Saturday, September 20, 2014
TFF YAITAKA YANGA KUWASILISHA RASIMU YA KATIBA YAKE
Shirikisho
 la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limeitaka klabu ya Yanga kuwasilisha 
rasimu ya Katiba waliyoipitisha, kwa kuzingatia kuwa Muhtasari wa kikao 
cha Mkutano Mkuu wao wa Juni 1 mwaka huu umeainisha baadhi ya 
marekebisho waliyofanya kwa tulivyowaelekeza.
Yanga 
wanatakiwa kuwasilisha rasimu hiyo kabla ya Oktoba 5 mwaka huu. Ikiwa 
itakubaliwa na TFF, itapelekwa kwa Msajili wa Klabu na Vyama vya Michezo
 ili waweze kufanya uchaguzi wa viongozi wao. 
Subscribe to:
Comments (Atom)



