Facebook Comments Box

Sunday, November 4, 2012

YANGA NA AZAM KATIKA PICHA

Kiiza akijaribu bila mafanikio kufunga

Aggrey Morris akiruka juu ya Paul Ngalema kupiga mpira kichwa

Mbuyu Twite akimuacha chini Salum Abubakar

Kiiza akimtoka Hajjji Nuhu

Haruna Niyonzima 

Chuji akijadiliana na Niyonzima kabla ya kupigwa kwa mpira wa adhabu

Kiiza alivyomuenzi Mafisango

Mwadini akidaka mpira hewani 

Simon Msuva anateleza

Mwadini akiruka kupangua mpira

Msuva

Hatari kwenye lango la Yanga

Jabir Aziz akimdhibiti Chuji

Kiiza anapasua katikati ya Ibrahim Shikanda kulia na Sure Boy kushoto 

Nadir Haroub 'Cannavaro' akimdhibiti John Bocco

Hatari kwenye lango la Yanga

Stewart Hall alitia huruma

Frank Domayo kulia akipambana na Aggrey Morris

Niyonzima akipiga shuti mbele ya Shikanda

Twite anapasua

Sure Boy akimtoka Twite

Sure Boy na Twite

Chuji akipiga kisu mbele ya Sure Boy

Msuva anatafuta njia

Shughuli

Yanga wakipiga ndiki kabla ya mechi

Kikosi cha Azam leo

Kiiza anamtoka Erasto Nyoni

Kikosi cha Yanga leo

Hatari kwenye lango la Azam

Hatari kwenye lango la Yanga

Msuva akiwasalimia wenzake benchi baada ya kupumzishwa

Niyonzima kushoto, Nyoni kulia

Kiiza na Hajji Nuhu


Kiiza baada ya kufunga bao la pili


Kavumbangu wa pili kutoka kushoto, akishangilia bao lake na wenzake

Kavumbangu wa kwanza kushoto


LIVE SCORE : FT YANGA 2 - 0 AZAM, MTIBWA 2 - 0 SIMBA


Kutoka Taifa: Mpira umeisha Yanga wanatoka kifua mbele kwa Goli kwa sifuri

Kutoka Morogoro:  Mpira umeisha Mtibwa Inatoka kifua mbele kwa 2 kwa sifuri

Kutoka Morogoro: Gooooool Mtibwa wanapata goli la pili hapa. Nilisema huyu Javu ana historia ya kufunga katika uwanja huu. Ndio maana mara zote tunaandika mtibwa wanaongoza kwa goli la kwanza na hili ni la pili

Kutoka Mtibwa: Dk 88 Mtibwa bado wapo mbele kwa goli la kwanza

Kutoka Morogoro: Mwinyi kazimoto anaachia shuti kali linapanguliwa na kipa na kuwa kona. Simba wanalisakama lango la mtibwa

Kutoka Morogoro: Husein Javu anaingia kuchukua nafasi ya Muhamed Mkopi. Huyu Javu ana historia nzuri ya kufunga katika uwanja huu

Kutoka Morogoro: Dk 79 Okwi anawakosakosa mtibwa na inakuwa kona. Husein Sharrif anapewa kadi ya njano kwa kupoteza muda. askari wameongezwa uwanjani

 Kutoka Taifa: Gooooooool Yanga wanaongeza goli la pili. Ni Hamis Kiiza "diego" anafunga goli safi sana hapa. Alivua jezi hapa kiiza anapewa kadi ya njano

Kutoka Taifa: Abdi Kassim anachukua nafasi ya Hamis Mcha.

Kutoka Taifa: Msuva anaenda nje anaingia Luhende.Yanga wanakosa goli baada ya Kavumbagu kuchelewa krosi ya Niyonzima

Kutoka Taifa: Dk 51 Erasto Nyoni anaonyeshwa kadi ya njano baada ya kumkanyaga Niyonzima wa Yanga.

Kutoka Taifa: Dk 48 Bocco anashindwa kuuwahi mpira aliopigiwa na Khamis Mcha lakini Chuji anautoa na kuwa kona. Azam inapata kona ambayo inakolewa na mabeki wa Yanga.

Kutoka Taifa: Kipindi cha pili kinaanza hapa uwanja wa taifa kati ya Yanga na Azam

Kutoka Morogoro: Babu Ally anapewa kadi ya njano kwa kumfanyia madhambi emanuel Okwi. Na Mrisho Ngassa anaingia kuchukua nafasi ya Akuffor. Chollo anaingia nafasi ya Ochieng

Kutoka Morogoro: Mpira umeanza Jamal anatoka na anaingia Issa


Kutoka Morogoro: Washabiki wa Simba wamtupia chupa mwamuzi wa pambano hili, vile vile wamewarushia vilevile chupa wachezaji wao. mmoja wa washabiki hao wa simba amekamatwa na polisi. Ulinzi zaidi unahitajika katika mechi hii maana inaonekana washabiki wa simba hawana uvumilivu.

Taifa; Dk 45 HALF TIME..... AZAM 0-1 YANGA

 Kutoka Morogoro: Mtibwa wanapata kona tatu mfululizo, lakini, Kaseja anadaka, dakika ya 42 sasa

 Taifa: Dk 39 Yanga na Azam zinashambuliana kwa zamu na mpira unachezwa katikati sana.

Kutoka Morogoro: Mtibwa inaongoza kwa bao moja dhidi ya Simba, mfungaji Mohamed Mkopi. MTBWA 1-0 SIMBA


Taifa:  Dk 32 Azam inapata kona baada ya Mbuyu Twite kuutoa mpira nje
Khamis Mcha anapiga kona lakini Bocco anautoa mpira nje.
Dakika ya 28, Akuffor, anashindwa kutumia makosa ya mlinzi wa Mtibwa ambaye alipiga pasi fupi kwa mwenzake na kuiwahi. Lakini, akiwa ndani ya sita anashindwa kuamua kufunga au kutoa pasi, na kupiga pasi mkaa iliyonaswa na mlinzi wa Mtibwa. Dakika ya 30 sasa.
Kutoka Taifa: Dk 28 Bocco anapiga shuti kali langoni kwa Yanga lakini kipa Ally Mustapha anadaka
 Dk 26 Athuman Idd Chuji anamchezea faulo Michael Bolou.
Kutoka Morogoro: Kwa dakika 20 za mwanzo, mechi bado imebalansi hakuna mashambulizi ya maana sana ambayo timu zinayaandaa. Kila timu inacheza kama haitafuti ushindi. Mara mbili, mshambuliaji, Said Mkopi wa Mtibwa amejaribu kumtoka Amir Maftah, lakini hakufanya cha maana. Emmanuel Okwi anajitahidi kuwakimbiza mabeki wa Mtibwa Sugar, lakini bado hapati, sapoti ya karibu kutoka Sunzu na Akuffor. Mtibwa, wamepiga kona nne hadi sasa, wakati,Simba, wamepata kona moja tu. Kiujumla, mchezo bado umepooza hadi sasa.
 
 Kutoka taifa: Dk 18 Niyonzima wa Yanga,anakosa bao la wazi kwa kupiga nje mpira aliopokea kutoka kwa Oscar Joshua.
Dk 15 Erasto Nyoni wa Azam anamchezea rafu Msuva 
Dk 14 Simon Msuva wa Yanga anakosa bao la wazi baada ya kushindwa kuuwahi mpira uliopigwa na Haruna Niyonzima.
Dk 13 Mpira unachezwa kwa kasi sana na timu zote zinatawala kiungo
 
 Kutoka Morogoro - Kwa dakika hizi kumi za mwanzo, timu zote zinaonekana kucheza kwa kuogopana zaidi. Mtibwa, walianza kufika katika lango la Simba, kupitia kwa Shaaban Nditti. Walinzi wa Simba, Keita na Ochieng, wakamthibiti. Bado hakuna soka la kuvutia na la mipango, japo, Mtibwa, wanaonekana kucheza kitimu hadi sasa. Simba, wanapata kona ya kwanza, lakini haina madhara, dakika ya 12 
Dk 9 GOOO...... Didier Kavumbagu anaifungia Yanga bao la kwanza baada ya kutokea piga nikupige katika lango la Azam. AZAM 0-1 YANGA
Kutoka taifa: DK 3 Hamis Kiiza anakosa bao la wazi kwa upande wa Yanga.
 Kutoka taifa: Mpira ndio umeanza hapa Uwanja wa Taifa kati ya
Azam Fc Vs Young Africans
Morogoro - Mpira umeanza hapa Morogoro - Simba wakianza kwa kasi.
Leo tunaendeza utamaduni wetu wa kuwaletea matukio muhimu yanayoendelea kwenye viwanja tofauti vya ligi kuu ya Tanzania bara - kwa siku ya leo tunawaletea matukio ya mechi mbili kubwa kati ya Azam na Yanga, na Simba dhidi ya Mtibwa.
Kutoka Morogoro - Hiki ndio kikosi cha kwanza cha Simba kinachoanza: Kaseja, Kapombe, Maftah, Keita, Ochieng, Mkude, Kiemba, Kazimoto, Sunzu, Okwi, Akuffor
Hiki ndio kikosi cha Yanga ambacho tumefanikiwa kukipata. 
1.Ally Mustapha 'Barthez'
2.Mbuyu Twite
3.Oscar Joshua
4.Nadir Haroub 'Cannavaro'
5.Kelvin Yondani
6.Athuman Idd 'Chuji'
7.Saimon Msuva
8.Frank Domayo
9.Didier Kavumbagu
10.Hamis Kiiza
11.Haruna Niyonzima

Subs:
1.Yaw Berko
2.Juma Abdul
3.David Luhende
4.Nurdin Bakari
5.Nizar Khalfani
6.Jeryson Tegete
7.Said Bahanunzi


MAALIM SEIF AZUNGUMZA

Katibu Mkuu wa Chama Cha Wananchi CUF Maalim Seif Sharif Hamad ameelezea kuchukizwa kwake na vitendo vya vurugu na uvunjifu wa amani vilivyotokea hivi karibuni visiwani Zanzibar.

Amesema vitendo hivyo vimeigharimu Zanzibar katika Nyanja mbali mbali zikiwemo za kiuchumi, kisiasa na kijamii, sambamba na kuitia doa katika jamii ya kimataifa.

Akihutubia mkutano wa hadhara wa chama hicho katika viwanja vya demokrasia Kibandamaiti mjini Zanzibar, Maalim Seif ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar amevilaumu vyombo vya dola kwa kutochukuwa hatua zinazostahiki katika kudhibiti vitendo hivyo.

Amesema hatua zilizochukuliwa katika kurejesha amani baada ya kutokea kwa vurugu hizo hazikuwa muafaka, kwani zimekuwa zikiwadhalilisha na kuwanyanyasa wananchi wasiokuwa na hatia pamoja na kuhujumu mali zao.

Amesema yeye binafsi amechukizwa na kitendo cha kuuliwa kwa askari polisi katika eneo la Bububu, Koplo Said Abrahmani lakini bado serikali na vyombo vya dola vina jukumu la kulinda haki za raia kwa kuwasaka wanaohusika na tukio hilo, na sio kuwanyanyasa raia wasiokuwa na hatia.

“Nazungumza haya kwa unyonge sana leo, sikufikiria kuwa vitendo hivi vingetokea Zanzibar katika wakati huu tunaotekeleza maridhiano ndani ya serikali ya umoja wa kitaifa”, alieleza Maalim Seif na kuongeza: “Sipendi kuisema serikali yangu na Rais wangu hadharani, lakini inanibidi niseme ‘Rais wangu Dkt Shein unatuangusha’ kwa kuwa wewe ndiye mwenye jukumu kubwa zaidi la kulinda amani ya nchi hii” alieleza.

Ametahadharisha kuwa huenda vitendo hivyo vimepangwa kuvuruga umoja wa Wazanzibari ambao umeiletea sifa kubwa Zanzibar, na kuwataka wananchi kutokubali kuingizwa katika mtego utakaopelekea kuvunjika kwa umoja na mshikamano uliopo miongoni mwa wananchi.

Katibu Mkuu huyo wa CUF alienda mbali zaidi kwa kudai kuwa vikundi vinavyolalamikiwa kufanya vurugu vikiwemo vya ‘Ubaya ubaya, Mbwa mwitu na Janjawid vilikuwepo kabla ya tukio hilo na kwamba vimetokana na kundi kubwa la vijana la JANJAWID lililoahidiwa kupewa ajira na Serikali.

Katika hatua nyengine Maalim Seif ameitaka Tume ya mabadiliko ya katiba kufanya kazi kwa uadilifu na kuheshimu mawazo ya wananchi wanayoyatoa bila ya kuonyesha upendeleo kwa baadhi ya watu au makundi fulani.

“Tume hii inaonekana kuanza kuwa na ‘bias’ kwa baadhi ya watu na makundi fulani, lakini tunamwambia Jaji Warioba tume yake iheshimu mawazo ya wananchi”, alitanabahisha.

Katika risala ya wanachama wa chama hicho kwa wilaya sita za Unguja iliyosomwa na Katibu Mtendaji wa vijana CUF taifa Khalifa Abdallah walitahadharisha juu ya uwezekano wa kuwepo kwa ajenda ya siri ya kuvuruga Serikali ya Umoja wa Kitaifa.

Amesisitiza kuwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa bado inahitajika katika kupata ukombozi wa kweli wa Zanzibar, sambamba na kuendeleza umoja na mshikamano wa Wazanzibari.

Naye Kaimu wa Kaimu Naibu Katibu Mkuu wa CUF Bw. Salim Bimani amewasisitiza wananchi kuendelea kujitokeza kwa wingi kutoa maoni yao juu ya mabadiliko ya katiba, na kuiomba Tume inayohusika na ukusanyaji wa maoni kuwapa fursa wananchi kutoa maoni yao kwa uwazi.

“Wananchi msikubali kuchokozeka, nendeni mkatoe maoni kwani hii ni fursa pekee ya kupata katiba tuitakayo” alisisitiza Bimani.




SHABAN KADO APATA AJALI

 Mchezaji wa simba Uhuru Selemani aandika katika wall yake ya Facebook kuwa mchezaji wa Mtibwa Sugar Golikipa Shaaban Kado amepata ajali Chalinze. Hii labda ndio inayofanya leo asiwepo uwanjani. Blog hii inafuatilia na habari kamili itakupa baada ya muda.
Ndugu zangu mliopo chalinze naomba mfatilie hapo hospitali kado kapata ajari nasim yake haipatikan pls naomba mfatilie atakae kuwa nataarifa aniinbox namba yake sory jaman


LORD EYES APATA DHAMANA

.
Stori za uhakika nilizozipata muda mfupi uliopita ni kwamba mkali wa Hiphop kutoka A Town ambae alikua anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za wizi wa vifaa vya gari la Ommy Dimpoz, Isack Waziri (Lord Eyes) hivi sasa yuko nje kwa dhamana.
Ametoka nje kwa dhamana toka ijumaa ya novemba 2 2012.
Oktoba 23 2012 Kamanda wa polisi mkoa wa kipolisi Kinondoni Charles Kenyela alikaririwa na millardayo.com akisema “Watuhumiwa hawa wawili Kurushinde na Lord Eyes tunawashikilia kwa tuhuma zipatazo 30, yani matukio mbalimbali 30 pengine yanaweza yakaongezeka ambayo yameripotiwa kutokea katika maeneo mbalimbali kama vile Mlimani City, Kijitonyama, ufukwe wa bahari kama Coco beach, kwenye kumbi mbalimbali za starehe na pia  kwenye maeneo ambayo kunakua na harusi, sehemu ambazo kunakua na magari mengi watu hawa ndio huwa wanaitumia hiyo nafasi kufanya uhalifu, tunawashikilia kwa makosa ya wizi”
.


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU