Facebook Comments Box

Wednesday, February 27, 2013

ALIYEKUWA MWENYEKITI WA TUME YA UCHAGUZI KENYA SAMWEL KIVUITU AMEAGA DUNIA


336544_319369068086667_163569676999941_1031123_336563521_o

Wakili aliyekuwa mwenyekiti  wa tume ya uchaguzi ya Kenya,  ECK ndugu Samuel Kivuitu ameaga dunia
Taarifa zilizotolewa na familia ya Kivuitu zinasema kuwa marehemu aliaga dunia jana usiku mwendo wa saa nne katika hospitali ya MP Shah iliyopo jijini Nairobi, alikokuwa amelazwa kwa matibabu ya saratani.
Kivuitu alikuwa akisumbuliwa na saratani ya  koo ambapo alikuwa akipelekwa katika hospitali hiyo mara kwa mara kwa muda wa miaka miwili.

Marehemu Kivuitu alivuma sana mwaka 2007 baada ya matokeo ya uchaguzi wa Rais nchini Kenya yaliyotangazwa na Tume ya Uchaguzi ya Kenya wakati huo ECK yeye akiwa Mwenyekiti, matokeo ambayo yalipokelewa kwa hisia tofauti na kuwa sababu hasa ya kuchochea machafuko makubwa kuwahi kushuhudiwa katika historia ya Kenya ambapo watu 1,133 waliuawa na wengine laki sita na nusu kuachwa bila ya makazi.


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU