Facebook Comments Box

Wednesday, May 29, 2013

M TO THE P BADO MZIMA NA DAKTARI ATHIBITISHA

habari zenye uhakika kutoka kwa Dr aliekuwa ICU, katika hospitali ya St Hellen Joseph, zimethibitisha kuwa msanii aliekuwa na Ngwea wakati mauti yanamkuta, ambae yeye pia alikua hoi hospitali, anaendelea vizurin, na anaongea kwa sasa, ila uchunguzi wa kile kilichosababisha kufikishwa hospitali hapo bado unaoendelea
hapa Dr anaongea kuhusu maendeleo ya M2theP
 
 


UPDATES ZA KUHUSU MSIBA WA MANGWAIR IKIWEMO YA KUKATAZA NYIMBO ZAKE KUPIGWA CLOUDS FM

Picture
Pigo tena kwa muziki wa Bongo Fleva baada ya ripoti kusema, M To The P aliyekuwa na Mangwea jijini Johannesburg yupo hoi hospitali.


Mangwea na M To The P walisafiri pamoja hadi Afrika Kusini kwa ajili ya kufanya onesho (show) na baadaye waliendelea na maisha, lakini jana  Mangwea alikutwa amefariki dunia chumbani na M To The P akiwa taabani na kulimbizwa hospitalini.


Picture
Picture
MIPANGO YA MAZISHI

Baba Mdogo wa Marehemu Mzee Mangwea ambaye yuko Mbinga, Songea kikazi, amesema kuwa wamekubaliana na kaka yake mkubwa (Baba mkubwa wa Ngwair), David Mangwea (ambaye naye yuko Songea) pamoja na kaka yao mwingine aliyepo Mara kuwa watu watakutanika Mbezi kwa msiba na mapokezi kutafanyika Mbezi Beach, Dar es Salaam.

Maziko ya mwili wa Ngwair yamepangwa kufanyika Morogoro sehemu ambayo baba yake pia alizikwa.

Kwa wakati huu, ndugu, jamaa na marafiki wa karibu wanawasiliana na Ubalozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini kuhusu namna ya kuleta miili ya marehemu hao nyumbani.

Taarifa zaidi zitatolewa kufuatana na maamuzi ya viikao vya familia.

Source: wavuti


KESI YA UCHOCHEZI YA LEMA (MB) YA AHIRISHWA

Picture
Mbunge wa Arusha Mjini na Mjumbe wa Kamati Kuu (CHADEMA) akitoka Mahakamani na mawakili wake Humphrey Mtui na Method Kimomogoro asubuhi hii mara baada ya kesi inayomkabili kuahirishwa
Hakimu Devota Msofe wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha ameahirisha hadi Julai 7, 2013, shauri la kesi inayomkabili Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini, Godbless Lema (CHADEMA), kwa tuhuma za uchochezi kwa wanafunzi wa Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) anaotuhumiwa kuufanya Aprili 24 mwaka huu, ili kesi hiyo ianze kusikilizwa upelelezi utakapokuwa umekamilika.


RAIS WA ZANZIBAR DK. SHEIN AENDELEA NA ZIARA YAKE CHINA

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza  la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akisalimiana na Rais wa China Xi jinping alipofika Ikulu ya Mjini Beijing Nchini China akiwa katika ziara ya mualiko wa Serikali wa Jamhuri hiyo
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza  la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akiwatambulisha Viongozi katika ujumbe aliofuatana nao kwa Rais wa Jamhuri ya watu wa China Xi jinping, walipofika Ikulu ya Mjini Beijing Nchini China akiwa katika ziara ya mualiko wa Serikali wa Jamhuri hiyo.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza  la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akiwatambulisha Viongozi katika ujumbe aliofuatana nao kwa Rais wa Jamhuri ya watu wa China Xi jinping, walipofika Ikulu ya Mjini Beijing Nchini China akiwa katika ziara ya mualiko wa Serikali wa Jamhuri hiyo.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza  la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,(wa nne kushoto)akiwa na ujumbe wake katika mazungumzo na Rais wa China Xi Jinping,(wane kulia) katika Ikulu ya Mjini Beijing Nchini China.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza  la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akisalimiana na Makamo wa Rais wa China Li Yuanchao,katika makaazi yake Mjini Beijing nchini China akiwa katika ziara ya mualiko wa Kiserikali wa Nchi hiyo,
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza  la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akiwa katika  mazungumzo na  Makamo wa Rais wa China Li Yuanchao,katika makaazi yake Mjini Beijing nchini China akiwa katika ziara ya mualiko wa Kiserikali wa Nchi hiyo,
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza  la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,(wa pili kulia)akiwa katika  mazungumzo na Makamo wa Rais wa China Li Yuanchao,(kulia)katika makaazi yake Mjini Beijing nchini China akiwa katika ziara ya mualiko wa Kiserikali wa Nchi hiyo,pamoja na ujumbe aliofuatana nao.
 Mke wa Rais wa Zanzibar mama Mwanamwema Shein akisalimiana na mke wa makamo wa Rais wa China Mama Li Yuanchao katika makaazi yake Mjini Beijing nchini China akiwa katika ziara ya mualiko wa Kiserikali wa Nchi hiyo,pamoja na ujumbe aliofuatana nao.
  Mke wa Rais wa Zanzibar mama Mwanamwema Shein akisalimiana na  makamo wa Rais wa China Mama Li Yuanchao katika makaazi yake Mjini Beijing nchini China akiwa katika ziara ya mualiko wa Kiserikali wa Nchi hiyo,pamoja na ujumbe aliofuatana nao.




JIDE AAHIRISHA SHOO YAKE YA MIAKA 13 KUTOKANA NA KIFO CHA MSANII MWENZAKE ALBERT MANGWEA 'NGWEA'

Mwana Dada Komando katika mziki wa Bongo na mkongwe wa siku nyingi JUDITH WAMBURA 'Lady Jay Dee' Bint Machozi, Mamaa Somefood hayo yote ni majina yake si unajua tena sanaa, amesitisha onesho lake la kutimiza miaka 13 tangu aanze kufanya burudani lililokuwa lifanyike siku ya Ijumaa hii ya tar 31/05/2013 ndani ya Mjengo wake wa Nyumbani Lounge kutokana na Kifo cha Msanii mwenzake katika Bongo Fleva ambaye amepatwa na Msiba nje ya nchi huko Bondeni kwa MADIBA alikokwenda kutoa Show.
 
Jide amesema hayo alipokuwa akihojiwa katika kipindi cha Super Mix kinachorushwa na Kituo cha Televisheni cha East Africa Radio kwa masikitiko makubwa sana, na amesema show hiyo haitafanyika kama ilivyokuwa imepangwa na badala yake mpaka tarehe nyingine itakapo pangwa tena.


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU