Facebook Comments Box

Wednesday, December 25, 2013

MKURUGENZI WA KCMC AACHIA NGAZI

Mkurugenzi wa Hospitali ya KCMC ameachia ngazi. Hii imefuatia uamuzi wake alio utoa kwenye kikao cha bodi ya wakurugenzi wa msamaria mwema.
Dk Ntabaye ameomba bodi ya wakurugenzi wa msamaria mwema wasimuongeze mkataba mwingine tena.
Inasemekana mkurugenzi huyo ameacha manung'uniko na malalamiko mengi hospitali hapo pamoja na kushusha ari ya kazi kwa wafanyakazi wa hospitali hiyo.
Nafasi ya ukurugenzi kwa sasa imekaimiwa na Pro ulomi.


KOCHA WA SIMBA AFARIKI DUNIA

James Kisaka enzi za uhai wake.
Aliyekuwa kocha wa makipa wa Klabu ya Simba, James Kisaka amefariki dunia leo asubuhi katika Hospitali ya Burhan, Dar es Salaam. Kisaka aliyewahi kuwa kipa wa timu hiyo miaka ya nyuma, alikuwa akisumbuliwa na maradhi ya kichwa, macho na miguu kwa muda mrefu.
MUNGU AIPUMZISHE ROHO YAKE MAHALI PEMA PEPONI. AMINA
CHANZO: GPL


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU