Facebook Comments Box

Friday, November 27, 2015

RAIS AMSIMAMISHA KAZI KAMISHNA WA MAMLAKA YA MAPATO TANZANIA (T.R.A)


Rais Dk John Pombe Magufuli amemsimamisha kazi Kamishna Mkuu wa mamlaka ya mapato Tanzania ( TRA) Rished Bade na kumteua Philiph Mpango kukaimu nafasi hiyo.


Taarifa kutoka ikulu zimesema kuwa uamuzi huo wa Rais Magufuli umefuatia ziara ya waziri mkuu bandarini iliyobaini upotevu wa makontena 349.



Aidha Rais Magufuli amemtaka Rished Bade kutoa ushirikiano kwa Philiph Mpango wakati uchunguzi ukiendelea.



RISHED BADE aliyesimamishwa kupisha uchunguzi.
www.facebook.com/eatv.tv


MSHAURI WA RAISI WA BURUNDI ANUSURIKA KIFO

Mshauri wa Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza amenusurika shambulio alipokuwa akitoka nyumbani kwake katika eneo la Kajaga, magharibi mwa mji mkuu Bujumbura.
Zenon Ndaruvukanye alinusurika bila majeraha yoyote, lakini mlinzi wake, ambaye alikuwa afisa wa polisi, alifariki kutokana na majeraha ya risasi.
Washambulijai walitoroka wakitumia gari aina ya Toyota  Hilux lakini polisi walipashana habari na gari lao likazuiwa maili kadha kutoka Kajaga. Waliacha gari hilo na kutorokea soko lililo karibu, lakini mwishowe wawili walikamatwa. Mmoja wao alifanikiwa kutoroka.

Gari hilo aina ya Toyota Hilux lilipatikana na silaha mbalimbali zikiwemo bunduki aina ya AK47 na guruneti. 
Polisi baadaye walipelekwa kwenye nyumba moja viungani mwa mji wa Bujumbura ambapo walipata silaha zaidi.
Mji wa Bujumbura umekumbwa na machafuko ambayo yamesababisha vifo vya watu zaidi ya 200 tangu Aprili.


SOMA VICHWA VYA HABARI KATIKA MAGAZETI YA LEO IJUMAA TAREHE 27-11-2015 HAPA




MBUNGE WA JIMBO LA UBUNGO KUPITIA CHADEMA ANAEWAKILISHA UKAWA SAID KUBENEA AWATEMBELEA WANANCHI WAKE

Kubenea akizungumza na waandishi wa habari na wananchi katika Soko la Ndizi la Mabibo.

Said Kubenea Mbunge wa jimbo la Ubungo, akiongea na wananchi katika Stendi ya Mabasi ya Ubungo Dar es Salaam kuwashukuru kwa kumchagua na kujua changamoto zao mbalimbali. Mbunge huyo alitembelea Soko la Mabibo, Kituo cha Mabasi cha Mawasiliano.
Hapa akiwaunga mkono wananchi kununua mananasi katika soko la ndizi la mabibo.
Vijana wakiserebuka baada ya kuzungumza na mbunge wao Said Kubenea katika Soko la Mabibo.
Said Kubenea akiwahutubia wananchi katika soko la Mabibo.


Wednesday, July 15, 2015

HATIMAYE CUF WATOA MSIMAMO WAO KUHUSU KUJITOA / KUBAKIA UKAWA

Viongozi wa vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA), kama wanavyo onekana wakiteta jambo Toka kushoto ni Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe, wa katikati yao ni Profesa Lipumba wa CUF na mwisho ni Joseph Mbatia wa NCCR.

Viongozi hao wakiwa wameshikana mikono kuonesha kuwa wao ni wamoja.

Baada ya Chama cha mapinduzi CCM kumpata Mgombea wake wa kiti cha urais wiki iliyopita mkoani Dodoma ambae ni John Pombe Joseph Magufuli.
 
Wanachama wa Umoja wa Katiba ya wananchi (UKAWA) wamekuwa na duku duku la kufahamu mgombea wao atakuwa nani.

Hali hiyo imeleta hamasa sana kwa wanachama hao kiasi cha kuona kama viongozi wao wanachelewa kuwajulisha mgombea wao ni nani na pia kuleta hofu kuwa CUF wamejitoa katika umoja huo.

Lakini CUF kupitia Naibu Katibu Mkuu wao wa Bara Magdalena Sakaya ametoa ufafanuzi kuhusu taarifa zinazoendelea kuenea, amethibitisha kuwa wao hawaja jitoa Ukawa na kuhusu kutokuwepo kwenye kikao akasema walichelewa kupata taarifa za kikao hicho maana hata wao wana vikao vingi ambapo wanajadili jinsi ambavyo madaraka yatakavyo kuwa endapo wakishinda uchaguzi mkuu huo ambao utafanyika Oktoba.
Naibu Katibu Mkuu wa Cuf Bi Magdalena Sakaya akijibu baadhi ya Tuhuma hizo


Friday, June 5, 2015

BARCELONA NA JUVENTUS ZAWASILI KATIKA JIJI LA BERLIN TAYARI KWA FAINALI YA UEFA JUMAMOSI TAR 06-05-2015

 Mabasi ya timu hizo kama yanavyo onekana hapa:
Andrea Pirlo kama anavyo onekana hapo akishuka kwenye ndege:


175 WATHIBITIKA KUFARIKI KATIKA AJALI YA MOTO GHANA

Takriban watu 175 wamefariki mpaka sasa kufuatia moto uliotokea katika kituo kimoja cha mafuta katika mji mkuu wa Ghana Accra.

Moto huo uliozuka siku ya jumatano usiku ulianza wakati wakaazi wa mji huo walipokuwa wakikabiliana na siku mbili za mvua kubwa ambayo imewaacha raia wengi bila makaazi pamoja na stima.

Mafuriko hayo yaliathiri juhudi za uokozi na huenda yalisababisha moto huo, Tayari Ghana imetangaza siku tatu za maombolezo ya kitaifa kufuatia vifo hivyo.
 
Mlipuko huo ulitokea hapo jana wakati mamia ya watu walipokuwa wamejihifadhi katika kituo hicho cha mafuta kutokana na mvua kubwa zinazonyesha.

Rais wa Ghana, John Mahama amesema janga hilo halitajirudia tena. Bwana Mahama amesema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari katika mji mkuu, Accra alipotembelea eneo la tukio.



AFISA MMOJA WA FIFA AKIRI KUPOKEA RUSHWA

Wizara ya Sheria ya Marekani imechapisha taarifa inayoelezea jinsi Afisa wa zamani wa FIFA Chuck Blazer alivyokiri kuwa yeye pamoja na wenzake walipokea rushwa ikiwa ni pamoja na kuichagua Afrika Kusini kuwa mwenyeji wa fainali ya kombe la dunia mwaka 2010.

Katika taarifa hiyo imeweka wazi mtandao wa malipo ya rushwa ulivyokuwa ukifanywa ndani ya shirikisho la soka duniani FIFA, taarifa zinazoegemea uchunguzi uliofanywa na shirika la kijasusi la Marekani FBI.

Taarifa hiyo ambayo inamwelezea Afisa huyo wa zamani wa Fifa kukiri kupokea rushwa sasa huenda ikaibua mengi kwenye kashfa ya rushwa inayoindamana shirikisho la FIFA.

Mmerakani huyo kwenye taarifa hiyo inadai alikuwa ni mmoja wa watu waliosuka mipango ya kupokea rushwa katika tukio jingine la fainali la kombe la dunia 1998.

Taarifa za Kukiri zipo katika maandishi wakati wa kesi yake mwaka 2013 ilipokuwa akisikilizwa katika mahakama ya Easten New York huko Marekani ambapo alikiri makosa kumi yaliyokuwa yanamkabili.

Blazer alikuwa afisa wa ngazi ya juu wa FIFA eneo la kanda ya Amerika Kaskazini na Kati na ukanda wa nchi Caribbean kuanzia mwaka 1990 hadi mwaka 2011.

Marekani imefungua kesi ya rushwa inayowakabili maafisa wa FIFA jambo lililofanya Rais wa FIFA Sepp Blatter kuamua kutangaza kujiuzulu.

CHANZO: BBC

Tuesday, March 10, 2015

MANCHESTER UNITED YATOLEWA NA ARSENAL F.A CUP OLD TRAFFORD

 Monreal akishangilia bao lake
 Danny Wellbeck akiifunga timu yake ya zamani bila huruma
 Angel Di maria akioneshwa kadi nyekundu na Mwamuzi baada ya kupata kadi mbili za njano, wakati timu yake ilipotolewa na Arsenal katika kombe lenye hadhi kubwa nchini Uingereza la F.A kwa kufungwa mabao mawili kwa moja(1-2).
Sant Carzola na Laurent Koscielny wakishangilia baada ya kipyenga cha kuashiria kuwa dakika 90 zimekamilika.

Kocha wa zamani wa Manchesta Utd Alex Furgasson alikuwepo uwanjani hapo kushuhudia timu yake ikifungwa katika kombe hilo lenye hadhi kubwa Uingereza.



Sunday, March 8, 2015

RAISI KIKWETE AREJEA NCHINI BAADA YA ZIARA YA SIKU MOJA NCHINI RWANDA

   Raisi Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Mkuu wa wilaya ya Kinondoni Bw. Paul Makonda baada ya kuwasili uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es salaam akitokea nchini Rwanda alikokwenda kwa ajili ya kuhudhuria Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki, na aliyekatikati ni Mkuu wa Wilaya ya Temeke Bi Sophia Mjema



Saturday, March 7, 2015

AENDA JELA KWA KUWAHI KUFIKA KAZINI NA KUANZA KAZI YAKE MAPEMAA

Kevin McGill

Mwendesha lori la kuzoa taka kwenye majumba ya watu mji wa Sandy Spring jimbo la Georgia nchini Kevin McGill Marekani anatakiwa kwenda jela wikiendi 14 kwa kisa ni kuwahi kuchukua taka mida ya saa 11 asubuhi badala ya saa 1 asubuhi.na kuwapigia watu kelele wakiwa wamelala.

Kervin McGill yeye mwenyewe alibaki mdomo wazi baada ya kusomewa mashitaka kwamba anapochukua taka saa 11 asubuhi anawapigia kelele waliolala na inakua usumbufu kwa 

wengine na majirani hao walijaribu kuifungulia kampuni yake Kervin McGill lakini wao walisema sisi hatuondeshi hilo lori, na ikabidi kibao kimgeukie yeye na kuhukumiwa kwenda jela wikiendi 14.

Kesi hiyo imewashtua watu wengi na kuwa gumzo kwenye vyombo vya habari huku wengi wao wakiwa wamepigwa na butwaa kwa mtu kwenda jela kwa sababu ya kuwahi kufanya kazi yake. 

Mtu kama huyu alistahili kupata onyo sio kwenda jela. Hakimu alimwambia Kervin McGrill kuanzia sasa anatakiwa achukue taka saa 1 asaubuhi na saa 1 usiku tu na si vinginevyo.


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU