Facebook Comments Box

Sunday, October 12, 2014

MECHI YA MASHEIKH WA BAKWATA NA VIONGOZI WA KIKRISTO YAMALIZIKA

Mh Mizengo Pinda akiongea
Mechi ya kudumisha amani na mshikamano baina ya Viongozi wa dini ya kiislamu na kikristo, imekwisha kwa timu ya Amani kuifunga timu ya Mshikamano kwa goli moja kwa bila.

Mechi hiyo iliyochezwa kwa dakika 30 kwa kila kipindi, goli la timu ya Amani lilifungwa katika dakika za mwisho za mchezo huo na timu zilikuwa mchanganyiko bila ya kuweka watu wa dini moja kuwa timu moja.

Mgeni rasmi katika pambano hilo alikuwa Mheshimiwa Waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mizengo Pinda.

Refarii wa mchezo huo alikuwa Kamanda wa polisi kanda maalumu Dar es Salaam, zawadi kwa Mshindi wa kwanza na wa pili zilikabidhiwa na Waziri mkuu Mizengo Pinda Waziri Mkuu Mizengo Pinda akizungumza Kepteni wa timu ya Amani Sheikh Alhad Mussa aliyefahamika kwa
jina la muda katika mchezo huo 'Jaja', ndiye aliyekabidhiwa kombe na Waziri Mkuu.

Pambano hilo litafanyika kila mwaka na kufahamika kama 'Amani Cup'.


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU