Facebook Comments Box

Thursday, October 23, 2014

SOMA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI TAREHE 23 SEPTEMBA 2014 HAPA


 
 



YP AZIKWA KATIKA MAKABURI YA CHANG'OMBE MADUKA MAWILI

Msanii wa Muziki wa Bongo Fleva Yesaya Ambikile au YP kama ambavyo yeye mwenyewe alipenda kujiita ambaye alifariki juzi katika hospitali ya Temeke amezikwa leo katika makaburi ya Chang'ombe maduka mawili baada ya mwili wake kuagwa katika viwanja vya Sigara.

Wasanii wa muziki huo pamoja na wale wa Bongo muvi walikuwepo kumsindikiza msanii huyo katika nyumba yake ya milele.
Wasanii waliokuwepo hapo katika viwanja vya Sigara wakiwa tayari kuuaga mwili wa mwenzao katika viwanja vya TCC - Chang'ombe, Dar es salaam. Kwa mbali wanaonekana Chege, Juma Nature, Keisha, Madee na wengine wengi.
Juma Kassim Kiroboto "Nature" akiufunua Jeneza ili wasanii pamoja na waombolezaji waanze kuuaga mwili huo.
Waombolezaji ambao ni wananchi mbali mbali wa Chang'ombe na Temeke kwa ujumla waliofika kumuaga na kumzika mwenzao Yesaya Ambikile YP.
 Mke wa Marehem YP Bi Sakina Robert akiwa na huzuni mwenye kilemba cheupe.
 Juma Kassim Kiroboto "Nature" akitoa neno la shukurani kwa niaba ya wasanii wenzake waliofanya kazi na Marehemu YP.
 Mtoto wa marehem akienda kuuaga mwili wa Baba yake YP.
 Msanii wa vichekesho Kitale a.k.a Mkude Simba akienda kuaga mwili.
 Mtitu William akipita kuaga mwili wa marehemu.







 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU