Facebook Comments Box

Wednesday, August 20, 2014

TETESI: PICHA YA HELKOPTA YA MCHUNGAJI NGWAJIMA

Tetesi zilizopo mtaani zinasema hii ni helkopta ya mchungaji Ngwajima.





E-FM YAENDELEA KUIBOMOA ITV/R.ONE BAADA YA KITENGE, YAMCHUKUWA KATANGA

Omar Katanga

Katanga

Aliyekuwa mtangazaji wa Radio One,OMARY KATANGA (mlinda mlango no.1) hatimaye leo amejiunga na kituo kipya cha radio(E.FM) kinachorusha matangazo yake toka mikocheni Jijini Dar es salaam.

Katanga ametangaza kupitia katika ukurasa wake wa facebook kuwa amejiunga na E - fm.

Bila shaka wapenzi wa kipindi hicho watahama na watangazaji hao maana kipindi ndiyo kama kimevunjwa kabisa kwa kuwachukuwa waendeshaji wake maarufu ambao wamejizolea sifa hapa nchini.

"WAUNGWANA: WENGI MMEKUWA MKINIULIZA MBONA HAMNISIKII KWENYE KIPINDI CHA SPOTI LEO-NICHUKUE FURSA HII KUWAJULISHA KWAMBA HAMTANISIKIA TENA RADIO ONE KUANZIA IJUMAA ILIYOPITA AGOSTI 15,2014.

KWA UWEZO WA MUNGU MTANISIKIA TENA.......POLENI KWA USUMBUFU LKN....ASANTENI KWA USHIRIKIANO WENU."

Hayo ni maneno aliyo andika Omar Katanga kwenye ukurasa wake wa face book.


RAIA WA LIBERIA WAKATAZWA KUTOKA NJE ILI KUJIKINGA NA EBOLA


 Rais Ellen Johnson Sirleaf wa Liberia.
 
Rais wa Liberia Ellen Johnson Sirleaf ametangaza amri ya kutotoka nje kwa wananchi wake nyakati za usiku kuanzia saa tatu usiku hadi saa kumi na mbili asubuhi katika eneo la Kitongoji cha West Point viungani mwa Jiji la Monrovia.

Hali hiyo imetokana na tukio lililotokea hivi karibuni la watu kushambulia kituo cha afya katika eneo hilo na kusababisha wagonjwa 17 wa Ebola kutoroka.


Mgonjwa mmoja kati ya 17 waliotoroka katika kituo cha afya akiwa amebebwa na kijana.
 
Rais Sirleaf ameilaumu serikali yake kwa kutothibiti homa hiyo ya Ebola, kwani haikufanya vya kutosha kuboresha hali ya maisha ya raia walipopuuza ushauri wa wafanyakazi wa huduma za afya na kutotilia maanani tahadhari rasmi za Ebola.

Hata baada ya Liberia kutangaza hali ya dharura kufuatia mlipuko wa Ebola mapema mwezi huu, ugonjwa huo unazidi kusababisha vifo nchini humo.

Ebola haina tiba lakini Shirika la Afya Duniani (WHO) liliidhinisha matumizi ya dawa zilizokuwa zikifanyiwa utafiti kufuatia mlipuko mkubwa wa Ebola Afrika Magharibi .


PICHA:MWALIMU MKUU AKIPEWA ZAWADI YA KUFELISHA

Mwalimu mkuu shule ya msingi kamanga Bw.Lucas Nicolaus(Pichani) iliyoko wilaya ya chato amekabidhiwa zawadi ya kinyago cha kutisha (kina sura ya mtu zoba /mburura) baada ya shule yake kuburuza mkia katika matokeo ya mtihani wa taifa (NECTA) wa darasa la saba 2013. Wilaya ya chato huwa na utaratibu wa kuwatunuku zawadi za ngao na fedha taslimu kwa shule zilizofanya vizuri na kinyago cha kuogofya kwa shule zilizofanya vibaya. Zawadi hizo zilizotolewa na afisa elimu wa wilaya ya chato Bw.Angasirin Obed Kweka mbele ya baraza la Madiwani wilaya ya chato hapo jana.

Mimi nimependa sana utaratibu huu wa kuwatunuku, rai yangu ni kuomba na halmashauri zingine nchini ziinge utaratibu huu katika mitihani yote kuanzia shule ya msingi mpaka kidato cha sita,pia na NECTA waige mfano huu.  
Wadau mnaionaje huu mtindo kwani elimu hata ya zile shule kongwe nchini imekuwa ikizidi kushuka siku hadi siku. hii inaweza kuwa njia ya kurudisha hadhi ya elimu yetu kwa kiasi falani.


YANGA NA COASTAL ZAGONGANA PEMBA


Kikosi cha Yanga
Kikosi cha Coast Union
Picha Maktaba:
 
Katika kile kilichodaiwa kuwa ni maandalizi ya Ligi kuu ya Tanzania Bara ambayo inataraji kuanza hapo mwezi ujao wa Tisa ilitokea hali ya kushangaza pale timu mbili ambazo pia zinajiandaa na ligi hiyo YANGA na COASTAL Ziligongana Pemba jana. 

Baada ya timu ya Yanga kutua kisiwani kwa mafungu (juzi)siku ya Jumatatu na timu ya Coastal union nayo ilitua kwa mafungu kisiwani humo jana (siku ya Jumanne). 

Hali hiyo ilileta mkanganyiko wa nani atautumia uwanja wa Gombani kabla ya kukubaliana kuwa timu zote zitakuwa na vipindi viwili vya kufanya maoezi uwanjani hapo ambapo Coastal ndiyo wanaanza saa 12 asubuhi mpaka saa 2 mbili asubuhi na Yanga wanaanza saa 2 asubuhi mpaka saa 4, na wanarudi tena saa 8 mchana mpaka saa 10 jioni, ndiyo Coastal wanaingia tena kumalizia awamu yao ya pili.

Awali iliarifiwa kuwa ziara ya wana jangwani hao ilipangwa kuanza tarehe za mwanzoni mwa mwezi huu hivyo kufikia tarehe 17 hadi 18 ndiyo wangekuwa wanaondoka, lakini kwa kuwa jambo hilo limewekwa sawa ratiba ndiyo itakuwa hiyo, kufatia timu 2 hizo za bara kugongana kisiwani humo na wekundu wa msimbazi kuwa Unguja wadau wanahoji kuna ni visiwani??

 Chanzo: kitongoni(Pemba)


KIBONZO: KIPANYA NA SERIKALI MBILI AU TATU




MAGAZETI YA LEO: JUMATANO 20/08/2014





VIDEO: BARABARA ZA MAGARI YAENDAYO KASI ZIKIKAMILIKA HALI ITAKUWA HIVI




 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU