Facebook Comments Box

Friday, July 12, 2013

OPRAH WINFREY KUJA TANZANIA KESHO

. 
Inaelekea President Obama kaacha upepo mzuri Tanzania manake taarifa zilizotufikia muda mfupi uliopita baada tu ya bondia Evander kuthibitishwa na yeye kuja Tanzania, mtangazaji staa wa dunia Oprah Winfrey nae anatarajiwa kufika Tanzania.
Staa huyu ambae amewahi kufanya interview na mastaa wengine kama marapper  Jay Z na 50 Cent, unaambiwa usitegemee kumuona Dar es salaam au sehemu nyingine maarufu za town, anatua Serengeti kesho July 13 2013 kwa ajili ya mapumziko tu na kuondokea hukohuko.


TANGAZO LA AJIRA KUTOKA UTUMISHI


Sekretarieti ya Ajira kwa niaba ya Tanzania Dairy Board, Tanzania Institute of Accountancy, College of Business Education, National Institute of Transport, Tanzania Broadcasting Cooporation, Tanzania Institute of Education, Tanzania Library Services Board, Local Government training Institute, Institute of Finance Management, National College of Tourism Agency, Law school of Tanzania, Tanzania Metrological Agency, Moshi Unoversity college of cooperative and business Studies, Dar es Salaam Marine Institute, Kibaha Education Centre, Institute of Rural Develepment Planning, Tanzania Public Service College, Tanzania Wildlife Research institute, Institute of Accountancy Arusha na National Examination Concil of Tanzania inawatangazia furasa mbalimbali za Ajira Serikalini, Kwa maelezo zaidi fungua kwenye TOVUTI ya Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma ambayo ni www.ajira.go.tz. 


TANGAZO LA KAZI-JULY 2013

PICHA: WABUNGE WAKIPIGANA BUNGENI


Hawa ni wabunge wa Ukraine wakipeana makonde bungeni

POLISI WAFANYA UPELELEZI KUMPATA ALIE RUHUSU KILO 150 ZA MADAWA YA KULEVYA KUPITA AIR PORT

Akizungumza na gazeti la NIPASHE lililochapisha habari ya dawa za kulevya kilo 150 zilizokamatwa kwa wasichana wa Kitanzania nchini Afrika Kusini, Kamanda wa Polisi Kikosi cha Viwanja wa Ndege Nchini, Deusdedit Kato, amesema tukio hilo ni baya, limeifedhehesha Tanzania na kuiitia dosari nchi ambayo ilisifika kuwa na watu waminifu.

Hivyo amesema kuna haja ya kusaidiana ili kurudisha imani kwa nchi.

“Ni lazima tupambane kurudisha heshima kwa sababu watanzania watakuwa hawaaminiki tena katika nchi nyingine, ni  mapema mno kuinyoshea kidole taasisi yeyote kwani uchunguzi bado unaendelea ili kubaini aliyeruhusu kupitisha mzigo huo, ”alisema alipoulizwa na gazeti hili kama wasichana hao walikaguliwa.

Alisema ni lazima kwa pamoja kufanya uchunguzi na kubaini ni taasisi gani ilipwaya katika kutekeleza majukumu yake ipasavyo na kuruhusu dawa hizo kupita.

Alisema mpaka sasa uchunguzi umefikia katika hatua nzuri na watatoa taarifa wakati wowote.

Alizitaja Taasisi hizo kuwa ni Polisi,Usalama wa Taifa,Uhamiaji na Mamlaka ya Viwanja vya ndege (TAA).

“Tukio hili ni baya limeiitia dosari nchi ambayo ilisifika kuwa na watu waminifu lakini sasa limetuchafua sana, tunahitaji kusaidiana ili kurudisha imani kwa nchi yetu iliyokuwapi hapo awaliaaaa,” alisema na kuongeza: "Wasichana hao inadaiwa kuwa walisafirisha dawa hizo kwa ndege ya Shirika la Ndege la South African Airways linalomilikiwa na serikali ya Afrika Kusini."

Hadi sasa wasichana hao bado wanashikiliwa na   Jeshi la Polisi la Afrika Kusini kwa ajili ya upelelezi.



 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU