Facebook Comments Box

Wednesday, July 3, 2013

KIBONZO: TASWIRA ZA DAR ES SALAAM INAPOKUWA NA UGENI NA UGENI UKIONDOKA

Picture
Picture
 


MUHIMBILI KUTENGENEZA CHUO KINGINE CHA UDAKITARI

Picha onayoonesha mchoro wa jengo

Na: Belinda Kweka- MAELEZO
CHUO Kikuu cha Sayansi na Tiba Muhimbili(MUHAS)  kipo katika mpango wa kujenga chuo kipya kwa ajili ya ufanyaji mazoezi kwa wanafunzi.Ujenzi huo  unatarajiwa kuanza Agosti mwaka huu katika eneo la Mloganzila Kibamba  ambapo , ukimalizika  utachukua wanafunzi 15,000  watakaosoma  taaluma  mbalimbali za afya. Akizungumza  na
waandishi wa habari  leo kwenye   Maonesho ya 37 ya Biashara ya Kimataifa  yanayoendelea katika viwanja  vya  Mwalimu  J. K Nyerere  jijini  Dares Salaam (sabasaba) ,Afisa Mipango Mkuu wa chuo hicho Ulimbaga Kijobile alisema  uamuzi  huo umetokana na ongezeko la wanafunzi ni wengi.
Alisema  eneo hilo   lita wezesha wanafunzi hao kupata sehemu  za kusomea kwa ufanisi  kama vile  ya maabara za kisasa, madarasa, na sehemu za ufanyaji mazoezi.

“Tumeamua kuanzisha mradi kwa kujenga chuo kipya kwa sababu MUHAS ina sehemu ndogo na hatuwezi kuipanua kwa ajili ya kuongeza ukubwa wa chuo ili kuweza kutosha kwa wanafunzi” alisema Kajobile.
Aidha alisema wanafunzi hao , walikuwa wakipata tabu katika kufanya mazoezi ,hivyo hulazimika  kwenda  hospitali za Mwananyamala na Amana.“Muda mwingine tunatumia hospitali nyingine ili kupata sehemu ya kutosha lakini hospitali hii itakayojengwa itasaidia kuchukua wanafunzi wote ili kuweza kufanya mazoezi yao bila usumbufu” alisisitiza Ulimbaga.
Alisema  ujenzi wa  chuo hicho, kinakadiriwa kujengwa ndani ya mwaka mmoja,ambapo  wanafunzi wa muhula wa kwanza wa mwaka 2015 wanatarajiwa kuanza.
Aliongeza  kuwa kitatoa huduma za kiafya kama hospitali nyingine hivyo wananchi wa eneo hilo wanashauriwa kufika mara baada ya ufunguzi wa chuo hicho ili kupata matibabu mbalimbali.


KIBONZO: ANGALIA KITUKO HIKI CHA KISARAWE

.
.
Huku tunakoishi uswahilini wengi wetu huwa hata majumba ya Cinema wanakolipia elfu kumi kutazama movie huwa hatuyafahamu au hatujawahi kwenda kabisa…. hivyo kuna kautaratibu ketu ka kuchangisha hizi mia mia na mia mbili kwa ajili ya kuingia ‘vibanda umiza’ ambavyo huwa vinatutoza hizo senti kwa ajili ya kutazama movie zilizotafsiriwa pamoja na mpira…. yani kutazama hivyo vitu viwili sehemu kama hizo ni kawaida kabisa.
Sasa bwana kwenye eneo la Kisarawe ambalo liko kwenye mkoa wa Pwani, kuna mjanja mmoja alitumia akili ya ziada kujua kwamba sio kila mmoja anaweza kwenda town kusubiria kuona msafara wa Rais Obama, hivyo akaamua kuchangisha hizo mia mia kwa kila anaetaka kutazama ujio wa Rais Barack Obama Tanzania ambao ulikua unaonyeshwa moja kwa moja na vituo mbalimbali vya TV ikiwemo ya Taifa TBC1 na Clouds TV.
Uhakika wa kuzikusanya hizo mia mia ulikuwepo sana kwa sababu kwanza Kisarawe sio kila Mwananchi anamiliki TV au nyumba yake ina umeme hivyo ni lazima tu kama angekua na shilingi 100 angejikusanya kwenye kibanda umiza kucheki hilo movie la Obama kwenye ardhi ya Tanzania.

 SOURSE:MILLARD AYO 

 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU