Facebook Comments Box

Wednesday, February 13, 2013

TANESCO AND SYMBION POWER SIGNS MoU FOR A JOINT VENTURE IN 400MW MTWARA PLANT



TANESCO and Symbion Power today signed a Memorandum of Understanding for building and operating a 400MW power plant in Mtwara through a Public Private Partnership. The work will include the construction of a 650 km transmission backbone from Mtwara to Songea where it will be connected to the TANESCO national grid through a line that will be built from Makambako to Songea.

 This development will be phased and it will take three years from financial closure to completion. The first phase will involve increasing the existing capacity in Mtwara to meet the growing demand in the southern regions including Lindi and Mtwara. Engineering study work will commence in March.

TANESCO and Symbion have been in discussions since Symbion presented a proposal to TANESCO and the Ministry of Energy in September 2012. This has now led to the signing of the board-approved MOU that allows the two companies to form a Public Private Partnership and develop the project. It will take around 12 months to put the necessary financing in place before the three-year clock begins to tick.

Speaking at the signing of the MOU in Dar es Salaam, Paul Hinks, the Chief Executive Officer of Symbion Power said, “The south of this country has been starved of energy for decades and this has severely stunted its development. This project will succeed because it includes transmission lines that will feed the grid system. The transmission lines will be owned exclusively by TANESCO but they will be built as a part of the project.”

 “Symbion and TANESCO will be working with a number of international funding agencies, banks and private equity firms in 2013 to put the financial package together, many of whom have already expressed great interest in the project. We are hopeful that U.S. government agencies such as the U.S. Exim Bank and the U.S. Overseas Private Investment Corporation will show keen interest in the investment too.”

 “In the three years since Symbion came to Tanzania we have seen rapid development and improved network stability. Tanzania will in the future have an abundance of gas and it can become entirely self sufficient and even a regional exporter to countries that are not blessed with the fuel resources that are available in the country. The days of complete reliance on rain-driven hydro electric systems are gone and alternative sources of power need to be implemented to ensure that there is security of supply.”

 Speaking during the signing event, TANESCO’s Acting Managing Director Eng. Felchesmi Mramba said, “For many years the Southern part of the country has been suffering from poor power reliability due to the region not being connected to the National Grid. However, through this planned partnership, Lindi, Mtwara and Ruvuma will be connected to the National Grid. Connecting the Southern regions to the National grid will significantly improve reliability of the entire network. This is one of the ways TANESCO can benefit from the PPP arrangement whereby the Public and Private sector join forces to undertake projects that would otherwise be difficult to implement.”

BUNGE KUFUTA MATANGAZO YA MOJA KWA MOJA

Picture
Katibu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Thomas Kashilila akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari kuhusu ukiukwaji wa kanuni za bunge uliofanywa na baadhi ya wabunge wakati wa mkutano wa 10 wa bunge uliomalizika mjini Dodoma na mabadiliko yaliyofanyika kwa baadhi ya kamati kuondolewa pamoja na uundwaji wa kamati mpya 3 zitakazoshughulikia Ushirikiano wa Afrika, Mashariki, Bajeti, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa. (Picha na Aron Msigwa)
Katibu wa Bunge Dk Thomas Kashilila akizungumza na Wanahabari jijini Dar es Salaam leo wakati akitoa taarifa ya mapendekezo ya kuanzisha kamati ya bajeti na kuvunjwa kwa baadhi ya kamati za bunge amesema Bunge linatarajia kufuta utaratibu wa kurusha matangazo ya moja kwa moja (LIVE) kupitia televisheni kwa  nia ya kukomesha vitendo vya baadhi ya Wabunge wanaokikuka kwa makusudi Kanuni za Bunge na kuleta vurugu kwa kutafuta umaarufu bila na hivyo kutoa picha mbaya katika jamii.

Akasema ili kurejeza maadili kwa sasa wameomba kufutwa utaratibu wa kurusha matangazo ya bunge ya moja kwa moja badala yake watarekodi ili kuondoa hoja zisizokuwa za msingi.

Akasema jamii imeendelea kutazama mabishano yasiyokuwa na hoja za msingi kutokana na kukiukwa kanuni hizo.

Dk Kashilila amesema kuwa kwa sasa kuna baadhi ya kamati za bunge ambazo zimevunjwa kutokana na baadhi ya kamati hizo kuingilia katika utendaji jambo ambalo limekuwa likipoteza maana ya kamati hizo.

Ameahidi kuwa ofisi yake itaendelea kushirikiana na vyombo vya habari katika utoaji wa taarifa mbalimbali za bunge pamoja na uandaaji wa mafunzo ya mara kwa mara kwa waandishi wanaoandika habari za bunge, huku akiwasisitiza waandishi wa habari kuitumia ipasavyo ofisi yake kupata  taarifa sahihi za kuwasaidia katika uandishi.


BARUA YA JAMAL MALINZI YAGONGA MWAMBA

 
Taarifa kwa Vyombo vya Habari
Tarehe 13 Februari 2013

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linapenda kuwajulisha wapenzi wa mchezo huu kuwa limepokea barua kutoka kwa Ndg. Jamal Malinzi ambayo inaomba kuangaliwa upya kwa maamuzi ya Kamati ya Rufaa za Uchaguzi ya TFF ya kuliondoa jina lake kwenye orodha ya wagombea urais wa Shirikisho.
 

Barua hiyo ya tarehe 13 Februari 2013 ilielekezwa kwa mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya TFF. Baada ya kuipata barua hiyo, Sekretarieti iliwasiliana na Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ambaye alielekeza kuwa Ndg. Malinzi alielekeza barua yake kwenye chombo ambacho hakikufanya uamuzi wa kuliengua jina lake na hivyo hakina mamlaka ya kuangalia upya suala hilo.
 

Mwenyekiti alishauri kuwa TFF imwandikie Ndg. Malinzi barua ya kumshauri kuwa aelekeze maombi yake kwenye chombo kilichofanya maamuzi kwa kuwa ndicho kinachoweza kuangalia upya maamuzi yake.
 

Sekretarieti pia imepokea maamuzi rasmi ya Kamati ya Rufaa za Uchaguzi ya TFF na imeshayawasilisha kwenye Kamati ya Uchaguzi ya TFF kwa ajili ya kuendelea na mchakato wa uchaguzi kwa mujibu wa Katiba na Kanuni za Uchaguzi za TFF.

Angetile Osiah
Katibu Mkuu,
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)


YANGA YAINYANYASA AFRICAN LYON


 

 Mabingwa wa kombe la Kagame timu Young Africans leo imeendeleza wimbi lake la ushindi katika mzunguko wa pili wa ligi kuu ya Vodacom baada ya kuichapa timu ya  African Lyon jumla ya mabao 4-0, katika mchezo uliofanyika jioni hii katika dimba la Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Young Africans ambayo inaongoza ligi kwa kuwa na pointi 36 na mabao 33 ya kufunga, iliingia uwanjani kwa ajili ya kusaka pointi 3 muhimu ambazo imefanikiwa kuzipata.
Kikosi cha mholanzi Ernest Brandts kiliuanza mchezo kwa kasi, na katika dakika 15 za kwanza washambuliaji wake Hamis Kiiza na Jerson Tegete walikosa nafasi za wazi za mabao ya mapema, kufuatia kutokua makini katika umaliziaji.
Jerson Tegete aliwaiunua mashabiki wa Yanga katika dakika ya 21 baada ya kuipatia timu yake bao la kwanza kwa kichwa akimalizia pasi safi iliyopigwa na mlinzi wa pembeni David Luhende ambaye alipanda kuongeza nguvu mashambulizi.
Yanga iliendela kuutawala mchezo na hasa sehemu ya kiungo, ambapo Haruna Niyonzima, Athumani Idd Chuji, Frank Domayo waliweza kuitawala sehemu hiyo ya katikati hali iliyopelekea wachezaji wa African Lyon kuutafuta mpira kwa tochi.
Dakika ya 42, Jerson Tegete tena aliipataia Young Africans bao la pili kwa staili ya peke, baada ya kuupiga kwa kisigino mpira wa krosi uliokuwa umepigwa na Haruna Niyonzima na kumfanya mlinda mlango wa African Lyon Abdul Seif na walinzi wake wasijue cha kufanya.
Saimon Msuva alitengeneza nafasi nyingi za kufunga lakini mipira hiyo ilipowakuta wafungaji hawakua katika nafasi nzuri ya umaliziaji hali iliyopelekea kukosa mabao mengine ya wazi katika kipindi cha kwanza. 
 
 Kocha wa African Lyon, Salum Bausi, akiwa katikati ya uwanja akiwatuliza wachezaji wake kukubali kupigwa penati, waliyokuwa wakiigomea, huku wakimzonga refa.
Mpaka dakika 45 za kipindi cha kwanza Young Africans 2-0 African Lyon.
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi na Yanga kuutawala mchezo hali iliyopelekea kujipatia penati dakika ya 48 ya mchezo, kufuatia walinzi wa African Lyon kuzidiwa na kiungo Haruna Niyonzima hali iliyowapelekea kumcheza madhambi mchezaji huyo ndani ya eneo la hatari, mwamuzi aliamuru ipigwe penati ambayo iilipigwa na Hamis Kiiza ambaye alikosa penati hiyo.
Kocha wa Yanga Ernest Brandts alifanya mabadiliko ya kuwaingiza Didier Kavumbagu, Said Bahanuzi, na Nizar Khalfani ambao walichukua nafasi ya Hamis Kiiza, Jerson Tegete na Saimon Msuva.
Mabadiliko hayo yalizidi kuongeza kasi ya mashabuluzi langoni mwa African Lyon kwani dakika ya 70, Didier Kavumbagu aliipatia Yanga bao la tatu kwa mkwaju wa penati kufuatia mlinzi wa African Lyon Obina Salamusasa kuunawa mpira ndani ya eneo la hatari.
Dakika ya 80 Nizar Khalfani aliipatia bao la  nne kwa ustadi mzuri wa umaliziaji, akimalizia pasi ya Said Bahanuzi ambaye aliwazidi ujanja walinzi wa African Lyon na kupiga krosi hiyo iliyowapita walinzi na mlinda mlango Juma Abdul.
Mpaka mwisho wa mchezo Young Africans 4 - 0 African Lyon

Kocha mkuu wa Yanga Ernest Brndts amesema anashukuru timu yake  kupata kwa ushindi katika mchezo wa leo, kipindi cha kwanza washambuliaji wangu hawakuwa makini lakini kipindi cha pili timu ilibadilika sana hali iliyopelekea kuutawala mchezo kwa kipindi chote na kuongeza mabao mawili ya haraka.
Baada ya mchezo huu wa leo kikosi cha Young Africans kitaendelea na mazoezi yake kesho asubuhi katika uwanja wa Mabatini Kijitonyama ikiwa ni maandalizi ya mchezo unaofuata dhidi ya timu ya Azam FC februari 23 katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.

Young Africans: 1.Ally Mustapha 'Barthez', 2.Juma Abdul, 3.David Luhende, 4.Nadir Haroub'Cannavaro', 5.Kelvin Yondani, 6.Athuman Idd 'Chuji', 7.Saimon Msuva/Nizar
 Khalfani, 8.Frank Domayo, 9.Jerson Tegete/Didier Kavumbagu 10.Hamis Kiiza/Sadi Bahanuzi, 11.Haruna Niyonzima
African Lyon: 1.Abdul Seif, 2.Yusuf Mlipili, 3.Sunday Bakari, 4.Ibrahim Job, 5.Obina Salamusasa, 6.Abdulehan Gulam, 7.Amani Kyata, 8.Mohamed Samata, 9.Idd Mbaga, 10.Bright Ike, 11.Adam Kingwande

Katika michezo mingine ya ligi hiyo iliyochezwa leo, JKT Mgambo imeifunga Oljoro JKT mabao 2-0, Kagera Sugar imeifunga Coastal Union bao 1-0, Toto African imetoka sare ya mabao 2-2 dhidi ya Polisi Moro na Mtibwa Sugar imetoka suluhu na Ruvu Shooting.


TANZIA: SHEIKH NASSOR ABDALLAH BACHOO

UPDATE/TAARIFA MPYA

Waheshima  Taarifa Kamili ya Maziko ya Mpendwa Shekh wetu Nassor Bachu yatafanyika Kesho katika Msikiti wa Kikwajuni Saanne Asubuhi

Kwa taarifa ya jamaa wa marehemu waliitowa marehema amefarikia majira ya saa nne asubuhi ya yale, baada ya kuuguwa kwa muda mrefu,  marehemu alisafirisha Mjini Dar-es-Salaam kwa matibabu zaidi.kwa kipindi alikuwa akipata matibabu katika hospitali za Mjini Dar. hatima marehemu  amerejeshwa Zanzibar na kuendelea na matibabu.

Shekh. Nassor alikuwa akipata matibabu kwa jamaa zake nje kidogo ya mji wa Zanzibar katika maeneo ya Chukwani hadi mauti yanamkuta leo asubuhi alikuwa chukwani Zanzibar.

 Maziko yatafanyika kesho katika msikiti wa Kikwajuni na kuzikwa Kijijini kwao Donge Mkoa wa Kaskazini Unguja, Zanzibar.

Mwenyezi Mungu amlaze pema peponi

Innaa lillahi wainnaa ilayhi raajiuun.

Sheikh Nassor Abdalla Bachoo ametangulia mbele ya haki.

Allahumma thaabit-hu biqauli thaabit. Allahumma gh-firlahu warhamhu waafihi waaf-anhu.

Sheikh Nassor Abdalla Bachoo hatosahaulika kamwe kwa mchango wake mkubwa katika elimu ya Uislamu na maendeleo ya Uislamu kwa ujumla ndani ya Afrika Mashariki na ulimwengu kwa jumla.

Kwa niaba ya Familia yangu natanguliza mkono wa ta’azia kwa familia ya sheikh, ndugu, jamaa na Waislamu wote kwa kuondokewa na kiungo muhimu katika dini yetu tukufu ya Kiislamu.

Tunamuomba Allah Taala kwa utukufu Wake Ampokee sheikh miongoni mwa waja wake wema, Amsamehe madhambi yake na Amjazie penye upungufu. Ameen.

Tembelea bog: Miujiza-ya-quran na/au Facebook: Groups/Miujiza ya Quran
Kama kutakuwa na maswali tafadhali usisite kuwasiliana kwa email: miujizayaquran@gmail.com

Shukran

kitongoni.blogspot.com inaungana kuwaombeeni faraja nyote mlioguswa na msiba huu. Roho ya marehemu Sheikh Nassor Abdalla Bachoo ipumzike pema! AMIN!



TAARIFA YA KIFO CHA MSANII WA WANAUME HALISI


.

.
Taarifa ambazo millardayo.com imezipata muda mfupi uliopita ni kwamba msanii Baraka Sekela maarufu kama BK wa TMK Wanaume halisi amefariki usiku wa kuamkia leo, alikua amelazwa katika hospitali ya Muhimbili kwa tatizo la moyo.

ANGALIA MAZOEZI YA SIMBA KUJIANDAA NA LIBOLO NA MIPANGO YA KUENDA UINGEREZA

Tizi kali likiendelea wakati Simba wakijiandaa kwa mechi  dhidi ya mabingwa wa Angola, C.R.Libolo kwenye mchezo wa awali na endapo watafuzu basi watakutana na El Merrikh ya Sudan  kwenye hatua ya 16 bora hapo mwezi Machi 15, 16, 17.
 Tizi likindelea

 Kocha msaidizi Jamhuri Kihwelu Julio akisimamia tizi

Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Fedha ya Simba, Rahma Al Kharusi akiwa na Mwenyekiti wa Sunderland ya England, Ellis Short baada ya kukutana jana kwenye hoteli ya Hayat jijini Dar es Salaam.

 Baada ya kukutana, wawili hao walijadili kuhusiana na klabu hizo mbili kuanzisha uhusiano wa kibiashara pamoja na mafunzo na Simba imepata mwaliko.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Short alisema ushawishi wa Malkia wa Nyuki umechangia yeye kutoa mwaliko huo na anaamini timu zote zitafaidika.

"Mazungumzo yetu na Rahma yalikuwa mazuri sana, nimefarijika na ninaamini mwaliko niliotoa utakuwa mwanzo wa uhusiano mzuri kwa kuwa mwanamama huyu amenishawishi," alisema.

Malikia wa Nyuki ataiongoza Simba nchini England mwezi Machi ambako watatembelea viwanja vya Sunderland ikiwa ni pamoja na kujifunza uendeshaji wa klabu.

Awali Simba, ilijulikana kwa jina la Sunderland.


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU