Facebook Comments Box

Sunday, August 25, 2013

AJALI YA GARI LA MAFUGA ENEO LA RIVER SIDE DAR ES SALAAM JIONI HII

Gari la mafuta limepata ajali na kuingia mtaroni maeneo ya River Side Dar es Salaam jioni hii.
Hamna mtu yoyote aliepoteza maisha zaidi ya majeraha madogo kwa dereva wa gari hilo. Gari lilikuwa halina mafuta.
Mashuhuda wa ajali hiyo wanasema hij inatokana na mwendo kasi wa dereva wa gari hilo.
Chini ni picha za ajali hiyo



MSIMAMO WA LIGI KUU YA TANZANIA BAADA YA MECHI ZA JANA




VIDEO: ARSENAL WALIVYOIPIGA FULHAM


Arsenal vs Fulham 3-1 by FootyLight0

ASKARI WA JWTZ ALIETOROKA NI MZALIWA WA KAGERA: UTORO WAKE HAUNA TISHIO KWA TAIFA

JESHI LA wananchi wa Tanzania (JWTZ), limetoa ufafanuzi kwa kusema kuwa askari wake aliyetoroka jeshini Luteni Kanali Coelestine C. Seromba kwa kusema kuwa ni mzaliwa wa Kagera na siyo Rwanda.

Jeshi hilo limevitaka vyombo vya habari kuacha kuripoti taarifa potofu za afisa huyo ambaye alikuwa akikabliwa na tuhuma za makosa ya kijeshi na baadaye akatoweka wakati mchakato wa kumfungulia mashitaka ukiendelea.

Msemaji wa Jeshi hilo Meja Erick Komba Tamba akizungumza na wanahabari Dar es Salaam siku ya Jumamosi, alisema Seromba alitoroka Desemba 17 mwaka jana baada ya kuona kosa lililokuwa linamkabili linaweza kumtia hatiani, hatua ambayo amesema haina madhara kwa jeshi hilo. Kwa kuwa Lut. Kan. Seromba alitambua kuwa ametenda kosa na kuamua kutoroka, hatua ambayo ni kinyume cha sheria za JWTZ, ataendelea kutafutwa na akipatikana, atafunguliwa mashitaka kwa kosa la kutoroka JWTZ.

---

Blog moja inasema kutokana na serikali kupenda kuajiri vyeti badala ya watu, kuna kundi kubwa la askari wa majeshi ya Tanzania ambao siyo raia wa nchi hii na inasisitiza kuwa imewahi kuripoti uwepo wa raia wa Rwanda na Burundi katika majeshi ya Tanzania



 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU