porojo tu.Wakati huo huo timu ya Young Africans Sports Club inatarajiwa kujitupa uwanjani katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam kupambana na Coast Union ya Tanga.
Mbuyu Twite akiitumikia Yanga huko Rwanda

Mbuyu Twite akisaini Yanga mbele ya Bin Kleb



AKUFFOR NA NGASSA WAING`ARISHA SIMBA ARUSHA

Daniel Akuffor akikabidhiwa jezi ya simba wakati wa usajili
Simba wameibuka kidedea baada ya kutoka kifua mbele kwa mabao mawili kwa moja. Mabao ya Simba yalifugwa na mshambuliaji wa kimataifa kutoka Ghana Daniel Akuffor na mshambuliaji aliehamia hapo ktoka Azam FC Mrisho Khalfan Ngassa. Goli la Ngassa lilifungwa kwa tictak.

BABA LEVO,LINEX NA SUMA LEE WAPATA AJALI KIGOMA

Wasanii wa bongo fleva Baba levo Linex na Suma lee wamepata ajali wakati wakielekea katika show yao kigoma. Ajali hiyo ilitokana na basi lililokuwa limepaki katikati ya barabara kwenye kona. Gari la wasanii hao lilikuwa linaendeshwa na Suma lee ambae ndio mmiliki wa gari hilo. mtu mmoja tu ambae ni dancer wa suma lee yeye ndio alie umia mguu tu. Suma lee alijaribu kulikwepa gari hilo ndipo akashindwa kulimudu gari vizuri kitu kilichosababisha kutoka nje ya barabara na kugonga mti. Linex anasema kitu kilichosababisha kusiwe na majeruhi ni mwendo ambao dereva alikuwa akiendesha ulikuwa sio mkali sana. Wasanii hao watakuwa na show kigoma Jumamosi na Jumapili baada ya hapo wataenda Bujumbura kwa shows mbalimbali.
Kitongoni tunawapa pole na safari njema
Linex

Baba Levo



Tuesday, August 28, 2012

CHADEMA YASEMA POLISI HAIWEZI KUKWEPA LAWAMA YA MAUAJI

Chadema imesema kuwa polisi haiwezi kukwepa lawama juu ya kifo cha kijana Ally Zona mwenye umri wa miaka 38 kilichotokea huko Morogoro. Vilevile CHADEMA kimesitisha maandamano katika Mkoa wa Iringa kupisha zoezi la sensa. akizungumza na waaandishi wa habari katibu mkuu wa cha hicho Dr. Slaa amesema baada ya zoezi hilo kuisha wataendelea na maandamano na kampeni yao maarufu kwa jina la Movement for Change (M4C). Wakati huhuo chama cha chadema kimesema kitagharamia mazishi ya kijana huyo aliefariki huku ikisubiri ripoti kutoka kwa Daktari na mwanasheria wao ili kujua hatua gani ya kuchukua

Katibu mkuu wa CHADEMA Dr. Slaa akiongea na waandishi kwenye hoteli ya Mount Uluguru




VURUGU KATI YA POLISI NA CHADEMA IRINGA

Kumetokea vurugu leo wakati wa jioni katika mji wa Iringa mjini kati ya Polisi na wafuasi wa  Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Vurugu hizi zilitokea mitaa ya Miyomboni
Wananchi wakishuhudia kwa mbali vurugu kati ya wanaodaiwa wafuasi wa CHADEMA na Polisi eneo la Iringa Miyomboni


MSIKITI WA IJUMAA KITONGONI

Masjid Jumaa Kitongoni (Sunni walJamaa Istiqama)



MAGAZETI YA LEO AUGUST 28, 2O12



































 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU