Facebook Comments Box

Monday, February 25, 2013

HUYU NDIO MTOTO WA MIAKA NANE ALIE MUOA MWANAMKE WA MIAKA 61

Zaidi ya watu mia moja walikusanyika katika nchi ya Zimbabwe kushuhudia mtoto wa miaka nane (8) akimuoa mwanamke mwenye umri wa miaka (61) ambae anaweza akafaa kabisa kuwa bibi yake. Cha kushangaza zaidi familia zote mbili za wanandoa hao pamoja na watoto watano wa mwanamke huyo walikuwepo.
Shangazi wa mtoto huyo mwenye miaka (46) alitoa sababu za kutokea ndoa hiyo alisema "Huyu kijana alipewa jina la bibi yake ambae hakuwahi kufunga ndoa, mizimu imemuamuru afunge ndoa na Hellen (Mmama huyo) ndio imekuwa chaguo lake.
Wanafamilia walichukulia matamanio ya huyo kijana kufunga ndoa kwa umakini sana na kuamua kumruhusu kufunga ndoa na kulipia kila kitu. Na bibi huyo alieolewa na kijana huyo pamoja na kuwa na mume alikubali kuolewa kwa kuwa alijua ndio mizimu ya mababu waliokufa inavyo waamuru na kutaka.
Mtoto huyo alimuambia mama yake "Nataka kuoa kwa kuwa nataka kufanya hivyo na nimemchagua mwanamke huyu kwa kuwa nampenda na baada ya ndoa hii nitasoma kwa bidii sana na nikiwa mkubwa nitamuoa mwanamke ninalingana nae"
Mume wa mwanamke huyo alisema yeye hana shida wala wivu na kijana huyo kwa kuwa ni mdogo na ni mizimu iliyoyataka hayo. "watoto wangu na mimi hatuna shida na hili na tumefurahi sana"
Baadhi ya wanafamilia walioneshwa kushitushwa na ndoa hiyo na wanafamilia wenzao kuchukulia swala la mizimu kwa umakini wa kiasi hicho.
Wanandoa hao walimaliza harusi yao kwa mabusu moto moto.




Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU