Facebook Comments Box

Sunday, March 31, 2013

ANGALIA SIRI YA MTUNGI SEHEMU YA 11 HAPA




LADY JAY DEE: CLOUDS FM NI WANAFIKI WANATAKA WAHONGWE NDIPO WAPIGE NYIMBO ZA WASANII

Lady Jay Dee
East African popular musician Lady Jay Dee ameamua kuwapa modongo Clouds fm kupitia Twitter kutokana na wimbo wake mpya uliotoka hivi karibuni Joto hasira kutopigwa katika radio hiyo. Jay dee ameandika kuwa radio ya watu isiyopiga nyimbo za wasanii wa watu ila wasanii wao tu. Angalia tweet za Queen of Bongofleva huyo.

"Radio ya watu isiopiga nyimbo za wasanii wa watu ila za wasanii wao tu, wasiopendwa na watu. "Anaedai kuianzisha bongoflava aliapa kuiua bongo flava. Sasa hata wasioijua Hiphop nao wana beef na Bongo flava! Damn !!"

Jay Dee pia anaonekana kujizatiti na kujiamini kuonyesha kuwa yupo kwa lolote yeye kama Komandoo Binti Machozi aliandika tena "Kill me if u can. Am on Fire, siogopi ng'oooooo Jipangeni, Ni kweli nimelamba sumu, lakini hainidhuru. Nakunywa maziwa daily, I will survive".

"Hee! Kuna watu wanadhani nili tweet nikiwa nimelewa, nilimaanisha na msimamo ni huo. Sitasema oooh kuna mtu ka hack ac yangu nooo its me"

" Kuna DJ flani alikuwa akipiga nyimbo nilizoshirikishwa akifika sehemu nilioimba mimi anakata verse yangu nimtaje?? Sa hivi anakat ya Prof J"

Hata hivyo si Jay Dee pekee kuanza kulaumu kwani wapo wanamuziki wengine wanaolaumu nyimbo zao kutokupigwa.

SOURCE:JAMII FORUM

ANGALIA MSIMAMO WA LIGI KUU BARA BAADA YA MICHEZO YA JANA TAR 30/03/2013, JUMAMOSI.


MSIMAMO WA LIGI KUU BARA BAADA YA MICHEZO YA JANA TAR 30/03/2013, JUMAMOSI


YANGA WAKAMATWA NA POLISI HUKO MKOANI MOROGORO


 Kikosi kamili cha timu ya Yanga kilichowekwa Korokoroni hapo jana Morogoro.(Yanga 0-Polisi 0)
 Kikosi cha Timu ya Polisi kilichoiwekea ngumu Yanga huko Morogoro jana kwa kutoka nayo bila kufungana.



UHURU KENYATA AIBUKA KIDEDEA MAHAKAMANI BAADA YA MAHAKAMA KUTOA UAMUZI KUWA UCHAGUZI ULIKUWA HURU NA WA HAKI

MAHAKAMA:
Kenya imeamua leo kuwa Uhuru Kenyatta alichaguliwa katika uchaguzi uliokuwa huru na wa haki,  na kutupilia mbali pingamizi lililowekwa na mgombea Raila Odinga aliyedai kwamba kura zilichakachuliwa.
Uamuzi huo umesafisha njia kwa Uhuru Kenyatta kuingia Ikulu. Anatarajiwa kuapishwa wiki ijayo Aprili  9, 2013 uwanja wa michezo wa Moi.

 Aliyekuwa Waziri Mkuu wa Kenya Mhe Raila Odinga amekubali uamuzi wa mahakama kuu, na kukubali yaishe (shingo upande?) kuashiria kwamba sasa mambo ni tambarare, na sio kama ilivyohofiwa awali kuwa kutatokea vurugu kama za uchaguzi wa mwaka 2007.

uamuzi wa mahakama hii kwamba walalamikiwa wa tatu na wa nne walichaguliwa kwa
haki”, alisema Jaji Mkuu wa Kenya Willy Mutunga, wakati wa kutoa uamuzi huu, akimaanisha Kenyatta na
mgombea mwenza na Naibu Rais William Ruto wameshinda kihalali.

Jaji Mkuu huyo alisema mahakama imetekeleza wajibu wake katika muda huo wa
kihistoria. “Sasa ni juu ya Wakenya, viongozi wao, taasisi za kijamii, sekta
binafsi na vyombo vya habari kutekeleza wajibu wao kuhakikisha umoja, amani,
utaifa na maendeleo ya taifa vinahifadhiwa”, aliongezea.

Rais mteule wa Kenya huyo alimshinda mpinzani wake kwa asilimia 50.07 dhidi ya
asilimia 43,28 za Odinga.


Saturday, March 30, 2013

MAKAMU WA RAIS DK. GHARIB BILAL ALIPOTEMBELEA ENEO LILIPODONDOKA GHOROFA JANA

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano waTanzania, Dk. Gharib Bilal akiwa eneo la tukio ili kujionea mwenyewe pamoja na kupata maelezo kutoka kwa mashuhuda wa ajali ya kudondoka kwa Jengo la Ghorofa 16 jana asubuhi katikati ya Jiji.
Makamu wa Raisi Dk. Gharib Bilal akipata maelezo kutoka kwa Kamanda wa JWT kama anavyoonkana katika picha.

Uokoaji ukiendelea.

Askari wa JWTZ wakisaidiana na Wananchi kusukuma Jenereta kubwa kulisogeza eneo la tukio ili eneo hilo liwe na mwanga wakati wa usiku na kuwezesha uokoaji kuendelea hadi jana usiku.


Friday, March 29, 2013

DIAMOND NA WEMA WATAMBIANA KATIKA PESA

Wakati WEMA ISACK SEPETU akifungua bonge la ofisi ya kuzalisha filamu, aliyekuwa Mpenzi wake Nasibu Abdul 'DIAMOND PLATNUM' amemjibu kwa kukamilisha mjengo wa maana uliomgharimu takriban Shilingi za Kitanzania Milioni 260 hivyo kwa pamoja kuonesha jeuri ya pesa walizo nazo.

WEMA alifanya uzinduzi wa ofisi yake hiyo bila kumpa taarifa Mama yake mzazi MARIAM SEPETU ili iwe bonge la Surprise kwake pamoja na watu mbalimbali kama vile Diamond Platnumz mwenyewe siku ya Jumatano iliyopita, Jina la Ofisi hiyo ni ENDLESS FAME FILMS iliyopo Mwananyamala- Komakoma Jijini Dar es Salaam.

Wema akiwa katika Ofisi yake hiyo Mpya ya Filamu
Wema akiwa Nyumbani kwake.
Wema akitoka kwake na gari yake aina ya Audi Q7.

Pamoja na Diamond kutoalikwa katika Sherehe za Uzinduzi wa Ofisi hiyo ya Wema lakini chanzo cha habari kinasema alikuwa katika harakati za kumalizia Mjengo wake ulioko Tegeta ili nae afanye uzinduzi rasmi. Akizungumza na kitongoni blog akiwa kwenye eneo ilipo nyumba hiyo ambayo ilikuwa ikifanyiwa ‘finishing’, Diamond alisema kuwa nyumba hiyo yenye thamani ya Sh. milioni 260 ni zawadi kwa mama yake SANURA KASSIM ‘SANDRA’.

“Mama yangu ndiyo kila kitu kwangu, mara ya kwanza nilimnunulia gari aina ya Toyota Alteeza nikaona haitoshi, nikaamua kumjengea hii nyumba ambayo itakuwa kama urithi wake hata nikifa leo,” alisema Diamond.

Diamond alimzungusha paparazi wetu na kujionea mjengo huo wenye vyumba vinne vya kulala ambavyo vyote ni ‘self contained’ (chumba chenye choo na bafu), studio kubwa ya kurekodi muziki, eneo ambalo limetengwa kwa ajili ya kujenga bwawa la kuogelea ‘swimming pool’, uwanja wa basketball na sehemu maalum ya kufanyia mazoezi (gym) ambapo alisema hadi ifikapo Septemba, mwaka huu kila kitu kitakuwa kimekamilika.
Hii ndiyo Nyumba ya Diamond anayojenga huko Tegeta na gari linalo onekana hapa ndilo gari lake anlotumia ukiachilia mbali Altezza aliyo mnunulia Mama yake.Ukiachana na ukubwa wa nyumba hiyo, uwanja ambao ameuzungushia uzio wa ukuta kuna nyumba nyingine ndogondogo tatu ambazo kwa mujibu wa staa huyo zitakuwa zikipangishwa.
Diamond akiwa Nyumbani kwake Sinza Mori anapoishi sasahivi.







MHANDISI MKUU NA MHANDISI WA WILAYA YA ILALA WASHIKILIWA NA JESHI LA POLISI KANDA MAALUM YA DAR ES SALAAM KUTOKANA NA KUPOROMOKA KWA JENGO LA GHOROFA 16


 Bango linaloonesha Ujenzi wa Ghorofa lililoporomoka leo Jijini Dar es Salaam, Jengo ambalo Mhandisi Mkuu na Mhandisi wa Wilaya ya Ilala wanashikiliwa na Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam kwa Uchunguzi zaidi.
Raisi Jakaya Mrisho Kikwete akipatiwa Maelezo na Kamanda wa Kanda Maalum ya Kipolisi Dar es Salaam Suleiman Kova wakati alipofika eneo la tukio ambapo Jengo la ghorofa 16 liliporomoka leo katika makutano ya Mitaa ya INDIRA GANDHI na ASIA.

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linawashikilia kwa pamoja MHANDISI MKUU WA JENGO na MHANDISI WA WILAYA YA ILALA kutokana na kuporomoka kwa Jengo la ghorofa 16 leo asubuhi Jijini Dar es Salaam.

Kwani Mhandisi wa Wilaya ya Ilala ndiye aliyetoa kibali cha kujengwa jengo hilo na Mhandisi Mkuu kuwa yeye ndiye msimamizi mkuu wa Ujenzi katika jengo hilo. Lakini pia MKUU WA MKOA wa Dar es Salaam amesitisha ujenzi wa jengo lingine lililopo pembezoni mwa Jengo lililoporomoka ambalo pia linasimamiwa na Mhandisi huyo huyo anayeshikiliwa na Jeshi la Polisi.

Kwa Habari zaidi juu ya Tukio hilo endelea kufuatilia kwa karibu kitongoni blog


POLISI ZANZIBAR: MTUHUMIWA WA MAUWAJI YA PADRI MUSHI AKAMATWA

Picture 
SOURCE:WAVUTI

BREAKING NEWS: JENGO LA GHOROFA 16 LAPOROMOKA KATIKATI YA JIJI LEO HII


Taarifa iliyotufikia hivi punde inasema:
Jengo la ghorofa 16 limeporomoka asubuhi ya leo katikati ya Jiji la Dar es Salaam katika mtaa wa INDIRA GHAND karibu kabisa na Msikiti wa SHIA na Kuua watu watatu(3) na Kujeruhi kadhaa, ila inasemekana idadi ya watu wanao kadiriwa kuwa wamefunikwa na kifusi ni 60 lakini 17 kati yao tayari wameokolewa na kukimbizwa hospitali kwa ajili ya kupata matibabu.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamanda KOVA amesema Uokoaji unaendelea japo vifaa muhimu vya kuokolea bado havipo lakini wataalamu mbali mbali kutoka Manispaa wapo pale kuhakikisha hali inafanikiwa na kuwaokoa watu zaidi walioko ndani.


 Mtoto Maisamali Kareem (6) ambaye ameokolewa kutoka katika madrasa ya Msikiti wa Shia ulioangukiwa na Jengo hilo
 Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk. Emmanuel Nchimbi (kushoto) akipata maelezo kutoka kwa Kamanda Suleiman Kova na Kulia kwake ni Kamanda wa Polisi mkoa wa Ilala, Marietha Minangi.

 Kamanda Kova akizungumza na James Mbatia (Mbunge, Mwenyekiti wa chama cha NCCR-Mageuzi)


Thursday, March 28, 2013

MBUNGE WA CHAMBANI SALIM HEMED KHAMIS AMEFARIKI DUNIA

Mbunge wa Chambani Salim Hemed Khamis,amefariki dunia muda mfupi uliopita katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili .Taratibu za kuusafirisha mwili kuelekea Pemba kwa mazishi zinafanyika.

INNA LI LAHI WA INNA ILAIHI  RAJIUUN
Breaking News:Mbunge wa Chambani  Salim Hemed Khamis,amefariki dunia muda mfupi uliopita katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili .Taratibu za kuusafirisha mwili kuelekea Pemba kwa mazishi zinafanyika.


CHUKUA MUDA WAKO KUMSIKILIZA MBOWE AKIZUNGUMZIA UONGOZI WA MAJIMBO




CHEGGE FT MALAIKA - USWAZI TAKE AWAY (OFFICIAL VIDEO)




HUYU NDIO BINTI WA MIAKA 16 ALIEFANYIWA UKATILI WA KUTISHA


Vituko mjini Iringa haviwezi kuisha kama jamii haitakubali kwa moyo mmoja kupambana na ukatili wa kijinsia. Huyu ni Binti ZAWAD KARIM miaka 16 mkazi wa mshindo nyuma ya banki ya NBC manispaa ya Iringa amepigwa na hatimaye kunyweshwa mkojo na mama yake mdogo aitwaye Ever ubamba.
 
Tukio lilikuwa hivi:
Zawadi  kimsingi anaishi na mama yake mzazi ambaye kwa kipindi hicho dada mtu huyo alikuwa anaumwa. Ever alikuwa nje na marafiki zake ndipo mama yake mdogo huyo akamwiita ndani ya nyumba yao hiyo wanayoishi mtaa wa mshindo.
Baada ya kumwita na kisha mtoto huyo kushindwa kusikia baadaye aliitika na kuingia ndani na  ndipo alipo ambiwa avue nguo zote na huyo mama yake  mdogo Ever .Baada ya muda mfupi Zawadi alianza kupokea kipigo kikali kutoka kwa mama yake  mdogo.
Katika kipigo hicho Zawadi  alipigwa pamoja na kunyweshwa mkojo kutoka kwa mama yake mdogo huyo.Zawadi ambaye ni mtoto wa kuzaliwa na Dada yake Ever inadaiwa kipigo hicho kimesababishwa na tuhuma kwamba eti familia hiyo haina mtoto kama yeye zawadi.


MSANII HUYU KAMTELEKEZA MTOTO WAKE KAHAMA NA KUJA DSM KULA RAHA

Naitwa sakina mimi ni mtangazaji wa radio hapa kahama. kuna habari nyingi ninazozipata huku nimeona nianze na hii...

huyu jamaa ambae nimeambatanisha picha zake ni msanii ambae anajiona maarufu anaetokea hukuhuku kahama ila kwa sasa yuko dar. anafanya kzi yake ya sanaa kwenye kampuni ya tuesday film entaiteinment.  jamaa huyu ambae amewahi kucheza filamu ya ''BEAUTIFUL'' kama mpenzi wake ray c aliyekuwa anaishi porini na ambae anajulikana sana kwa jina la 'TONY WA RAY C' anadaiwa kutelekeza mtoto wa kike wa miaka sita kwa maelezo yafuatayo...

HUYU NDIYE MSANII ALIYEKIMBILIA DSM NA KAUCHA MTOTO
juzi asubuhi alikuja dada mmoja hapa ofisini kwetu nikamkaribisha na akaanza kunielezea kwamba ye anaitwa 'JUSTINA IKOMBE'  alikuwa mchumba wa msanii huyo ambae jina lake kamili ni 'JANUARY NYANDA' , na hata wakafikia kuzaa nae mtoto mmoja wa kike anaejulikana kwa jina la 'TUNDA'  lakini baada ya dada huyu kujifungua jamaa huyo aliaga anakwenda dar. kufanya shughuri zake za sanaa na tangu hapo hana mawasiliano nae wala hajui binti huyu anaishije na mtoto. na mbaya zaidi ni kwamba mama wa mtoto anapojitahidi kumtafuta jamaa humkatia simu akionyesha kutokuwa na shida kabisa ya kuongea nae na mpaka hivi sasa mtoto amekua na anahitaji kwenda shule lakini hakuna msaada wowote...binti huyo alikuwa akiongea kwa uchungu kiasi cha kunihuzunisha hata mimi pia kama mwanamke mwenzake...nilimuomba namba za msanii huyo ambazo ni 0756 570907 na nilipopiga na kujitamburisha jamaa alinijibu matusi kama hana wazazi akidai kuwa hamfahamu huyo binti na wala yeye hana mtoto anaeishi kahama na wala yeye mwenyewe hajawahi kuishi kahama, na wakati amezaliwa kahama katika kijiji kinachoitwa 'kagongwa' na amesoma shule ya msingi 'KISHIMA'  na secondary 'ISAGEHE' na mpaka sasa wazazi wake wote wanaishi hapa kijijini 'kagongwa'
MTOTO WA MSANII  




















ENDELEA KUISOMA HAPA


KIPANYA NA UFUNGUO WA CHINA




HASHEEM THABEET AKIPIGA MKUNO WA UKWELI

HASHEEM THABEET AKIPIGA MKUNO WA UKWELI BAADA YA KUPATA PANDE KUTOKA KWA KELVIN DURANT



RAIS AZINDUA TAARIFA YA UTAFITI WA VISAHIRIA VYA UKIMWI NA MALARIA

r1Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikata ukanda kuzindua rasmi taarifa ya utafiti wa viashiria vya ukimwei na malaria mwaka 2012 leo Machi 27, 2013 katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es salaam.
Kulia kwake ni Waziri Mkuu Mhe Mizengo Pinda na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe Saidi Meck Sadiki. Kushoto kwake ni Mkurugenzi wa Tume ya Kudhibiri Ukimwi (TACAIDS) Mama Fatma Mrisho na
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), Mhe William Lukuvi.
 (PICHA NA IKULU)
r2Rais Jakaya Mrisho Kikwete akinyanyua juu baada ya  taarifa ya utafiti wa viashiria vya ukimwei na malaria mwaka 2012 leo Machi 27, 2013 katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es salaam.
Kulia kwake ni Waziri Mkuu Mhe Mizengo Pinda’,  Kushoto kwake ni Mkurugenzi wa Tume ya Kudhibiri Ukimwi (TACAIDS) Mama Fatma Mrisho.
r4Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipitia baada ya kuzindua rasmi  taarifa ya utafiti wa viashiria vya ukimwei na malaria mwaka 2012 leo Machi 27, 2013 katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es salaam.
Kulia kwake ni Waziri Mkuu Mhe Mizengo Pinda na kushoto kwake ni Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dkt Hussein Mwinyi, Waziri wa Fedha Dkt William Mgimwa.
r5Wadau kutoka sekta mbalimbali wakiangalia matangazo ya kupiga vita UKIMWI na Malaria wakati wa uzinduzi rasmi wa taarifa ya utafiti wa viashiria vya ukimwei na malaria mwaka 2012 leo Machi 27, 2013 katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es salaam.
r7Meza kuu ikimsikiliza kwa makini Mkurugenzi wa Tume ya Kudhibiri Ukimwi (TACAIDS) Mama Fatma Mrisho akisoma taarifa ya utafiti wa viashiria vya ukimwei na malaria mwaka 2012,  katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es salaam.


MBUNGE WA CUF SALIM HEMED KHAMIS AANGUKA GHAFLA



Mbunge wa chambani (CUF) Visiwani zanzibar Salim Hemed Hamisi ameanguka ghafla akiwa katika kikao cha kamati ya mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa katika ofisi ndogo za bunge jijini Dar es salaam wakati kamati hiyo ikiendelea na kikao chake

Mbunge huyo ambaye siku za hivi karibuni ametoka nje ya nchi kwa matibabu ya afya yake amefikwa na dhahama hiyo na kubebwa na baadhi ya wabunge kwa kushirikiana na baadhi ya wandishi wa habari kutolewa nje ya chumba cha mkutano na kupelekwa hospital ya taifa ya Mhimbili kwa uchunguzi na matibabu zaidi.

Mwenyekiti wa kamati ya bunge ya mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa Edward Lowasa amethibitisha kutokea kwa tukio hilo.


AZAM YAZIDI KUIKARIBIA YANGA YAITANDIKA PRISONS TATU BILA


 
  Pichani juu, nahodha John Bocco, Khamis Mcha na Humphrey Mieno wakimpongeza Kipre Tchetche baada ya kufunga goli la tatu

Timu ya Azam FC imezidi kusonga mbele kwenye ligi Kuu ya Vodacom baada ya kuichapa Tanzania Prisons 3-0 katika mchezo uliochezwa kwenye Uwanja wa Azam Complex Chamazi.


Azam FC imepata ushindi huo wa nyumbani huku mshambuliaji wake Kipre Tchetche akijiweka katika nafasi nzuri ya kutwaa kiatu cha dhahabu kwa kufikisha magoli 12 tofauti na wafungaji wengine kwenye ligi kuu.

Katika mchezo huo Azam FC walipata goli la kwanza katika dakika ya 17 kupitia kwa Kipre Tchteche aliyecheza vizuri crosi iliyopigwa na Khamis Mcha, shuti la Kipre lilimbabatiza kipa wa Prisons David Burhan na kutinga wavuni, matokeo yakawa Azam FC 1-0 Prisons.

Goli hilo lilidumu hadi mapumziko huku Azam FC wakiwa wameutawala mchezo kwa kutengeneza nafasi nyingi dk 23 John Bocco alishindwa kumalizia krosi ya Tchetche na mpira ukatoka nje, dk 34 Tchetche alipiga shuti likatoka nje na kupeleka timu zote mapumziko Azam FC ikiwa mbele kwa 1-0 dhidi ya Prisons.

Kipindi cha pili timu zilirejea uwanjani kwa kasi kila moja ikisaka bao la kumalizia mchezo, Kipre tena alipiga shuti likadakwa na kipa David wa Prisons, Humphrey Mieno naye alipiga shuti likaenda nje, huku Prisons dk 58 Elias Maguli alijaribu kufunga lakini shuti lake likatoka nje.

Wakipata nafasi nyingi na kukosa magoli ya wazi, dk 75 mshambuliaji mahiri wa Azam FC, John Bocco aliandika bao la pili kwa timu yake baada ya kuachia shuti la mbali lililongonga mwamba wa chini na kutinga wavuni, Bocco alibadili matokeo na kuwa Azam FC 2-0 Prisons.

Tchetche alizidi kulisakama lango la Prisons na dakika ya 84 alihitimisha kalamu ya magoli kwa kuandika bao la tatu akimalizia kazi nzuri ya Seif Abdalah ‘Karihe’, na kuipa Azam FC ushindi wa 3-0 dhidi ya TZ Prisons.

Katika mchezo huo Azam FC walifanya mabadiliko dk 65 alitoka Khamis Mcha akaingia Seif Abdalah ‘Karihe’, dk 70 akaingia Abdi Kassim ‘Babi’ kuchukua nafasi ya Humphrey Mieno na dk 73 Salum Abubakar ‘Sure Boy’ alipumzika nafasi yake ikachukuliwa na Ibrahim Mwaipopo, mabadiliko hayo yaliimarisha kikosi hicho na kucheza kandanda safi muda wote wa mchezo.

Prisons waliwatoa Nurdin Iss na Aziz Sibo nafasi zao zikachukuliwa na Peter Kazengele na Henry Mwalugala, mabadiliko yaliimarisha safu ya ushambuliaji lakini hayakuweza kubadilisha matokeo ya mchezo huo na kuicha Azam FC kupata ushindi huo mnono wa 3-0.

Kocha msaidizi wa Azam FC, Kali Ongala amefurahishwa na matokeo hayo na kiwango cha timu yake, amesema kilichopo sasa ni kuhakikisha hawapotezi  hata mechi moja katika michezo iliyobaki ya ligi kuu.

Azam FC kesho itaingia kambini kwa maandalizi ya kucheza dhidi ya Ruvu Shooting, mechi itakayopigwa Uwanja wa Mabatini, Mlandizi mkoani Pwani.

Azam FC, Mwadini Ally, Himid Mao, Waziri Salum, Luckson Kakolaki, Jockins Atudo, Michael Bolou, Tchetche Kipre, Salum Abubakar ‘Sure Boy’/Ibrahim Mwaipopo 73’, John Bocco, Khamis Mcha/Seif Abdalah ‘Karihe’ 65’ na Humphrey Mieno/Abdi Kassim ‘Babi’ 70’.
SOURCE:AZAMFC.CO.TZ


HUMUD KUELEKEA JOMO COSMOS WIKI HII

Kiungo mwenye mapafu ya mbwa Abdulhalim Humud Gaucho huenda akasafiri kuelekea bondeni Afrika ya Kusini wikiendi hii kufuatia kupata nafasi ya majaribio kwenye timu ya Jomo Cosmos aliyowahi kuchezea watanzania mengine Nteze John na Ally Shah siku za nyuma.

Cosmos inayomilikiwa na kocha wa zamani wa Bafana Bafana Jomo Sono imempa nafasi hiyo humudi baada ya kufanyiwa mipango na uongozi wa Azam FCkatika kutekeleza sera yake ya kutengeneza uwanja mkubwa kwa wachezaji wa kitanzania kwenye ligi mbalimbali zinazoendeshwa kisasa.

Cosmos ambao wapo kwenye kampeni ya kurejea PSL watahitaji huduma ya Humud msimu ujao ambao Jomo Sono ameahidi kuwa watakuwa wakicheza PSL
SOURCE:AZAMFC.CO.TZ


Wednesday, March 27, 2013

MAHAKAMA YAAMURU MATOKEO YA URAIS KENYA YAHESABIWE UPYA KATIKA VITUO 22 KATI YA 33


Nairobi. Mahakama ya Juu (Supreme Court) ya nchini Kenya imeagiza kuchunguzwa kwa fomu 34 za matokeo ya uchaguzi wa rais kutoka katika vituo vyote 34,400, vilivyotumika kupigia kura katika Uchaguzi Mkuu wa nchi hiyo uliofanyika Machi 4, mwaka huu.
Kadhalika mahakama hiyo jana iliagiza kuhesabiwa upya kwa kura za urais katika vituo vya kupigia kura 22 kati ya elfu 33 vilivyolalamikiwa na aliyekuwa mgombea urais wa Muungano wa Cord, Raila Odinga.
Katika malalamiko yake yaliyowasilishwa katika mahakama hiyo kupinga Uhuru Kenyatta kutangazwa mshindi wa urais katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika Machi 4, Odinga alidai kuwa vituo hivyo 22 kura zilizopigwa zinazidi idadi ya wapigakura walioandikishwa.
Akisoma uamuzi huo kwa niaba ya majaji wenzake watano, Jaji Smokin Wanjala alisema kwamba uhesabuji kura wa vituo hivyo utafanyika leo kuanzia saa 2.00 asubuhi kwa lengo la kubaini ukweli kuhusu madai hayo.
“Matokeo ya kura zitakazohesabiwa katika vituo hivyo 22 yawasilishwe katika mahakama hii Jumatano, saa 10.00 jioni,” alisema Jaji Wanjala.
 
Kikao hicho, ambacho Jaji Mkuu wa Tanzania, Mohamed Othman Chande amealikwa kama mwangalizi, ni cha awali kabla ya kesi hiyo kuanza kusikilizwa rasmi keshokutwa (Alhamisi) na kuendelea kwa mfululizo hadi kufikia uamuzi ikiwa madhumuni yake.
Lengo ni kupitia madai yaliyowasilishwa mahakamani hapo na pande zote zinazohusika na kuamua mwenendo wa kesi utakavyofanyika.
Ukiachilia mbali kesi iliyofunguliwa na Odinga kupinga Kenyatta kutangazwa mshindi wa uchaguzi huo wa tano tangu kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi hapa Kenya, kuna kesi nyingine ambayo imefunguliwa na muungano wa mashirika yasio ya kiserikali, `The African Centre for Open Governance’ (Africog).
Katika kesi hiyo inayorushwa moja kwa moja na vituo kadhaa vya televisheni nchini Kenya, Africog inahoji uhalali wa uchaguzi huo.

“Kesi yetu haihusiani na nani ameshinda au kushindwa bali jinsi umma ulivyoshindwa, tumepoteza ahadi ya uchaguzi uliowazi,” alisema Gladwell Otieno, Mkurugenzi Mtendaji wa Africog.
Kesi ya tatu ambayo imefunguliwa na wajumbe wa timu ya kampeni ya Kenyatta, mwanaharakati katika mitandao ya kijamii Dennis Itumbi na Moses Kuria wanaopinga uamuzi wa Tume Huru ya uchaguzi na Mipaka (IEBC) ya kujumuisha kura zilizoharibika wakati wa kujumlisha kura za wagombea urais.
Katika uamuzi wake, mahakama iliamua kwamba kesi zote tatu zitaunganishwa kuwa moja, huku ile iliyowasilishwa na Odinga ikiwa ndiyo kinara wa kesi zote.
Pia mahakama iliamuru Muungano wa Vyama vya Siasa wa Cord na Jubilee kuteua mawakala 10 kila mmoja ambao watakula kiapo mahakamani hapo kabla ya kuanza kuhesabu upya kura hizo.
Katika uamuzi wake jana jioni, mahakama hiyo ilikubali ombi la Mwanasheria Mkuu wa Kenya, kushiriki katika kesi hiyo kama rafiki wa mahakama na siyo mdaiwa kama ilivyokuwa awali. Wakili wa Cord, George Oraro alikubali uamuzi huo licha ya kuupinga awali.


ALIYEMGONGA TRAFIKI ENEO LA BAMAGA NA KUMUUA AFIKISHWA MAHAKAMANI




 Jackson  Simbo anayedaiwa kumgonga kwa gari marehemu trafiki Elikiza Nko wiki iliyopita katika taa za kuongozea magari za Bamaga-Mwenge  jijini Dar ss Salaam amepandishwa kizimbani leo katika mahakama ya Wilaya ya Kinondoni. 

Mshitakiwa huyo ameachiwa kwa dhamana hadi kesi hiyo itakapo tajwa tena Aprili 15 mwaka huu.


MWANAFUNZI WA KITIVO CHA SHERIA UDSM AJINYONGA


Picha hii kwa hisani ya Maktaba:

  Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) mwaka wa pili Kitivo cha Sheria, Joseph Bernadina (25), amejinyonga kwa kutumia kamba na kukutwa ameifunga juu ya mti, katika eneo la Yombo chuoni hapo.

Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Utawala, Profesa Yunus Mgaya, alithibitisha  kutokea kwa tukio hilo na kwamba alipata taarifa hizo jana asubuhi.

Aliongeza kuwa Jumamosi iliyopita alipokea simu kutoka kituo cha polisi cha chuo hicho akielezwa kuwa kuna mwanafunzi alitishia kujiua, lakini aliwahishwa hospitali na kupatiwa ushauri kutoka kitengo maalum cha washauri wa chuoni hapo na kuruhusiwa Jumapili.

“Nilikuja tena kushituka leo asubuhi napokea simu kutoka kwa mshauri wa wanafunzi kuwa kuna wanausalama wamemkuta mwanafunzi akiwa amejinyonga juu ya mti huku akiwa na karatasi kwenye mfuko wa sharti ikimtambulisha pamoja na ujumbe uliosema, kifo chake kisihusishwe na mtu yeyote kwani amejiua kwa ridhaa yake --asisumbuliwe mtu yeyote kwani nimefanya hivi kwa maamuzi yangu mwenyewe pia nizikwe kwetu--” alisema.

Profesa Mgaya alisema taratibu za mazishi zinaendelea kufanywa na Uongozi wa chuo kwa kushirikiana na ndugu wa marehemu na kwamba Chuo kitagharamia kuusafirisha mwili kama alivyoomba katika ujumbe aliouacha wa kupelekwa wilayani Ludewa Mkoa wa Iringa.
 
Naye rafiki wa marehemu, Daniel Mwamlima, alisema marehemu hakuwahi kuzungumza chochote kilichoashiria kuwa ana matatizo wala mgogoro na mtu yeyote.  Alisema walimuacha hospitalini Jumamosi na kesho yake kumchukua, lakini  baadaye aliwatoroka.

“Sasa leo (jana) asubuhi tulipata taarifa za mwanafunzi kujinyonga mbaya zaidi tukakuta ni yeye,” alisema Mwamlima.

Waziri Mkuu wa Serikali ya Wanafunzi wa chuo hicho (DARUSO), Yasini Athumani, alisema wamezipokea taarifa hizo kwa masikitiko makubwa.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Charles Kenyela, alithibitisha kutokea kwa tukio na alisema uchunguzi wa awali umebaini kwamba marehemu aliwahi kuwa na historia ya kwenda Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa ajili ya kupata matibabu ya ugonjwa wa msongo wa mawazo.

Source: WAVUTI

Tuesday, March 26, 2013

ZITO KABWE, IDD AZAN NAO WAMALIZA MAFUNZO YAO JKT MGAMBO 835KJ - TANGA





Mbunge wa Kigoma CHADEMA, Zitto Kabwe pamoja na Wabunge wenzake kadhaa vijana leo wakemaliza rasmi mafunzo yao ya awali ya JKT katika kambi ya Mgambo 835KJ kilichopo Mkoani Tanga.

Pichani juu ni Zitto Kabwe akijiandaa kwenda katika gwaride la mwisho na picha chini akiwa shambani pamoja na Mbunge mwenzake  Iddi Azan, Abdallah haji, Raya Ibrahim na Antony Mbassa kambi ya Mgambo 835KJ.
Aidha Zitto Kabwe amesema anafuraha isiyo na kifani kumaliza mafunzo hayo na ameweka historia kubwa katika maisha yake leo hii. Anapasha zaidi katika wakati wa Zoezi la kulenga shabaha alifanikiwa kulenga risasi 3 akiwa amelala, 3 akiwa amepiga magoti na 1 akiwa amesimama. 


HATIMAYE WABUNGE WAMALIZA MAFUNZO YA MUDA MFUPI YA JKT RUVU

8E9U3088Amiri Jeshi Mkuu,Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi cheti cha kuhitimu mafunzo ya muda mfupi kwa viongozi mbunge wa viti maalum Ester Bulaya leo katika kambi ya RUVU JKT.Rais Kikwete amefunga rasmi mafunzi hayo leo  yaliyofanyika kwa wiki tatu.
8E9U3121


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU