Facebook Comments Box

Saturday, March 16, 2013

KINANA NA UJUMBE WAKE WAKIWA MJI WA CHENGDU,CHINA


KATIBU Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana (kushoto) akimpa zawadi ya kinyago cha 'Ujamaa', Katibu Mkuu wa Chama Cha Kikomunisti cha China (CPC), Kamati Kuu jimbo la Sichuan, Zhang Ning, baada ya mazungumzo yao, Machi 15, 2013, katika hoteli ya Jinjiang, mjini Chendu, China. Kinana yupo nchini China  na ujumbe wa viongozi 14 wa CCM kwa ajili ya ziara ya mafunzo. (Picha na Bashir Nkoromo).

KATIBU Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana (kushoto) akipewa zawadi ya picha na Katibu Mkuu wa Chama Cha Kikomunisti cha China (CPC), Kamati Kuu jimbo la Sichuan, Zhang Ning, baada ya mazungumzo yao, Machi 15, 2013, katika hoteli ya Jinjiang, mjini Chendu, China. (Picha na Bashir Nkoromo

Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana (aliyefunfa mikono kifuani), na baadhi ya wajumbe katika msafara wake, wakimtazama kwa makini kijana, Hu Qingzhong, aliyekuwa akichora katuni kwenye kompyuta kwa ajili ya kuwekwa kwenye simu za mkononi. Kinana na ujumbe wake walipotembelea kituo cha Wajasriamali wasomi cha Chengdu-High-Tech zone, jijini Chengdu, China, Machi 15, 2013.  Kinana yupo nchini China  na ujumbe huo kwa ajili ya ziara ya mafunzo. (Picha na Bashir Nkoromo).
Katibu wa Jumuia ya Wanawake Tanzania (UWT) Amina Makilagi (kulia) akicheza muziki na mmoja wa wasanii wa kundi linalotumbuiza kwa kupewa fedha yoyote na anayevutiwa, kwenye eneo la Mji wa Kihitoria ya zaidi ya miaka 100 wa Jin Sha, jijini Chengdu, China.


UONGOZI:MKUTANO MKUU SIMBA SC KESHO NI BATILI

Mwenyekiti wa Simba Aden Rage


Na Princess Asia
KLABU ya SImba SC imesema kwamba Mkutano Mkuu wa Wanachama wa Simba uliopangwa kufanyika Kesho katika ukumbi wa Star Light Hotel mjini Dar es Salaam kujadili mustakabali wa klabu ni batili.
Taarifa ya Ofisa Habari wa Simba SC, Ezekiel Kamwaga imesema kwamba ikumbukwe kwamba Mkutano Mkuu wa Wanachama ndiyo chombo cha juu kabisa cha maamuzi kwa klabu yetu. Katiba ya Simba SC imeupa Mkutano Mkuu hadhi ya juu mno na ndiyo maana imeweka utaratibu wa kufanyika kwake.
Taarifa hiyo imesema miongoni mwa utaratibu ni kwamba ni lazima uitishwe na Mwenyekiti aliye madarakani wa klabu. Kwa kushirikiana na Kamati ya Utendaji, ndiye atakayepanga ajenda, mahali na wakati wa kufanyika kwa mkutano wenyewe. 
Imesema katika miaka ya nyuma, zilikuwepo nyakati ambapo klabu ilikaa hadi miaka mitatu pasipo kuitishwa kwa Mkutano Mkuu wowote wa wanachama. 
Imesistiza hakuna mwanachama au kikundi chochote kilichojitokeza kudai mkutano wa dharura wakati huo ingawa ilikuwa ikifahamika kwamba huo ulikuwa ni ukiukwaji mkubwa wa katiba ya klabu.
Imesema tangu uongozi huu uingie madarakani takribani miaka mitatu iliyopita, mikutano mikuu miwili ya wanachama imefanyika kwa mujibu wa KATIBA na kwamba Mungu akijaalia, uongozi huu utafanya mkutano mwingine wa kawaida wa wanachama baadaye mwaka huu.
Hata hivyo, taarifa hiyo imesema kwa kuzingatia hali halisi ya klabu, Mwenyekiti wa Simba, Alhaji Ismail Aden Rage (Mb), mwezi uliopita alitangaza dhamira yake ya kuitisha Mkutano Mkuu wa Dharura wakati wowote kuanzia sasa.
Taarifa imesema Rage alisema mkutano huo ungekuwa na ajenda moja tu; Kujadili Mwenendo wa Klabu kwenye mashindano inayoshiriki msimu huu.
Imeendelea kusema kwamba kwa bahati mbaya, Mwenyekiti alishikwa na maradhi na akapelekwa India kwa matibabu na yuko huko hadi Mola atakapomjalia afya njema na kurejea. Kuna uwezekano mkubwa, Inshallah, akarejea mwishoni mwa wiki ijayo.
“Hii maana yake ni kwamba uongozi umeridhia kufanyika kwa Mkutano wa wanachama. Kimsingi, kama uongozi umeridhia, hakuna mwanachama mwingine anayeweza kuitisha mkutano mkuu mwingine,”.
“Mwenyekiti ameruhusiwa kuitisha Mkutano Mkuu kwa sababu alichaguliwa na wanachama na hivyo ana nguvu ya kisheria (locus standi) kufanya hivyo. Hawa wengine wanaoitisha mkutano wana nguvu gani ya kisheria kufanya hivyo? Walichaguliwa na nani kuwakilisha wanachama? Lini na wapi?”
“Uongozi pia unaweza kuitisha mkutano kwa vile wenyewe ndiyo wenye leja ya wanachama. Klabu sasa ina database yake ya kompyuta inayotambua wanachama walio hai na wasio hai,”. 
“Kwa kutumia database hiyo, uongozi huu unatambua wanachama walio hai na wasio hai. Hakuna mtu mwingine yeyote, aliye nje ya uongozi huu anayefahamu wanachama walio hai na wasio hai. Hao wanachama wanaoitana kufanya mkutano, wamehakikiwa na nani kubaini uhalali wao huo?”
“Uongozi wa Simba SC unaona kwamba wale wanaolazimisha kufanyika kwa Mkutano Mkuu wana ajenda binafsi na si za maslahi ya klabu. Kama kweli wangekuwa na nia njema na klabu wangesubiri mkutano ambao utaitishwa punde,”.
“Kwani, kuna uharaka gani wa kufanyika mkutano kesho? Kwanini hawataki Mwenyekiti, ambaye wanachama walimpa mamlaka ya kuongoza klabu kwa kipindi cha miaka minne, awepo kwenye mkutano huo?”
“Kwanini hawataki kuungana na wana Simba wengine kumwombea Mwenyekiti kwa Mungu ili amwepushe na ugonjwa na kumrejesha salama hapa nyumbani? Kwanini mikutano hii iitishwe katika kipindi ambacho uongozi umefungua mikono yake na kukaribisha kila mmoja mwenye mapenzi mema na klabu kuja kuchangia?”
“Kwenye macho ya Katiba ya Simba na sheria za Tanzania, huu mkutano wa kesho ni batili na una lengo la kuleta vurugu na mifarakano kwenye jamii na michezo kwa ujumla wake. Michezo ni amani na furaha na michezo si vurugu,”.
“Tayari uongozi wa Simba umetoa taarifa kwa Jeshi la Polisi na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kuhusiana na ubatili wa mkutano huo. Tunapenda kuwaomba wanachama wetu wasiopenda fujo na vurugu kwenye michezo kukaa mbali na mkutano huo kwa vile vyombo vya dola vitaufuatilia,”.
“Uongozi hautajiingiza katika kutoa dhamana au msaada wa namna yoyote kwa yeyote ambaye atachukuliwa hatua na vyombo vya dola kutokana na kujihusisha na mkutano huo,”.
“Pia, Simba SC inatoa wito kwa vyombo vya habari kuwa makini wakati vinaporipoti matukio ya vurugu kwenye michezo. Kabla mtu hajahojiwa kujieleza kama mwanachama wa Simba, ni vema kwanza akaonyesha kadi yake ya uanachama na risiti za malipo yake,”.
“Wakati mwingine, waandishi huwa tunawapa nafasi kwenye vyombo vyetu vya habari watu ambao hawana mchango wowote kwenye kukuza michezo bali kuleta vurugu. Kwanini, tungejiuliza, ni watu wale wale ambao kila mwaka huonekana wakati wa vurugu na wakati wa amani huwa hawaonekani?”
“Kwanini, vyombo vyetu vinatoa nafasi kwa watu ambao lengo lao ni kuhakikisha vilabu vyetu vinazidi kubaki nyuma, vinakuwa na vurugu kila wakati na michezo inaonekana kama ni sehemu ya wahuni na watu wasio na utaratibu?”
“Mpira bado haujaleta tija kubwa kwenye uchumi wa Tanzania na kunufaisha wachezaji kwa sababu baadhi ya watu makini na makampuni makubwa yanaogopa kujiingiza kwenye michezo kwa sababu ya tabia kama hizi,”.
“Ni vema vyombo vya habari vikafanya jitihada kubwa katika kuwatambua waleta vurugu, si katika klabu ya Simba pekee, bali kwenye sekta ya michezo kwa ujumla, ili visiwape nafasi ya kuharibu na badala yake vitoe nafasi kwa wale wenye lengo la kujenga,”.
“Tunasisitiza, uongozi huu utaitisha Mkutano Mkuu wa Wanachama Wote mara baada ya kurejea kwa Mwenyekiti,”.
 
SOURSE: BIN ZUBEIRY


PAMOJA NA BARABARA KUKARABATIWA UPYA MAJI YAENDELEA KUTUAMA BUGURUNI SOKONI (BARABARA YA UHURU)

 Hii ni hali ilivyo sasa barabara ya uhuru baada ya barabara kukarabatiwa upya na lami iliyokuwepo kuondolewa na kuwekwa mpya. Kabla ya hapo maji yalikuwa yakituama na kusababisha eneo hili la barabara kuwa na mabonde na madimbwi mengi wananchi walipoona inakarabatiwa wakadhani kampuni iliyopewa kazi hiyo itazingatia hilo na maji hayatatuama tena. Cha kushangaza kwa mvua hizi ndogo maji yametuama tena kwa maana rahisi kampuni imechakachua kazi hii. Angalia picha hapo chini

Ukifika Rozana tu unaliona hilo dimbwi
Hili ni eneo la buguruni sokoni karibu na kituo cha polisi cha buguruni. Angalia maji hayo yalivyo tuama. Malaria haikubaliki? Kipindupindu je?
Kampuni imeshamaliza kazi hapo na lami mpya imewekwa


kwa mbaali unaliona dimbwi alilotengeneza bwana injinia

Ukiangalia vizuri utaona gari linavyowamwagia maji wapita njia pamoja na nyanya na matunda yanayowekwa hapo chini. Tunaolala hoi tunakazi sana

Matope yaliyocchanganyikana na uchafu wa sokoni buguruni.



HIVI NDIVYO BASI LILIVYOUNGUA LOTE KIBAHA LEO


Basi la ndenjela likiwa linatoka dar kuelekea mbeya limeteketea kwa moto kibaha kongowe asubuhi ya leo. Abiria wote wamenusurika janga hilo.MIZIGO IMTEKETEA KATIKA JANGA HILO


KIBONZO CHA LEO: AJALI ZA BODABODA




SUNDERLAND YA ENGLAND YAIPIGA CHINI SIMBA SPORTS CLUB


SUNDERLAND ya England imevunja uhusiano wake na Simba baada ya kutoridhishwa na baadhi ya mambo

Klabu hiyo ya England sasa inafikiria kufanya kazi na Yanga au Azam ili kutekeleza miradi mbalimbali ikiwemo ya kukuza fursa ya uwekezaji na kutoa msaada wa kiufundi kwa klabu moja kati ya hizo.

Habari za ndani zinasema kwamba Sunderland ilianza kuwasiliana na uongozi wa juu wa Simba lakini kukawa hakuna mrejesho wowote kutoka kwa viongozi wa klabu hiyo ya barabara ya Msimbazi.

Habari zinasema Sunderland walituma barua pepe tatu (email) kwa uongozi wa juu wa Simba lakini baada ya kuona hakuna majibu wakaandika ya mwisho kuwajulisha kwamba wamesitisha urafiki kwani hawawezi kufanya mambo ya kimagumashi.

Endapo dili ya Simba ingefanikiwa wangekuwa wakipata vifaa mbalimbali, pamoja na misaada ya kiufundi na fursa kadhaa kila mwaka.

Awali Simba ambayo iliasisiwa mwaka 1936 ilikuwa ikitumia jina la Sunderland kabla kubadili na kuanza kutumia hili la sasa tangu 1971.

Simba ilipanga kuanzia kutumia jezi za Sunderland msimu ujao ambazo zina maandishi ya 'Invest in Africa' ambayo huvaliwa pia na Sunderland ya England, lakini kutokana na dili hilo kufa, Simba wataendelea kuvaa jezi zao za Kiliamanjaro

Simba imekuwa katika hali ambayo watafsiri wa mambo wanasema ni mgogoro wa chini chini kwa kuwa baadhi ya viongozi wake wa juu mameanza kujiuzuru mmoja mmoja huku mwenyekiti wa kilabu hiyo Mh Aden Rage aking'ang'ania kubaki madarakani.


AFYA YA LWAKATARE YAZIDI KUZOROTA

Mkuu wa Usalama na Ulinzi wa Chadema, Wilfred Lwakatare 
 

Hali ya afya ya Mkuu wa Usalama na Ulinzi wa Chadema, Wilfred Lwakatare anayeshikiliwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za kuwahamasisha watu kufanya vitendo vya uvunjifu wa amani kupitia mitandao ya jamii, imezorota.
Mwandishi wa gazeti la Mwananchi amemshududia jana akizungumza na wakili wake Nyaronyo Kicheere, huku akilalamikia hali yake kuwa si njema kutokana na ugonjwa wa kisukari alionao.
Alikuwa akitembea kwa kujivuta, na alidai kuwa ameshindwa kula chakula inavyotakiwa.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, wakili Kicheere alisema amehangaika sana katika kuhakikisha kuwa mteja wake anapata dhamana lakini imeshindikana, hali ambayo inamtia hofu kutokana na hali aliyomwona nayo.
“Mteja wangu ni mgonjwa wa kisukari, kwa kawaida hutakiwa kula chakula na kunywa maji mengi, lakini nimehangaika sana, leo (jana) nilikuwa na matumaini kwamba atapelekwa mahakamani ambapo nilijipanga kwa kuandaa watu makini wenye hati za nyumba nikiwa na imani kwamba angepata dhamana, lakini wamemrudisha mahabusu,” alisema Kicheere.
Kicheere muda mwingi alionekana kuhaha kuwasiliana na viongozi wa Chadema kwa simu yake ya mkononi, pamoja na kuwasiliana na baadhi ya wanasheria akiwamo Tundu Lissu na Peter Kibatala ambao walijipanga katika kuhakikisha kuwa wanapata wadhamini watakaoweza kumdhamini Lwakatare.
Wakili huyo alisema kuwa kinachotendeka kwa mteja wake ni kinyume cha sheria kwa kuwa ni tuhuma ndizo zimemfanya akamatwe.
Alisema mteja wake ana haki ya kupewa dhamana hasa kwa kuzingatia kuwa saa zaidi ya 24 zimepita na hali yake si njema, na kwamba kuendelea kuwa mahabusu ni kuhatarisha usalama wa afya yake.
Maofisa wa juu kutoka ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelelezi wa Makosa ya Jinai, waliwasili Kituo Kikuu cha Polisi jijini Dar es Salaam ambapo walikutana na wakili Kicheere na mtuhumiwa huyo na kufanya mazungumzo.
Taarifa za kuaminika zilizopatikana awali zilieleza kuwa juzi saa 11 jioni maofisa kadhaa wa polisi, walimchukua mtuhumiwa huyo na kwenda naye nyumbani kwake wakiwa na lengo la kufanya upekuzi kwa mara ya pili lakini juhudi zao ziligonga mwamba baada ya kutokuwa na kibali cha upekuzi.
“Wakili wake anawabana maofisa wa polisi akitaka wafanye kazi zao kwa mujibu wa sheria hivyo juzi hawakuweza kuingia ndani, pia walizuiwa na wakili huyo huyo kumhoji kwa kumrekodi kwa video, ambapo kulitokea hali ya majibishano ya kisheria, lakini hatimaye akahojiwa bila kurekodiwa,” kilieleza chanzo cha habari.
Lwakatare alikamatwa Jumatano ya wiki hii katika makao makuu ya chama hicho na tangu siku hiyo anaendelea kushikiliwa na polisi kwa mahojiano.

SOURSE: MWANANCHI


DIAMOND KUPATA MTOTO NJE YA NDOA


Kupitia segment ya U Heard ya XXL Clouds FM na Soudy Brown, mwimbaji Diamond Platnums ambae aliongoza kwa kuwa msanii wa bongo alieandikwa sana kwenye internet mwaka 2012 amethibitisha kumnunulia mkoko mama watoto wake mtarajiwa.

Soudy Brown alimuuliza kuhusu fununu za kutumia Milioni 15 kununua gari la mke wake mtarajiwa mtangazaji Penny ambae kwa sasa ni mjamzito.

Diamond amekiri kwamba ni kweli kamnunulia Penny gari kwa sababu anaelekea kuwa mama watoto ambapo namkariri akisema “nilimuuliza gari gani
anapenda, nimemuagizia iko njiani inakuja kwa hiyo sasa hivi anatumia la muda wakati akisubiria gari lake”

Alipoulizwa kuhusu kumuoa na kama mtoto atazaliwa nje ya ndoa, Diamond amejibu “siwezi kusema lini ila Mwenyenzi Mungu ndio anajua inaweza ikawa harusi ila kuna time inafika inabidi utulie, siwezi kusema chochote kwa sababu inawezekana mtoto akazaliwa ndani ya ndoa pia “




WAVUNJA REKODI KWA UFUPI DUNIANI HEBU CHEKI UJIONEE

.
.
.
.
.
.
.
.
Harusi ilifana baada ya Matt Mccarthy mwenye urefu wa futi nne kumtamkia mpenzi wake Amazing Chapman mwenye urefu wa futi tatu nia ya kumuoa ambapo rafiki wa wawili hao Todd Ray ambae ni mtangazaji wa show ya Tv ya Venice aliwafanyia bonge la party kwenye harusi yao. Ray amesema hawa wapendanao wanafuraha na maisha yao lakini swala la kupata mtoto ni kikwazo na linazungumziwa sana, Matt anataka watoto lakini Ali hana uhakika.

.
.


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU