Facebook Comments Box

Sunday, November 9, 2014

MWANAMUZIKI MKONGWE AMIGOLAS AFARIKI DUNIA

AMIGOLAS
Mwanamuziki mkongwe wa Bendi ya Africans Stars maarufu kama Twanga pepeta amefariki dunia katika hospitali ya taifa ya Muhimbili.
Marehemu alipelekwa hapo akiwa nasumbuliwa na matatizo ya moyo.


PICHA YANGA ILIPO WAONESHA MGAMBO MATAA YA MJINI

Timu ya Young Africans Sports Club jana imewaonesha Mgambo JKT mataa ya mjini baada ya kuwachabanga mabao mawili kwa bila. Mabao ya Yanga yamefungwa na Simon Msuva katika kipindi cha pili.
Kiungo mbrazili Coutinho akitafuta njia ya kumtoka beki wa mgambo

Kikosi cha Yanga

Kikosi cha Mgambo JKT

Msuva akishangilia bao lake la pili




PICHA ZA BARABARA YA UKONGA MAZIZINI ILIYOTUMIA MILIONI 90 ILIVYO SASA



Hii ndiyo ile barabara ya Ukonga Mazizini- Moshi Bar ambayo inadaiwa kugharimu kiasi cha shilingi milioni 90 kuikarabati kwa kiwango cha changarawe kwa umbali wa kilometa tatu. Picha hizi ni madimbwi ya mwanzo tu ya hizo kilometa tatu.



Meya Jerry Silaa wa Ilala ambaye ni Diwani wa Gongo la Mboto alipotembelea aliwaambia wananchi kuwa fedha za ujenzi huo ni kutoka mfuko wao. 
Picha zifuatazo ni za siku Meya Silaa alipotembelea ujenzi.



Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala Jerry Silaa jana amefanya ziara fundi ya ukaguzi wa ujenzi wa barabara ya Ukonga Moshi Bar ya kilometa 3 kwa kiwango cha changarawe awamu ya kwanza, ikiwa ni utekelezaji wa miradi ya dharura kulingana na uharibifu wa miundo mbinu uliotokea baada ya mvua kubwa kunyesha. Mradi huo unagharimu kiasi cha shilingi millioni 90. Pesa za ujenzi huo zinatoka Halmashauri ya Manispaa ya Ilala. Pia barabara hiyo itawekwa lami kwa awamu ya pili ndani ya mwaka huu kwa kilomita tatu.



Greda likirekebisha Barabara ya Ukonga-Mazizini kulekea Moshi Bar



Mwonekano wa barabara hiyo


SHEREHE ZA JANDO BUTIAMA



Wanamwita "Dokta" wa kijiji cha Ryamisanga wilayani Butiama akiendelea na shughuli yake ya kumtahiri kijana kwa dakika 17 bila ganzi.



Baadhi ya vijana ambao wameshatahiriwa wakimtizama mwenzao ambaye anafanyiwa tohara



"Dokta" akijiandaa kuifanya kazi yake




Mashuhuda







Baadaye ni vinywaji



Msosi kama huu pia ulikuwepo



Picha, maelezo na Shomi Binda: HIVI NDIVYO TOHARA ZA KABILA LA KIKURYA ZINAVYOFANYIKA

WIMBO AMBAO LOKASSA YA MBONGO AMEMUIMBIA RAIS KIKWETE





 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU