Facebook Comments Box

Thursday, May 1, 2014

MBUYU TWITE NAE KUJIUNGA NA AZAM?

Uongozi wa klabu ya Young Africans unapenda kuwajulisha
wanachama wake, wapenzi wa soka na wadau kwa ujumla kuwa
taarifa za kuhama kwa wachezai wake Didier Kavumbagu na Frank
Domayo kwenda kujiunga na Azam FC zisiwakatishe tamaa, ni
mapenzi ya wachezaj wenyewe kwani walishakubaliana na uongozi
kila kitu juu ya kuendelea kuitumikia Yanga kabla ya siku mbili hizi
kuonekana wakiwa wamejiunga na wana ramba ramba.
Yanga tayari ina wachezaji watatu wenye mikataba inayoendelea na
kama kanuni za VPL kwa wachezai wa kimataifa kuwa watatu
zitatumika wachezaji Haruna Niyonzima, Hamisi Kizza na Emmanuel
Okwi ndio watakaoendelea, hivyo uongozi uliomba mwongozo kwa
TFF juu ya taratibu zitakazotumika kwa msimu ujao kabla ya
kuwasainisha Kavumbagu na Twite.
Awali uongozi wa Yanga ulikuwa kwenye mazungumzo na wachezaji
hao tangu mwanzoni mwa msimu wa 2013/2014 juu ya kuongezewa
muda wa mikataba yao ili waweze kuendelea kuitumika Yanga kwa
ajili msimu mpya ujao 2014/2015.
Didier Kavumbagu na Mbuyu Twite ambao mikataba yao ilikuwa
mwishoni waliongea na uongozi tangu mapema mwaka jana mwezi
wa Septemba juu ya kuweka sahihi zao na kuendelea kuitumikia
Yanga na kukubaliana mambo yote ya msingi kikubwa kilichokuwa
kinasubiriwa ni maamuzi ya TFF juu ya usajili wa wachezaji wa
kigeni msimu mpya wa 2014/2015 kwani Azimio la Bagamoyo
linapaswa kuanza kutekelezwa msimu huu
Uongozi wa Yanga uliandikia TFF barua mapema kuomba kupewa
mwongozo wa kanuni zitakazotumika kwenye usajli kwa wachezaji
wa kimataifa kwa msimu mpya kufuatia Azimio la Bagamoyo
kuelekeza msimu huu kila timu inapasa kuwa na wachezaji watatu
wa kigeni, mpaka sasa uongozi wa Yanga haujapata majibu juu ya
utaratibu utakaotumika kwenye msimu wa Ligi Kuu ijayo.
Hivyo makubaliano ya wachezaji Didier Kavumbagu, Mbuyu Twite
na uongozi wa Yanga SC yalikua yakisubira majibu ya TFF juu ya
kanuni zipi zitakazotumika kwenye usajili msimu wa 2014/2015 kwa
wachezaji wa kigeni na katika hali ya kushangaza Kavumbagu
akaonekana tayari ameshasaini kuichezea timu ya Azam FC.
Kuhusu Frank Domayo aliyeripotiwa jana kujiunga na Azam FC pia
alikuwa katika makubaliano ya kuongeza mkataa tangu mwezi Julai
2013, alikubaliana na uongozi juu ya mambo yote ya msingi na
kilichobakia ilikuwa ni kuweka sahihi kwenye mkataba mpya, lakini
Domayo alisema hawezi kusaini mpaka siku atakapokuja mjomba
wake ambaye ndie wakala wake na ahadi hiyo iliendelea kwa muda
wa mwaka mzima kabla ya jana kusikia ameshasaini timu nyngine.
Habari hizi zimewashitua wapenzi, wanachama na washabiki wa
Young Africans lakini ukweli ni kuwa wachezaji wenyewe walisindwa
kuwa wakweli kwa viongozi na mwisho wa siku walikua na mipango
yao ya kuondoka, hivyo uongozi ulijtahid kadri ya uwezo wake lakini
wachezaji wanaonekana hawakua tayari kuendelea kuichezea Yanga
SC.
Taarifa kamili kuhusu mipango ya timu kwa msimu ujao pamoja na
ripoti ya kocha mkuu Hans pamoja na benchi lake la Ufundi
zitatolewa hivi karibuni baada ya benchi la ufundi na uongozi kukaa
kwa pamoja na kuafikiana mipango ya msimu ujao.
Aidha uongozi wa Yanga SC unawaomba wanachama wake,
wapenzi na washabiki wasiwe na wasi wasi juu ya kuondoka kwa
wachezaji hao kwani Yanga bado ina nafasi wachezaji wengi wenye
vipaji na itaendelea kuboresha kikosi chake kwa kuzingatia
maelekezo ya kocha mkuu Hans katika usajli wa msimu ujao.
Kwa maelezo hayo hapo juu inaonesha Mbuyu twite hana nafasi tena maana azimio la Bagamoyo limetiliwa mkazo sana na TFF.
Na kuna habari kocha wa Azam ameuambia uongozi uhakikishe imemsajili 


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU