Facebook Comments Box

Friday, August 16, 2013

DOWNLOAD WIMBO MPYA WA ZAY B MWANA DADA GAIDI UNAITWA MY BOY FRIEND




TRA ILALA YAKAMATA BIDHAA AMBAZO WAFANYABIASHARA WADAIWA KUKWEPA KODI KUPITIA MASHINE ZA EFD

2 
Meneja Msaidizi wa Mamlaka ya Mapato (TRA), Mkoa wa Ilala, Catherine Nkelebe (kushoto), akizungumza na waandishi wa habari  Dar es Salaam jana , kuhusu  TRA mkoa huo kukamata bidhaa mbalimbali za dukani ambazo wafanyabiashara wanadaiwa kukwepa kuzilipia kodi kupitia mashine za kielektroniki.
 
  3 
Marobota ya bidhaa mbalimbali yakiwa TRA Mkoa wa Ilala baada ya kukamatwa.


MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA), Mkoa wa Ilala jijini Dar es Salaam, imekamata bidhaa mbalimbali za dukani zenye thamani ya mamilioni ya fedha ambazo wafanyabiashara wamefanya hujuma ya kukwepa kulipa kodi kupitia mashine za kielektroniki (EFD-Electronic Data Enterchange).
 
Meneja Msaidi wa TRA Ilala, Catherin Nkelebe akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, alisema bidhaa hizo ambazo ni pamoja na sufuria, Khanga na mitumba zilikamatwa kufuatia msako unaoendeshwa na mamlaka hiyo kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi.
 
Nkelebe alisema wafanyabishara wamekuwa wakitumia mbinu nyingi kuwepa kulipa kodi kwa kukataa kutumia mashine maalum za kielektroniki zilizotolewa na TRA kwa kukata stakabadhi kwa wateja wanaokwenda kununua bidhaa katika maduka yao.
 
Alisema ujanja unaofanywa na wafanyabiashara ni kwamba mteja akienda kununua bidhaa hususan katika maduka ya jumla wanampatia stakabadhi yenye thamani ndogo wakati mzigo huo unakuwa na thamani kubwa.
 
“Unakuta mfano mteja amenunua bidhaa za thamani ya shilingi milioni moja lakini mwenye duka anampatia stakabadhi mnunuaji yenye thamani ya Sh. 200,000 ili kukwepa kulipa kodi,”alisema.
Nkelebe alisema hujuma nyingine inayofanywa na wafanyabiashara ni kutoa stakabadhi ambazo hazina maelezo yeyote au mchanganuo wa bidhaa zilizonunuliwa kwa lengo la kuiibia serikali mapato yake.
 
Aliongeza kuwa wafanyabishara wanafanya ujanja huo kwa hofu ya kwamba iwapo wataandika stakabadhi yenye malipo halali watakadiliwa kiwango kikubwa cha kodi  wakati siyo kweli kwani TRA haifanya hivyo kwani inamkadiria mtu kodi kulingana na biashara yake.
 
Alisema TRA kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi wataendelea kufanya msako wa wafanyabiashara wanaofanya hujuma hizo na kuchukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria.


NGASSA AHALALISHWA KUCHEZEA YANGA


Kwa mujibu wa Page ya mwandishi maarufu wa habari za michezo ndugu Edo Kumwembe amesema kuwa Mrisho Khalfan Ngassa amehalalishwa kuchezea Yanga na atarudisha hela asilimia hamsini ya gharama za Simba na amefungiwa mechi sita.
Hapo chini ni jinsi Bwana Edo Kumwembe alivyo andika:

CHINI NI HABARI HIYO KUTOKA VYANZO VINGINE:
 
Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imepitia usajili wa wachezaji wa klabu za Ligi Kuu ya Vodacom na kumuidhinisha Mrisho Ngasa kuchezea timu ya Yanga baada ya kukamilisha usajili wake.

Hata hivyo, Kamati hiyo chini ya Mwenyekiti wake Alex Mgongolwa imebaini kuwa Ngasa alisaini mkataba mwingine Simba (katika kipindi ambacho alikuwa na mkataba na Azam) ambapo anatakiwa kurejesha fedha alizopokea (sh. milioni 30) pamoja na fidia ya asilimia 50 (sh. milioni 15) ya fedha hizo kwa Simba.

Kamati pia imemfungia mechi sita za mashindano (kuanzia mechi ya Ngao ya Jamii), na anatakiwa awe amelipa fedha hizo ndani ya kipindi hicho cha kukosa mechi hizo. Akishindwa, hataruhusiwa kucheza hadi atakapolipa fedha hizo.

Vilevile Kamati imepitia pingamizi zote zilizowasilishwa kuhusu usajili wa wachezaji, kukatiza mikataba ya wachezaji na kuzitaka klabu husika ziwe zimetatua masuala hayo hadi Alhamisi (Agosti 22 mwaka huu).

Kwa upande wa wachezaji wa kigeni, Kamati imeagiza wasiruhusiwe kucheza hadi watakapopata Hati za Uhamisho wa Kimataifa (ITC) pamoja na vibali vya kufanya kazi nchini (work permits).

Kamati hiyo itakutana tena Ijumaa (Agosti 23 mwaka huu) ili kupata ripoti za pingamizi ilizoagiza ziwe zimefanyiwa kazi hadi Agosti 22 mwaka huu na kutoa uamuzi kwa pande ambazo hazikuafikiana.


WABUNGE 11 WANASURIKA KIFO BAADA YA BASI WALILO PANDA KUTAKA KUUNGUA

wabunge wakoswa ca547
Wakati msafara wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu ukielekea Wilayani Missenyi kukagua sehemu utakapojengwa uwanja wa Kimataifa wa Ndege wa Omukajunguti, gari aina ya Costa lenye namba za usajili T 570 BYU lilowabeba Waheshimiwa Wabunge 11 lilipata hitilafu na kutaka kuungua.
wabunge tena 5ee72
Ajali hiyo ilitokea eneo la Mwanzo Mgumu kilometa moja kutoka mpakani mwa Wilaya ya Bukoba na Wilaya ya Missenyi ambapo gari hilo aina ya costa lilianza kutoa moshi mwingi kwa upande wa nyuma wakati likiwa kwenye mwendo mkali na kuleta hofu kubwa kwa abiria walikuwemo ndani ya gari hilo.
Mara baada ya dereva kugundua kuwa gari analoendesha linataka kuungua alilisimamisha na kuwaambia abiria wake kuwa gari linaungua.
wabunge nao 9808e
Kwa mujibu wa wabunge waliokuwemo kwenye gari hilo, baada ya kuambiwa kuwa gari linaungua kila mmoja alifanya juhudi za kujiokoa, wengine wakipitia madirishani.
Kwa Bahati hakuna Mbunge aliyeumia isipokuwa Mhe. Batenga aliumia mkono kidogo baada ya kubanana sana mlangoni.
Baada ya kila mmoja kutoka gari hilo liliendelea kutoa moshi mzito sana lakini kwa halikushika moto na baadae lilizimika na kuacha kutoa moshi.
wabunge daah c0bab
Wabunge waliokuwemo katika gari hilo ni Rebbecca Mngondo (Arusha Viti Maalumu), Rita Kabati (Iringa Viti Maalumu), Mariam Msabaha (Zanzibar Viti Maalumu), Mhe. Batenga (Kagera Viti Maalumu), Mhe. Madabida (Dar es Salaam Viti Maalum), Clara Mwatuka (Mtwara Viti Maalumu).
Wengine ni Mzee Hussein (Zanzibar), Mussa Haji Kombo (Pemba Zanzibar), Abdul Mteketa (Jimbo la Kilombelo), Mutula Mutula (Jimbo la Tunduru Kusini).
Aidha Mwenyekiti wa Kamati Mhe. Peter Serukamba Hakuwemo katika gari hilo lilotaka kuungua.


AUDIO: SIKILIZA WIMBO WA KWANZA WA FIESTA 2013 NOOMA SANA (TWENZETU)




SHEIKH PONDA APELEKWA GEREZANI SEGEREA


Leo hii, Sheikh Ponda Issa Ponda (54) aliyekuwa amelazwa katika wodi ya Kitengo cha Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Upasuaji wa Mishipa ya Fahamu (MOI) alikokuwa akipatiwa matibabu, amehamishiwa katika gereza la Segerea.Sheikh Ponda bado anauguza majeraha yake ya mkono aliyoyapata huko Morogoro ila jeshi limemchukua na kumpeleka Segerea akamalizie kuuguza majereha huko huko Segerea.
Kwa mujibu wa mashtaka aliyosomewa akiwa MOI, Sheikh Ponda atalazimika kurudishwa tena mahakamani siku kesi yake itakapotajwa Agosti 28 mwaka huu, ambapo upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika.


VIDEO: KIJANA AKAMATWA NA MADAWA YA KULEVYA UWANJA WA NDEGE WA DAR ES SALAAM

Siku moja baada ya ziara ya kushtukiza ya waziri wa uchukuzi Dk. Harison Mwakyembe, kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar-es-Salaam, kiasi kikubwa cha dawa za kulevya kimekamatwa uwanjani hapo katika harakati za kusafirishwa kwenda nchi za nje.


 Chuma Kikikatwa ili kutoa Heroin iliyofichwa ndani yake.
Heroin ikionekana baada ya Chuma kukatwa kama unavyoona hapo pichani.



PICHA: WATU WALIO ULIWA NA JESHI LA MISRI

Unrest: Egyptians look for their relatives amongst the bodies of protesters who died yesterday at al-Imene mosque




Посмотреть изображение в Твиттере

Unrest: Egyptians look for their relatives amongst the bodies of protesters who died yesterday at al-Imene mosque

 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU