Facebook Comments Box

Saturday, November 23, 2013

ZITTO KABWE KUONGEA NA WAANDISHI WA HABARI KESHO

Bila shaka hili ni jambo ambalo mimi na wewe tulilitarajia. Baada ya maamuzi ya Kamati Kuu ya CHADEMA ya kuwavua madaraka ya kiuongozi waliyokuwa nayo Mh.Zitto Kabwe na Dr.Kitila Mkumbo hapo jana, wawili hao wapo tayari kukutana na waandishi wa habari na kuueleza umma maoni na msimamo wao.
Katika ujumbe mfupi ambao Mh.Zitto Kabwe ameuweka kwenye ukurasa wake wa Facebook na taarifa hiyo hiyo kusambazwa kwa vyombo mbalimbali vya habari, mkutano na waandishi wa habari unatarajiwa kufanyika hapo kesho saa tano [asubuhi] katika Hoteli Ya Serena jijini Dar-es-salaam.


HII NDIO TWEET YA KWANZA YA ZITTO TOKA AVULIWE MADARAKA



KIBONZO: KIPANYA NA SAKATA LA CHADEMA



PROF BAREGU NAE AJIUZURU CHADEMA



 Habari zilizotufikia katika chumba chetu cha habari zinaeleza kuwa Mjumbe wa tume ya mabadiliko ya Katiba kutoka chama cha demokrasia na maendeleo (chadema) ametoa kauli ya kujiondoa na kujiuzulu nafasi zake ndani ya Chama hicho kupelekea maamuzi yaliyofanywa na kikao cha kamati kuu ya chama hicho


Huyu ni Mjumbe wa pili wa kamati kuu ya Chadema kuamua kujiuzulu wadhifa wake katika kipindi kisichozidi masaa 12.


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU