Facebook Comments Box

Saturday, January 26, 2013

HIVI VIBONZO NI KUTOKA KWA WAHARIRI WA VIBONZO MAARUFU TANZANIA







SIMBA, COASTAL UNION, AZAM ZAUA - MTIBWA YAPIGWA KWAO MANUNGU


Ngassa akipiga pushapu za kutambaa baada ya kufunga bao la tatu, aliyesimama jirani yake ni Haruna Chanongo na kushoto ni kipa Abdul Seif akitahari


Ngassa akiwa amejilaza kwenye nyavu baada ya kufunga.
Simba ya Dar es Salaam leo imeanza vyema mzunguko wa pili wa kuutetea ubingwa wao wa ligi kuu ya Tanzania bara baada ya kuichapa mabao 3-1 African Lyon katika dimba la uwanja wa taifa.
Pamoja na mechi ya Simba pia leo kulikuwa na mechi nyingine za ligi kuu ya bara na matokeo yalikuwa kama ifuatavyo

RUVU SHOOTING 1-0 JKT RUVU
 OLJORO 3-1 TOTO AFRICAN
 AZAM FC 3-1 KAGERA SUGAR
 MTIBWA SUGAR 0-1 POLISI MORO
 COASTAL UNION 3-1 MGAMBO SHOOTING

MTWARA GAS PIPELINE TO STRETCH UP TO MOMBASA THROUGH TANGA


 
The proposed Mtwara gas pipeline, which was scheduled to stretch from Mtwara to Dar es Salaam in Tanzania, will now reach as far as the Kenyan city of Mombasa, according to new East African Community (EAC) arrangements

The EAC has been working towards building a giant regional pipeline that will transport natural gas from Dar-es-Salaam to the Kenyan city of Mombasa via the Tanzanian port town of Tanga.

Speaking in Arusha, the EAC director of productive sectors, Nyamajeje Calleb-Weggoro, said the target was to again connect the pipeline with another trunk linking Mombasa and Kampala and later on to build the Kampala to Kigali and Bujumbura line to complete the cycle.

Recent discoveries of natural gas in deep sea have raised the total gas reserves in Tanzania to more than 7.5 trillion cu ft, volumes sufficient to allow Tanzania to export both natural gas and electricity throughout the EAC Region and beyond.

The feasibility study for the gas pipeline was initiated back in July 2010 under the execution of the Danish consulting firm, COWI in association with COWI Tanzania and Runji and Partners Consulting Engineers Limited of Kenya.

The African Development Bank had supported the EAC by financing the study.



MTWARA: NYUMBA ZA WABUNGE JENGO LA MAHAKAMA LATEKETEZWA KWA MOTO

  1. NEWALA: Nyumba ya Mkuchika inawaka moto -- Taarifa za redio mbao sasa  ni kwamba wananchi wanaendelea kufanya uharibifu mkubwa huko ambapo naambiwa wamevamia gereza wakafungulia wafungwa na kisha kupiga moto gereza. Polisi wamezidiwa na wamejifungia kituoni wanarusha mabomu yao tokea huko walikojificha maana nje hakutamaniki. Na wameshateketeza nyumba ya mama Anna Abdallah.
  2. Kikao cha dharura cha kamati ya ulinzi na usalama kinaendelea kwa kuwashirikisha maafisa wa polisi na maafisa usalama waliotoka Dar es Salaam kuongezea nguvu.
  3. Maaskari na makachero wawasili  Mtwara leo asubuhi na helkopta kuongezea nguvu.
  4. Hosteli ya wanafunzi wa chuo cha Utumishi maeneo ya Kiyangu B Mtwara yakoswa koswa kuchomwa moto kwa kile kinachodhaniwa kuwa na uhusiano na Hawa Ghasia mpaka sasa wanafunzi hawana mahala pa kukaa.  Kituo kidogo cha Polisi Cha Shangani mkoani Mtwara nacho chakoswa na moto. Ofisi ya Afisa Mtendaji Nkanaledi mkoani Mtwara nayo yavunjwa.
  5. Wananchi wamechoma moto mahakama ya Mwanzo na kuvunja vioo vya nyumba za waheshimiwa Hawa Ghasia (Waziri, TAMISEMI) na ya Mohamed Sinani (Mwenyekiti wa CCM Mkoa) zilizopo mtaa wa Sinani.
  6. Wakiwa katika mahakama ya mwanzo, Polisi walizingirwa na vijana waliokuwa wamebeba mawe na kufunga barabara zote za kuingia na kutoka Kituo Kikuu cha Mabasi na eneo la Soko Kuu, licha ya kufyatua hewani mabomu ya machozi. 
  7. Baadhi ya barabara za zimezibwa kwa kuchomwa matairi ya gari, na kuongeza hofu kwa wananchi.
  8. Hali imeshakuwa mbaya masasi taarifa zilizotufikia punde wamechoma eneo linaloitwa loliondo, ofisi za elimu na ofisi ya trafiki, inasemekana jamaa wameshavamia ofisi za halmashauri wengine wako njiani nyumbani kwa mama Ana Abdala, hapa Mtwara  mjini maduka yote eneo la soko kuu na stendi yamefungwa hakuna huduma, huko Newala , leo kuna mkutano mkubwa mchana huu wa kumkataa George Mkuchika.
  9. Vurugu zahamia wilaya ya Masasi mkoani Mtwara Nyumba ya Mbunge wa Masasi nayo yateketezwa kwa Moto hivi sasa...Madereva Bodaboda waandamana ...Vurugu zashamiri Mabomu Kibao..Hali ni tete







































































































































































































































































































 Kwa kile kinachoaminika kuwa ni kukua kwa MGOGORO WA GESI Mkoani Mtwara na Kusini kwa ujumla, usiku wa kuamkia leo Mahakama ya Mwanzo katika Manispaa ya Mtwara Mikindani imeteketezwa kwa moto huku nyumba ya Mbunge Hawa Gasia ikivunjwa vioo na kuchomwa motto wakati ile ya Mwenyekiti wa CCM Mtwara, ndugu Sinani ikiwa imevunjwa tu vioo.

Chanzo hasa cha vurugu hizo haziko wazi lakini wengi wanazihusisha na sakata la GESI kwani Hawa Gasia na Sinani wamekuwa kwa Muda Mrefu wakishutumiwa kwa kuchochea na kuridhia usafirishaji wa gesi hiyo kutoka Mtwara kwenda Dar es salaam. Uchomaji huo wa moto uliambatana na vurugu na ulipuaji wa mabomu ya machozi kutoka kwa polisi na hadi wakafanikiwa kuzima jaribio la uchomaji wa Kituo cha Polisi cha Shangani.

Wakati huohuo kuna taarifa kutoka Masasi zikieleza nako kuibuka tukio la chomachoma mchana huu wa leo ikihusisha uchomwaji wa Offisi za Serikali, Polisi, nyumba za Wabunge na Offisi za CCM. Hali ya Masasi inaelezwa kuwa ni tete zaidi kuliko ilivyokuwa hapa Mtwara Mjini usiku wa jana ingawaje napo palikuwa na kimuhemuhe cha mabomu ya machozi kutoka kwa polisi.

Bado mpaka sasa haileweki ni nini hasa hatma ya mgogoro huu, maana kwa upande wake Serikali inaonekana kushikilia msimamo wake uleule wa kutaka kusafirisha gesi hiyo wakati upande wa raia wakiwa na msimao wao wa GESI KWANZA MAISHA BAADAYE, kwa maana kutoridhia usafirishaji wa gesi hiyo ikiwa ghafi kupelekwa Dar es salaam.

Wito wangu kwa Serikali ni kuwa, muda ni huu wa kukaa na wananchi ili kujadiliana juu ya mstakabali mzima wa tatizo hili na kutafuta suluhu. Muda ni huu kwa sababu si vyema kuacha hali iendelee kuharibika ndipo tuje baadaye tulazimike kuunda tume za watu kuchunguzwa. Si vibaya kwa Serikali kukiri au kurudi kwa raia na kusema pale ilipoteleza na kutafuta ni namna gani na ni njia ipi sahihi ya kuliendea suala hili.

Ewe Mungu! Ibariki Tanzania, Wabariki Watanzania.

Hassani Samli,
Mtwara.
+255717340671
samlihassani@yahoo.com 



BREAKING NEWS: MRISHO NGASSA ASAINI YANGA RASMI

Mrisho Ngassa
 si mchezo wa kuvurugana akili, wala si hujuma ila ni hakika. Yanga imethibitisha 'kumsajili' winga machachari wa Simba, Mrisho Ngassa kwa mkataba wa miaka miwili.

Ngassa, ambaye alizaliwa Aprili 12, 1989 amechezea klabu tatu kubwa nchini: Yanga, Azam na Simba ingawa Kagera Sugar ndiyo iliyomfanya afahamike.

Ngassa, ambaye anachezea Simba kwa mkopo wa mwaka mmoja kutoka Azam FC, alitakiwa kujiunga na El Merreick ya Sudan mwishoni mwa mwaka jana, lakini akaingia mitini dakika za mwisho na kuchukuliwa na baadhi ya wadau wa Yanga ambako alisaini mkataba wa miaka miwili.

Mmoja wa wajumbe wa Kamati ya Usajili ya Yanga, aliithibitishia kitongoni jana Ijumaa kuwa, Ngassa amesaini mkataba na kikosi hicho kwa ajili ya msimu ujao wa Ligi Kuu Bara.

"Ninachoweza kuthibitisha ni kuwa Ngassa amesaini Yanga, masuala mengine ya mikataba na fedha utafahamishwa baadaye, lakini kusaini mkataba ni jambo ambalo ni uhakika wa asilimia 100," alisema.

Desemba mwaka jana, Mwanaspoti limewahi kuripoti kuhusu Ngassa kusaini mkataba wa kuichezea Yanga, lakini viongozi wa Jangwani hawakuwa tayari kuthibitisha.

Hata hivyo baada ya hali kutulia, Mjumbe huyo wa Kamati ya Usajili ya Yanga amethibitisha kuwa katika ligi ijayo, Ngassa atavaa jezi za kijani na njano.

Mwanaspoti linajua kuwa Ngassa amesaini mkataba wa miaka miwili na ametanguliziwa Shilingi 20 milioni, huku akisubiri kupewa fedha nyingine atakapoanza rasmi kuichezea timu hiyo ya Jangwani msimu ujao.

Hata hivyo, Simba kupitia kwa Makamu Mwenyekiti wake, Geofrey Kaburu imekuwa ikisisitiza kuwa Ngassa alisaini mkataba mwingine wa mwaka moja na Simba ambao utaanza Juni mwaka huu.

Ngassa aliichezea Yanga kwa misimu mitatu 2006 mpaka 2010 kabla ya kuhamia Azam ambako alidumu kwa misimu miwili na kutolewa kwa mkopo Simba msimu uliopita.

Simba ilimpa gari aina ya Toyota Verosa na Sh 12 milioni, lakini akiwa ndani ya miezi sita ya mwisho, ameamua kusaini Yanga, timu ambayo amekuwa akiipenda siku zote.

MRISHO NGASSA
Kuzaliwa: Aprili 12, 1989
Mahali: Dar es Salaam
Nafasi: Winga/mshambuliaji
Klabu
Kagera Sugar: 2005-2006
Yanga :2006-2010
Azam: 2010-2012
Simba: 2012-2013
Taifa: Tanzania


MKUU WA MKOA WA DODOMA AUAGA UJUMBE WA SEKRETARIETI YA CCM INAYOENDA KIGOMA KWA TRENI

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma,Dkt. Rehema Nchimbi (katikati) akiongoza mapokezi ya ujumbe wa Sekretarieti ya CCM,unaoelekea mkoani Kigoma mapema asubuhi hii kwa usafiri wa treni,ukiongozwa na Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM),Ndg. Abdulrahman Kinana (wa pili kulia) kwenye maadhimisho ya miaka 36 ya chama cha Mapinduzi CCM yatakayo adhimishwa mkoani humo.

Katibu wa NEC,Itikaji na Uenezi CCM,Nape Nnauye akizungumza na waandishi wa habari katika stesheni ya treni Mkoani Dodoma Mapema leo asubuhi.

 Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM),Ndg. Abdulrahman Kinana akizungumza na Wanachama wa CCM mkoani Dodoma waliokuwa wamefika Stesheni ya Dodoma asubuhi hii kuwalaki Wajumbe wa Sekretarieti ya CCM,wanaoelekea mkoani Kigoma kwa usafiri wa treni kwenye maadhimisho ya miaka 36 ya chama cha Mapinduzi CCM,Wajumbe wa Sekretarieti ya NEC wameondoka jana jijini Dar kwenda Mkoani Kigoma kuadhimisha miaka 36 ya Chama hicho.Kushoto kwake ni Katibu wa NEC,Siasa na Mahusiano ya Kimataifa,Dkt. Asha-Rose Migiro na kulia kwake ni Katibu wa NEC,Itikaji na Uenezi CCM,Nape Nnauye


 Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM),Ndg. Abdulrahman Kinana akiagana na baadhi ya WanaCCM wa Mkoani Dodoma waliofika kuwalaki na kuwatakia safari njema Wajumbe wa Sekretarieti ya CCM,wanaoelekea mkoani Kigoma kwa usafiri wa treni kwenye maadhimisho ya miaka 36 ya chama cha Mapinduzi CCM,Wajumbe wa Sekretarieti ya NEC wameondoka jana jijini Dar kwenda Mkoani Kigoma kuadhimisha miaka 36 ya Chama hicho.

Katibu wa NEC,Siasa na Mahusiano ya Kimataifa,Dkt. Asha-Rose Migiro  akiwa ndani ya treni asubuhi hii akiwapungia mkono WanaCCM wa Mkoani Dodoma waliofika kuwalaki na kuwatakia safari njema Wajumbe wa Sekretarieti ya CCM,wanaoelekea mkoani Kigoma kwa usafiri wa treni kwenye maadhimisho ya miaka 36 ya chama cha Mapinduzi CCM




MAANDAMANO YA GESI MTWARA NI MWAMKO WA WANANCHI

Tatizo linalojitokeza Mtwara isichanganywe na laana za rasilimali zinazoikumba bara la Afrika. Huu ni mwamko mpya ambapo wananchi wanatambua haki zao za msingi na kuamua kuyapigania, hasa rasilimali zao kwa lengo la kujikwamua kutoka kwenye umasikini unaowakabili. Serikali iliyo madarakani isiingize pamba masikioni na kuligeuza swala la kupingwa na wananchi kuwa la kisiasa. Ni vyema serikali ikajitathmini kwa umakini mkubwa na pia ikaheshimu maoni ya wananchi ili ijiokoe Desturi ya kutengeneza mikataba mikubwa kwa usiri na viongozi wa umma wasio na maadili, imewaletea wananchi wa Tanzania matatizo makubwa ya kiuchumi. Tatizo la Mtwara ni zao la udanganyifu kwenye mikataba yetu. Ni tatizo linalotoa nafasi ya kipekee kwa serikali yetu kujitathmini na kupitia upya sera zake za kiuchumu na uwekezaji, ambazo zimekuwa kandamizi, danganyifu na isiyo na tija kwa raia wa Tanzania. Kuna baadhi yetu ambao wanaweza kuyafananisha migogoro nchini Kongo na Nigeria na maandamano ya Mtwara. Kwa hakika Migogoro ya Kongo na Nigeria ni tofauti na huu wa Mtwara. Wa-kongo na Wanaigeria ni makundi ya kipiganaji ambayo yapo kwenye mapambano na serikali zao. Wanapigania uongozi na utawala wa nchi. Ni watu wenye silaha nzito zinazolenga kuzing’oa serikali zao, tofauti na wana mtwara wanaopigania haki na maendeleo ya kiuchumi. Wana Mtwara wanapinga ufisadi na dhuluma inayoendelezwa na serikali kupitia maandamano ya amani Wana Mtwara ni raia wa kawaida wasiokuwa na silaha yoyote isipokuwa nafsi zao. Wakufunzi wa historia watakubaliana nami kwamba, katika historia ya dunia, hakuna jeshi ambayo imeweza kuishinda nguvu ya umma, hasa pale wananchi wanapoamua kupigania haki zao kutumia njia ya amani. Mfano wa ufisadi unaopingwa na watu wa kusini mwa Tanzania ni ule wa gharama ya ujenzi wa bomba la gesi. Kwani vyombo vya habari vimenukuliwa vikisema kwamba, tathmini ya ujenzi kutoka mtwara hadi Dar-es-salaam, ilikuwa ni dola za kimarekani 600millioni, lakini cha ajabu, mwisho wa siku gharama hiyo imeongezeka na kufikia dola za kimarekani 1.2billioni. Wananchi hawawezi kunyamazia ufisadi kama huu. Na kwa mwenendo huu, nguvu yao inazidi kuongezeka na hakuna chochote ambacho serikali inaweza kukifanya kujinasua. Ni bora serikali ikakiri makosa na kuwashugulikia mafisadi waliojiusisha na huu hujuma dhidi ya watanzania. Kwani mwisho wa siku, hiyo hasara atakayebebeshwa ni mtanzania ambaye amechoswha na dhuluma pamoja na umasikini. Siyo fisadi aliyeficha fedha Uswisi Ugunduzi wa mafuta nchini Kanada umewaletea neema ya kiuchumi wananchi wa jimbo la Alberta, na uchumi wa Kanada kwa ujumla. Malipo ya dola 120 za kimarekani kwa lisaa limoja kwa wahitimu wa sekondari, ni ya kawaida. Wakazi wa Alberta wanafurahia rasilimali zao. Makampuni ya mafuta yanashiriki kikamilifu kusaidia miradi ya kijamii. Lakini katika hali ya kusikitisha kule Tarime (Nyamongo) wakazi wa maeneo yale wamekuwa masikini zaidi ya walivyokuwa kabla ya wawekezaji kuchukua ardhi yao. Vyanzo vyao vya maji vimechafuliwa na havifai tena, mifugo na hata baadhi ya wakazi wanakufa na mangonjwa yasiyojulikana Umasikini, ukiwa, na ukosefu wa ajira unatawala Tarime, kwani hata wachimbaji wadogo wadogo hawana ardhi tena ya kuchimba, huku wageni wakipewa ajira ndogo ndogo kama za kuendesha malori ya mchanga ambazo zingefanywa na wazawa wa Tarime. Inasikitisha kuwaona Wakenya, Wa Afrika Kusini, Wa Kanada na Wa Australia wakiendesha hayo malori huku wakazi wa Nyamongo wakionekana kama adui kwenye ardhi yao. Na hayo ndio baadhi ya matatizo ambayo serikali yetu imeyafumbia macho, hasa serikali inapoamua kuwatumia polisi kuwaua raia wanaodai haki yao ya kupata riziki. Wana Mtwara wanaandamana kudai maendeleo ya kiuchumi. Watu wa kusini wameiona gesi asilia kuwa ndio njia pekee ya kujikwamua kutoka kwenye umasikini. Wameshuhudia ndugu zao kule Tarime wanavyonyanyaswa na serikali na hata kuuwawa na polisi. Hawataki tena ahadi. Wanachokita ni utekelezaji utakao boresha maisha yao. Serikali isifanye kosa ya kupuuzia haya madia . Wasithubutu kuyaletea siasa au kajaribu kutumia nguvu ili kuwaziba midomo wanaharakati wanapinga gesi kupelekwa Dar-es-salaam, badala yake, serikali iwe makini katika kutafuta chanzo cha matatizo na suluhisho la kudumu Serikali makini itajiuliza maswali ya msingi kama vile ni kwa nini wananchi hawataki gesi isafirishwe kwenda Dar-es-salaam. Katika kujitathmini, bila shaka itapata majibu mbalimbali . Itagundua kwamba tupo katika nyakati tofauti. Wakati wa kizazi cha Intaneti, hasa vijana wenye muamko na hamasa wasiotaka kuwatwika wengine lawama ya matatizo yanayowakabili. Serikali itagundua kizazi cha kipekee kisicholaumu wengine kwa ufukara wao. Kizazi kisichoogopa mabomu ya machozi, maji ya kuwasha au risasi za moto. Kizazi kisichoshabikia uomba-omba. Serikali itagundua kizazi kinachotaka kujikwamua kutoka kwenye umasikini kutumia rasilimali na vipaji vyao. Ni kizazi kipya kinachotaka ajira, elimu bora, huduma bora za afya na miundombinu inayoridhisha. Ninamaanisha kizazi kinachoelewa wazi kwamba, WACHINA hawana upendo nao, ila WACHINA wanapenda rasilimali zao. Watu wa kusini wamegundua kwamba hadithi za Abunuwasi haziishi, na uhakika wa kuishi maisha ya neema ni lazima yaanzie kwao wenyewe kwa kuamka kutka usingizini. Na kwa hakika, wanakusini wameamka. Na kama serikali haitashugulikia madai yao, basi mwisho wa hiyo serikali siyo swala la mjadala. Wanakusini wamegundua kwamba, ni lazima “waamke” na kujitegemea badala ya kusikiliza ahadi ambazo wamekuwa wakiyasikia kwa miaka 50 iliyopita. Waheshimiwa Mwakyembe, Kagasheki, Magufuli na Muhongo wanajulikna kuwa wachapakazi wasiowaonea aibu majambazi ya kiuchumi -Mafisadi-. Lakini hawa viongozi wakiendelea kufanya kazi katika mazingira ya kuzungukwa na majambazi ndani ya serikali, na wanasiasa wasiokuwa na nidhamu katika kusimamia rasilimali za umma. Basi watabaki kuwa mateka wa mafisadi ingawa wengi wa hao mafisadi, serikali inawahamu. Kizazi cha simu za mikononi na ujumbe mfupi, na mitandao ya kijamii wameamka kutoka usingizini, na kasi yao ni ya kutisha. Hakuna wa kuwazuia. Hawataki propaganda za kisiasa na misaada ya KICHINA ambayo mara nyingi ndio chimbuko la ufisadi tunayoiona nchini kwetu, kama hiyo ya Mtwara. Wametambua wanayoyataka na kwa muda wanaoutaka wao. Maandamano ya Mtwara ni moto utakaosambaa kwa kasi. Ni moto wa UAMSHO. Unawaamsha wananchi waliolala kujua haki zao za kimsingi. Serikali ijitathmini na kuyashugulikia kero za wananchi mapema. Mafisadi wasipewe nafasi kuiyumbisha nchi Mungu Ibariki Tanzania

John Mashaka
mashaka.john@yahoo.com

KITABU KIPYA CHA ADAM SHAFI (MWANDISHI WA KULI) KIMETOKA


 
Juma hili habari kwamba kitabu kipya cha mwandishi nguli, Adam Shafi (mwandishi wa vitabu vya Kasr ya Mwinyi Fuad, Kuli, Vuta Nkuvute na Haini) kimetoka ni za kushangilia sana.

“Mbali na Nyumbani” inaangalia maisha yake msanii huyu Ughaibuni takribani miaka 50 iliyopita.

Mara ya mwisho nilipomhoji Mzee Shafi, Desemba 2007 alikuwa bado anakiandika kitabu hicho ambacho alisema kitaelezea maisha yake ya ujanani.

Katika uchambuzi wa kitabu hicho, mwandishi hodari wa Kenya, Profesa Ken Walibora, anasema mtindo wake wa kuangalia tawasifu- ambapo mwandishi au mhusika anaelezea maisha yake haujaenea sana katika maandishi ya Kiswahili seuze ya Kiafrika. Hivyo anasema Walibora, ni jambo zuri la sisi wengine pia kulifanya.

Mbali na kutukuza kitabu hiki, Profesa Walibora anachangamkia namna maandishi na lugha ya Kiswahili inavyoendelea kukua duniani. Hivyo, kututaka Waswahili kuendelea kuandika na kujenga na kuimarisha KISWAHILI.



 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU