Facebook Comments Box

Saturday, October 5, 2013

MAN CITY YAJIPOZA MACHUNGU YA KUFUNGWA NA BAYERN MUNICH, YAIKUNG'UTA EVERTON 3 - 1


Klabu ya Manchester City imemaliza rekodi ya Evertonkutofungwa katika Ligi Kuu ya England, baada ya kuifunga mabao 3-1 jioni hii.
 
Aston Villa na Bayern Munich Ziliwafanya City waingie kwa hasira leo na kipa wao Joe Hart na kufanya kweli Uwanja wa Etihad Stadium
 
Romelu Lukaku aliifungia Everton bao la kuongoza dakika ya 16, lakini Alvaro Negredo akasawazisha dakika moja baadaye na Sergio Aguero akafunga la pili kabla ya mapumziko.
 
Tim Howard akajifunga dakika ya 69, akitoka tu kuokoa penalti ya Aguero.
 
Kikosi cha Manchester City kilikuwa: Hart, Zabaleta, Kompany/Nastasic dk35, Lescott, Kolarov/Clichy dk58, Toure, Fernandhino, Milner, Negredo, Silva, Aguero/Nasri dk78.
 
Everton: Howard, Coleman, Jagielka, Distin,  Baines, Mirallas/Deulofeu dk62, McCarthy, Naismith, Osman/Gibson dk62, Barkley, Lukaku/Kone dk82.
Sergio Aguero
Sergio Aguero akishangilia bao
Everton City
Romelu Lukaku
Alvaro Negredo
Alvaro Negredo
Manchester City's Sergio Aguero
tim howard
Manchester City goalkeeper Joe Hart
Manchester City's Sergio Aguero
Joe Hart
Joe Hart
Everton City
City Everton
Manchester City captain Vincent Kompany



HAMIS TAMBWE AENDELEA KUWA KINARA WA UFUNGAJI HUKU RUVU IKIIPUNGUZA KASI SIMBA TAIFA


Hamis Tambwe akishangilia moja ya mabao yake.

LIGI Kuu ya Vodacom Tanzania Bara imeendelea leo, huku vinara Simba SC wakipunguzwa kasi kwa sare ya 1-1 na Ruvu Shooting Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Ruvu ndiyo waliokuwa wakwanza kupata bao la kuongoza katika dakika ya nane tu ya mchezo kupitia kwa Saidi Dilunga 'Said Magoli' na Simba kusawazisha kwa penati katika dakika ya 51 ya mchezo baada ya Betram Mombeki kuangushwa ndani ya eneo la hatari ndipo Hamis Tambwe alipoukwamisha mpira wavuni na kufunga bao lake la nane katika ligi ya vodacom Tanzania Bara.
 
Hata hivyo, wachezaji wa Ruvu Shooting walimzonga refa Mohamed Theophil wakipinga penalti hiyo, kabla ya kulainika na kukubali ipigwe na Mrundi Tambwe akaenda kufunga bao lake la nane ndani ya mechi saba katika msimu wake wa kwanza Simba SC.
 
Matokeo hayo, yanaifanya Simba SC itimize pointi 15 baada ya mechi saba na kuendelea kushikilia usukani wa Ligi Kuu. 
 
Beki wa Coastal Union, Juma Nyosso akimdhibiti mshambuliaji wa Azam FC, John Bocco 'Adebayor' katika mchezo wa leo, Uwanja wa Mkwakwani.   



Azam pia wakitoka sare ya bila kufungana na Coastal Union Uwanja wa Mkwakwani, Tanga ikiwa ni sare yao ya nne katika ligi hii, sare zingine ni zile za mechi kati ya Mtibwa & Kagera Sugar na ile ya Ashant.
 
Uwanja wa Mkwakwani, Tanga mechi ilikuwa kali, ilitawaliwa na vurugu za mashabiki tangu hata kabla mchezo haujaanza. Kosa kosa zilikuwa za pande zote mbili, safu ya ushambuliaji ya Coastal ikiongozwa na Mganda, Yayo Lutimba na Pius Kisambale na Azam ikiongozwa na John Bocco, Mganda Brian Umony na Kipre Tchetche wa Ivory Coast.

Refa Andrew Shamba aligeuka kituko kipindi cha pili, baada ya kuwapa kona isiyostahili Azam na ilipopigwa wakafanikiwa kupata bao, lakini akakataa bao hilo.

Baada ya kutoa kona hiyo, beki wa Azam Erasto Nyoni alienda kupiga vizuri ikaunganishwa nyavuni na John Bocco kwa kichwa dakika ya 71, lakini Shamba akaamuru mpira uwekwe chini upigwe kuelekea lango la Azam- kana kwamba kuna faulo ilichezeka.

Mshika kibendera namba mbili, Hassan Zani alisababisha mchezo kusimama kwa dakika tatu ili apatiwe huduma ya kwanza, baada ya kupigwa chupa na mashabiki wa Coastal Union dakika ya 43.

Beki wa kulia wa Coastal Union, Hamad Hamisi alitolewa nje kwa kadi nyekundu dakika ya 70 baada ya kumpiga kichwa Kipre Tchetche wa Azam FC. Tukio hilo lilifuatia  majibizano na kusukumana kwa wachezaji hao.

Mshambuliaji wa Azam, Kipre Tchetche alikutana na ‘mvua’ ya chupa dakika ya 73 akiambaa kuelekea langoni mwa Coastal Union, jambo ambalo lilimfanya refa asimamishe mchezo na kuomba Polisi waende kusimama mbele ya jukwaa la mashabiki wa Coastal.
 
Baada ya mchezo huo, mashabiki wa Coastal walitoka jukwaani na kuwafuata marefa, lakini Polisi walifanikiwa kuwadhibiti.

Kikosi cha Coastal Union kilikuwa; Shaaban Kado, Hamad Hamisi, Othman Tamim, Mbwana Hamisi ‘Kibacha’, Juma Nyosso, Jerry Santo, Uhuru Suleiman/Yussuf Chuma dk79, Crispin Odula, Pius Kisambale/Suleiman Kassi ‘Selembe’ dk64, Yayo Lutimba na Keneth Masumbuko.

Azam FC; Mwadini Ally, Erasto Nyoni, Waziri Salum, Said Mourad, Aggrey Morris, Kipre Balou, Brian Umony/Seif Abdallah dk69, Salum Abubakar, John Bocco, Humphrey Mieno na Kipre Tchetche.
 
Na katika Uwanja wa Chamazi kulikuwa na mechi kati ya JKT RUVU na Kagera Sugar ambapo Kagera Sugar imefungwa mabao mawili kwa sinia na wenyeji wao.
 
Nayo timu iliyokuja kwa kasi katika ligi hii Mbeya City ilikuwa wageni wa JKT Oljoro ambapo wageni hao Mbeya City wameibuka na ushindi wa mabao mawili dhidi ya moja la wenyeji wao.


ZITO KABWE (MB) AWAKILISHA MUSWADA BINAFSI KUFUTA SHERIA YA MAGAZETI YA 1976

Zitto-Kabwe_839e8.jpg
Zitto Kabwe
Napenda kuujulisha umma kwamba tarehe tarehe 4 Oktoba, 2013 niliwasilisha kwa Katibu wa Bunge muswada binafsi Bungeni kufuta Sheria ya Magazeti ya mwaka 1976.

Changamoto iliyopo ni Sheria mbadala ya vyombo vya habari baada ya Sheria ya sasa kufutwa. Hata hivyo wadau wa habari kama Baraza la Habari Tanzania wameshafanyia kazi suala hili kwa muda mrefu sana na wana mawazo kuhusu sheria mbadala.
 
 Nimejulishwa kuwa muswada wa sheria mpya ya habari tayari upo. Kwa hiyo katika mchakato wa kujadili muswada binafsi wa kufuta sheria ya magazeti ya mwaka 1976 mabadiliko yanaweza kufanywa ili kutunga sheria mpya. Hatua ya kwanza ni kuifuta sheria hii kandamizi ambayo kiukweli tumechukua muda mrefu sana na baada ya madhara makubwa kufikia hatua ya muswada wa kuifuta.

Nimeamua kutumia njia za kawaida za kuwasilisha muswada na kuepuka njia ya dharura ili kujenga mazingira ya wadau wa habari kushiriki vya kutosha katika mabadiliko yanayotakiwa. 
 
 Njia ya dharura ni ya haraka lakini huziba fursa za kupata maoni ya wadau ambao kimsingi ndio wenye sheria yenyewe haswa. Hivyo nimepeleka muswada leo ili uchapwe kwenye gazeti la Serikali (GN) kwa mujibu wa kanuni za Bunge, kisha usomwe kwa mara ya kwanza, uende kwa wadau kwa mjadala na marekebisho na kisha kusomwa kwa mara ya pili na kupitishwa na Bunge.
 
Ikumbukwe kuwa juhudi za kufuta sheria hii ni juhudi za wadau wa tasnia ya habari na ni juhudi walizofanya kwa muda mrefu sana. Mimi kama Mbunge ninawasilisha tu kwa sababu taratibu zetu za kuandika sheria zinataka ama Serikali, Kamati ya Bunge au Mbunge kuwasilisha muswada.
 
 Kwa muda mrefu tumewaangusha wana habari kwa kutosukuma vya kutosha mabadiliko waliyokuwa wanayapigania. Hata hivyo, kuna msemo wa kihindi 'asubuhi huanza pale unapoamka'. Sasa tuchukue hatua za kufuta sheria hii kandamizi.
Zitto Kabwe,Mb
Kigoma Kaskazini



TWENTY PERCENT NA MAN WALTER WAMALIZA TOFAUTI ZAO

Twenty Percent akiwa ameshikana mikono na Man Walter mara baada ya kupatana.

Hatimaye bifu kali kati ya msanii aliyewahi kutwaa tuzo 5 nchini za KTMA na kuvunja rekodi TWENTY PERCENT (kushoto) na aliyewahi kuwa Producer wake na pia ni mshindi wa tuzo ya mtayarishaji bora wa muziki nchini KTMA  2012 MAN WATER (kulia) limemalizika rasimi leo kwa wawili hao kukutana nakumaliza tofauti zao.

Man Water na 20% walikutana leo katika studio za Magic fm na Channel Ten ambapo wawili hao wamekubaliana kufanya kazi tena pamoja na kusahau yaliyopita.

Akizungumzia kiundani kuhusu tofauti zao Man Water alisema tatizo lilikua ni kutoelewana au kupishana kidogo kwa kauli ambazo leo walizimaliza na hatimaye kuweka mikakati mipya ikiwemo ya kufanya kazi pamoja kwa makubaliano maalumu.

Kwa upande wake 20% amesema tofauti zao hazikuwa za msingi bali ni kupishana tu kwa kauli na sasa yuko tayari kufanya kazi pamoja na Man Water.

Inaaminika kwamba kufanya kazi pamoja kwa wawili hao kuna maana kubwa kutokana na kuwezana na kuelewana katika kazi zao mbalimbali walizowahi kufanya ikiwemo kazi ya Yanini malumbano,Tamaa mbaya,Mama Neema na nyinginezo.
Peace And Love
Chanzo: Michuzi


DEOGRATIAS MUNISH "DIDA" AUMIA MAZOEZINI LOYOLA YANGA IKIJIANDAA KUWAKABILI MTIBWA TAIFA



Daktari wa Yanga SC, akimpatia huduma ya kwanza, kipa Deo Munishi 'Dida' baada ya kuumia kwenye mazoezi ya timu hiyo Uwanja wa sekondari ya Loyola, Mabibo, Dar es Salaam. Yanga inajiandaa kucheza na Mtibwa Sugar Jumapili katika Ligi Kuu.   

Kipa namba moja wa Yanga SC, Ally Mustafa 'Barthez' akimsaidia Dida baada ya kuumia. Wengine kulia ni Rajab Zahir na Mrisho Ngassa

Mrisho Ngassa akiwatoka wenzake mazoezini

Ngassa yupo fiti kwa ajili ya mechi ya Jumapili.

Yanga SC wakijifua Mabibo



Chanzo:BIN ZUBEIRY


RAIS JAKAYA KIKWETE AZINDUA KIWANDA CHA AZAM COLA RASMI


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete akisikiliza taarifa kuhusu kiwanda cha Azam Cola, kinachomilikiwa na kampuni ya S.S. Bakhresa Group kilichopo eneo la Mwandege, Mkuranga, mkoani Pwani wakati wa hafla maalum ya uzinduzi wa kiwanda hicho

Rais Kikwete alijionea shughuli nzima za uzalishaji hadi upakiaji kiwandani hapo

Rais Kikwete akitalii kiwandani hapo, akiwa ameambatana na mkewe Mama Salma 

Rais Kikwete akiwa na Mwenyekiti wa Makampuni ya S.S. Bakhresa, Alhaj Sheikh Said Salim Awadh Bakhresa na mkewe Mama Salma KIkwete. Kulia kwake ni Dk Abdallah Kigoda  

Rais Kikwete akihutubia kiwandani hapo


MAMA ASIYEFAHAMIKA APIGWA RISASI KWA KUTAKA KUINGIA IKULU YA WHITE HOUSE

Risasi zimesikika katika mji wa Washington DC baada ya Mwanamke mmoja aliekuwa akiendesha gari kwa kasi kutaka kuingia katika Ikulu ya Marekani ''WHITE HOUSE" pasipo kufuata sheria ya kusimama katika vizuizi vilivyopo katika eneo hilo la ikulu ili akanguliwe Baada ya kuona Mwanamama huyo hataki kutii amri ya kusimama ndipo wanausalama wa Ikulu walipoamua kumfyatulia risasi na  ndipo mauti yalipomkuta ndani ya Gari baada ya kuikagua walikuta kunamtoto mdogo wa kike, Polisi walidhani ni tukio la ugaidi 



MRITHI WA SHEIKH ABOUD ROGO NA WENZAKE WATATU WAUAWA MOMBASA




Watu ambao hawajabainishwa wamempiga risasi na kumuua kiongozi wa Kiislamu aliyeuawa Sheikh Aboud Rogo, Sheikh Ibrahim Rogo pamoja na wenzake watatu usiku wa kuamkia Ijumaa ya tarehe 04-10-2013.

Sheikh Ibrahim Rogo na wenzake wanne walikuwa wakielekea nyumbani kutoka Masjid Musa kwa ajili ya ibada ndipo gari yao ilipomiminiwa risasi zilizowaua wanne kati ya watu waliokuwa katika gari hiyo kwenye umbali wa nusu kilometa kutoka kituo cha polisi cha Bamburi.

Wengine waliokuwa katika hiyo gari ni bwana Gadaffi Muhammad anayesemekana kuwa fundi seremala, bwana Issa Abdalla shemeji wa Gadaffi na ambaye ndiye aliyekuwa akiendesha hiyo gari, Omar Abu Rumeisa na Salim Aboud ambaye alipona kimaajabu katika shambulizi hilo baada ya kujifanya kuwa amekufa.

Salim Aboud anasema kuwa walikuwa wakielekea nyumbani katika gari aina ya Toyota Fun Cargo ndipo watu waliokuwa wakitembea walianza kuishambulia gari yao kwa risasi na kuacha njia.

“Tumewamaliza,” Bwana Salim Aboud aliwasikia wakisema baada ya yeye kujifanya kuwa amekufa. Wauaji wanasemakana kutumia gari aina ya Mark X kutoka katika eneo hilo.

Viongozi kadhaa wa Kiislamu, akiwemo Sheikh Abubakar Sheriff anayejulikana kwa jina la Makaburi ambaye alifika katika eneo hilo baada ya tukio, alikinyooshea kidole Kikosi Maalumu cha Polisi cha Kupambana na Ugaidi kuwa ndicho kilichohusika na mauaji hayo.


“Kikosi cha ATPU kilikuwa hapa, kwa nini wamekimbia? Tumefanya nini na kwa nini wanatuua? Hatujamuua yeyote lakini polisi wanawaua Waislamu wasiokuwa na hatia,” alisema Sheikh Makaburi.


“Vitendo hivi vinaongozwa na Wamarekani na Waisraeli, Sheikh Ibrahim hakuwa katika Jengo la Westgate wakati wa shambuli kwenye jengo hilo. Serikali za Kimagharibi hawataki Waislamu wazungumzie Jihad. Jihad ni sehemu ya Uislamu, tuuweni sote,” alisema.


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU