Facebook Comments Box

Monday, May 13, 2013

REGINALD MENGI KUTOA MILIONI 1 KWA KILA TWEET ITAKAYO MFURAHISHA KWA MWAKA MZIMA



Hapa akimuelekeza mmoja wa watumiaji wa mtandao huo wa kijamii jinsi ya kushiriki. Inatakiwa uzielekeze zote kwake ili azione.



Hapa akisisitiza Tweet zihusu upambanaji na umasikini

Akaeleza na kusudio lake

Kabla ya kuja na wazo hilo yeye mwenye aliwahi ku tweet kuhusu umasikini kwa jicho la tatu


MTUHUMIWA WA BOMU LA KANISANI OLASITI ARUSHA AFIKISHWA MAHAKAMANI

Mtuhumiwa wa kurusha Bomu kwenye Kanisa Katoliki la Mtakatifu Joseph, parokia ya Olasiti, Jimbo Kuu la Arusha, Victor Ambrose Calist amefikishwa chini ya ulinzi mkali wa jeshi la Polisi kwenye  Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha, mbele ya Hakimu Mkazi, Devota Kamuzora leo.

Ambrose amesomewa  mashtaka 21 ya kuua na kujaribu kuua  wakati wa uzinduzi wa kanisa hilo ambao mgeni rasmi alikua Balozi wa Vatican nchini, Askofu Mkuu, Fransisco Padilla  ambaye alikuwa na mwenyeji wake Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Arusha, Josephat Lebulu.

Katika hatua nyingine Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha,Liberatus Sabas amesema kuwa watuhumiwa watatu raia wa United Arab Emirates (UAE) Abdul Aziz Mubrak (30) ambaye ni mfanyakazi wa Mamlaka ya Mapato, Fouad Saleem Ahmed Hareez Al Mahri (29), Saeed Abdulla Saad (28) ambaye ni askari Polisi  na raia mmoja wa Saudia Arabia, Al Mahri Saeed Mohseens (29) wamekutwa hawahusiki na tukio hilo na wamekabidhiwa kwenye idara ya uhamiaji mkoani Arusha ili kuangalia kama waliingia kihalali nchini.

Sabas amesema watuhumiwa wengine bado wanahojiwa kuona namna gani wanahusika na kitendo hicho cha kigaidi.



MSANII LADY JAY DEE APOKEA HATI YA MASHITAKA LEO

 

MSANII wa muziki wa kizazi kipya, Judith Wambura Mbibo a.k.a Lady Jaydee (Pichani) muda si mrefu amepokea hati yake ya mashtaka kutoka katika mahakama ya Kinondoni ambapo ameshtakiwa na Mkurugenzi wa vipindi wa Clouds FM baada ya kuwa na kutofautiana kwa muda.
Jaydee ambaye alikuwa Baraza la Sanaa ambapo alikuwa akiongea katika jukwaa la wasanii, alipata ujumbe wa kuitwa mahakamani na alipofika alikabidhiwa hati hiyo ambayo mwenyewe alikataa kusema makosa aliyoorodheshewa, na kusema kwamba anataka kwanza awasiliane na mwanasheria wake.
Kikubwa ambacho aliweza kusema kwa waandishi waliokuwa wameongozana naye ni kwamba, kesi itaanza kuunguruma tar 27 mahakamani hapo.
Kati ya vielelezo alivyopewa na mahakama ambavyo alivionesha kwa baadhi ya waandishi ni pamoja na nakala za magazeti na nakala za Post za blog yake pamoja na tweets!



LWAKATARE AKOSA DHAMANA ARUDISHWA RUMANDE

Hakimu anayesikiliza Kesi ya Lwakatare (CHADEMA) katika mahakama ya Kisutu Mh. Katemana yupo likizo kwa wiki mbili na hivyo Mahakama imeshindwa kutoa dhamana kwa Lwakatare na kuipiga kalenda kesi hiyo mpaka Tarehe 27 Mei.

Hata hivyo, Mawakili wa Lwakatare wanafanya juu chini ili waweze kupata dhamana yake japo juhudi zinaonekana kugonga mwamba


PICHA YA BASI LA SPORT LILIVYOPATA AJALI LEO


KONDAKTA WA GARI HILO AKIANGALIA JINSI GARI LILIVYOHARIBIKA 
BASI LA SPORT LENYE NAMBARI ZA USAJILI T 157 ASZ LINALOFANYA SAFARI ZAKE KUTOKA DAR KWENDA DODOMA LIMEANGUKA ENEO LA MWIDU MKOANI MOROGORO JANA  NA KUSABABISHA KIFO CHA MTOTO MMOJA NA WENGINE KADHAA KUJERUHIWA.
MASHUHUDA WA TUKIO HILO WANASEMA CHANZO CHA AJALI HIYO NI MWENDO KASI NA DEREVA ALIKUWA ANATAKA KUMKWEPA MTU MMOJA ALIYEKUWA ANATENGENEZA BAISKELI KANDO KANDO YA BARA BARA HIYO

BASI LA SPORT LENYE NAMBA ZA USAJILI T157 ASZ MARA BAADA YA KUANGUKA ENEO LA MWIDU MKOANI MOROGORO 




BAADHI YA MASHUHUDA ENEO LA TUKIO




MASHUHUDA WAKIANGALIA ENEO LA AJALI

ENEO LA CHASES LINAVYOONEKANA

BAADA YA KUPINDUKA

GARI HILI LILIANZA KUPOTEZA MWELEKEO HAPA KABLA HALIJAPINDUKA 


HIZI NDIO SABABU ZITAKAZO CHELEWESHA MATOKEO YA KIDATO CHA SITA

Matokeo ya mtihani wa kidato cha sita yaliyotarajiwa kutangazwa mwezi  huu yatachelewa  ili kutoa nafasi kwa Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA),  kurekebisha matokeo mabaya ya mitihani  kidato cha nne ya mwaka jana yaliyofutwa na serikali  mwezi huu.

Matokeo ya kidato cha sita ambayo huwa yanatangazwa mwanzoni  mwa mwezi Mei mpaka sasa hayajatolewa  na kwamba hayatatangazwa mpaka matokeo mapya ya kidato cha nne yatakaporekebishwa rasmi.

Alipoulizwa  juu ya suala hilo, Naibu Waziri   wa Elimu na  Mfunzo ya Ufundi  Philipo Mulugo alisema ingawa wakati huu ndio unaopaswa yatangazwe matokeo ya kidato cha sita haitafanyika hivyo hadi yatangazwe matokeo mapya ya kidato cha nne baada ya kufutwa.

Hata hivyo, akasema huenda yakatolewa  pamoja au yakafuata wakati mwingine lakini mara baada ya  kukamilisha kazi ya kurejea na kusahihisha matokeo ya kidato cha nne.

"Siyo kwamba yamechelewa kwani muda wa kujiunga na chuo ni Septemba hivyo haitawaathiri kwa hilo," alisema Mulugo.

Kuhusu hatma ya wanafunzi wa kidato cha nne ambao wapo mashuleni wanaendelea na masomo ya kidato cha sita, alisema  kama kutakuwa na wanafunzi ambao wapo madarasani  shule zilizowasajili  zitakuwa hazijafuata mfumo wa elimu unavyoelekeza.

Alifafanua kuwa mfumo wa elimu kwa kidato cha nne ulibadilishwa na kwamba endapo mwanafunzi akifaulu anatakiwa kujiunga rasmi kidato cha tano  Julai na si vinginevyo.

Alisema licha ya  ucheleweshaji  wa matokeo  hali hiyo haikuwaathiri wanafunzi hao kwa kuwa ratiba ya kwenda masomoni  haijaanza kwa mujibu wa kalenda  ya shule ya serikali.

Serikali ilifuta matokeo ya kidato cha nne ya 2012 na kuiagiza Necta kuyaandaa upya kwa kutumia utaratibu wa usahihishaji na upangaji madaraja uliotumiwa mwaka  2011

Taarifa ilisema mfumo uliotumika  mwaka jana na kusababisha wanafunzi kushindwa vibaya haukufanyiwa utafiti na maandalizi ya kutosha kabla ya kutumika.

Matokeo hayo  yaliyotangazwa  mwezi  Februari mwaka huu yalionyesha kuwa asilimia 60 ya wanafunzi walishindwa mtihani.



WAARABU WALIOKAMATWA KWA KUSHUTUMIWA KULIPUWA KANISA ARUSHA HAWANA HATIA POLISI YAWAACHIA HURU

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI JESHI LA POLISI TANZANIA
 logo_tpf
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSIANA NA MAENDELEO YA UPELELEZI WA TUKIO LA MLIPUKO WA BOMU KATIKA KANISA LA MT. JOSEPH – OLASITI JIJINI ARUSHA LILILOTOKEA TAREHE 05/05/2013
Ndugu wanahabari, mtakumbuka kwamba mara ya mwisho nilipokutana nanyi niliwaahidi kwamba nitaendelea kuwapa mara kwa mara taarifa juu ta maendeleo ya upelelezi wa tukio la mlipuko wa bomu lililotokea katika kanisa katoliki la mtakatifu joseph mfanyakazi parokia ya olasiti tarehe 05/05/2013 na kusababisha vifo vya watu watatu(3) na wengine kudhaa kujeruhiwa.
Kama nilivyowaeleza hapo awali, baada ya tukio hilo jumla ya watuhumiwa tisa(9) walikamatwa na kuhojiwa kuhusiana na tukio hilo la mlipuko wa bomu kanisani. Watuhumiwa haoa ni victor Ambros Kalist, (20), dereva wa bodaboda na mkazi wa kwa Morombo; Yusuph Lomayani Josee (18) mwendesha bodaboda mkazi wa kwa Morombo na George Bathlomeo Silayo (23) mfanyabiashara na mkazi wa Olasiti.
Watuhumiwa wengine waliokamatwa ni raia watatu toka nchi za falme za kiaruabu (UAE) Abdul Aziz Mubrak (30) mfanyakazi wa mamlaka ya mapato katika falme za kiarabu, Fouad Saleem Ahmed Al Hareez Al Mahri (29) mfanyakazi wa kikosi cha zimamoto katika Falme za Kiarabu, Saeed Abdulla Saad (28) askali polisikitengo cha traffic katika falme za Kiarabu, pamoja na raia mmoja wa Saudi Arabia Al-Mahri Saeed Mohseens (29)
Rai hao wa kigeni walikamatwa pamoja na wenyeji wao wawili ambao ni raia wa tanzania wenye asili ya Yemen.  Majina ya watanzania hao ni Mohamed Suleiman Saad, (38) mkazi wa ilala jijini Dar es Salaam na Jasm Mubarak (29) mkaazi wa mtaa wa Bondeni jijini Arusha.
Uchunguzi wa kina uliofanywa na timu ya upelelezi ukihusisha taaasis nyingine za upelelezi FBI pamoja na INTERPOL kuhusiana na tukio hilo la mlipuko wa bomu kanisani umebaini kuwa raia hao wanne wa kigeni hawakuhusika katika shambulio hilo. Baada ya jalada la tukio hilo kufikishwa ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali Arusha – divisheni ya mashtaka imeelekeza kuwa watuhumiwa hao wakabidhiwe ofisi za idara ya uhamiaji mkoa wa arusha ili kuona kama kuna taratibu zozote za kiuhamiaji ziikiukwa na wageni hao wakati walipoingia nchini ili hatua stahili ziweze kuchukuliwa dhidi yao. Pia ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali imeandaa mashitaka dhidi ya victor S/O Ambros kalisti na amefikishwa mahakamani leo kwa tuhuma za mauaji na kujaribu kuua. Uchunguzi dhidi ya watuhumiwa waliosalia unaendelea kwa sasa tunao wataalamu kutoka kenye na Uganda ambao tunashirikiana nao katika upelelezi wa shauri hilo.
Aidha, hadi sasa idadi ya majeruhi wa tukio hilo la mlipuko wa bomu wanaoendelea kupata matatibabu katika hospitali mbalimbali ni 31 ambao kati yao 19 wanaendelea na matibabu katika hospitali ya mkoa mount Meru arusha, 4 katika hospitali ya St. Elizabeth arusha na wengine 8 katika hospitali ya taifa muhimbili jijini dar es salaam na taarifa zinaonyesha hali zao zinaendelea kuimarika.
Hata hivyo jeshi la polisi linaendelea kufuatilia taarifa za watuhumiwa wengine wanaohusishwa na tukio hilo ili waweze kukamatwa na kufikishwa mahakamani pia jeshi la polisi linaendelea kuwaomba wananchi au raiayeyote mwenye taarifa zitakazowezesha kubaini mtandao wa kigaidi nawatuhumiwa wengine wanaohusika na tukio hilo wajitokeze na kuwasilisha taarifa hizo; tayari mkuu wa jeshi la polisi (IGP) amekwishaahidi zawadi nono ya Tshs. 50,000,000/= kwa mtu yeyote atakayetoa taarifa hizo za siri kwa kukamatwa kwa watu hao. ASANTENI KWA KUNISIKILIZA.
IMETOLEWA NA KAMANDA WA POLISI MKOA WA ARUSHA
LIBERATUSI SABAS – ACP
TAREHE 13/05/2013.


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU