Facebook Comments Box

Friday, October 31, 2014

SHEIKH SORAGA UNAJICHANGANYA NA UNAPOTOSHA

Sheikh Fadhil S. Soraga
Hivi karibuni kumekuwa na barua ya katibu wa mufti wa zanzibar Sheikh Fadhil S. Soraga kilichonichanganya ni Katibu huyo kuto ikanusha barua hiyo ambayo haina kichwa cha juu cha barua na anuani (Headed letter). Ukiiangalia utaiona imekaa kama tangazo na chini ina saini ya sheikh huyo.Nadhani wengi wetu hatuuijui saini ya Sheikh Soraga na huenda watu wameitumia vibaya ili kumdhalilisha. Kingine kinacho nichanganya ni kuwa kikao kilifanyika tarehe 18 mwezi wa 8 kwanini leo ndio iwekwe kwenye mitandao ya kijamii na iwe gumzo?

Nahisi kuna watu wanataka kuwavuruga waislam wa Zanzibar au kuanzisha mjadala huu ili baadae walipitishe maana ni dhahiri kuwa ile kuswali kufuata uislam na idadi ya waislam wa Zanzibar ina waumiza.

Labda tuzungumze upande wa pili huenda ni kweli Sheikh Soraga ameandika maana hawa BAKWATA kutumiwa ni raisi sana (Naomba wanisamehe kwa kauli hii lakini ndio ukweli) watakuwa wameambiwa na mtu mmoja mwenye hela ambae huwapa vijisenti sasa wamelileta hili. Wakasahau kuwa ikiishakuhusu swala atawaambia hata adhana na kwenda msikitini pia inamkera maana inaonesha haridhiki na uislam kabisa. Inakuwaje asichukizwe na adhana ambayo hutolewa kwa nguvu na kuna wakati mtu hugeuka kulia na kushoto ili kutawanya sauti. Aje achukizwe na nyiradi ambazo husemwa na imam mara moja tu na wengine kufuatiliza kwa mdomo.

Naomba BAKWATA wawe wanafikiria kidogo kabla ya kuamua jambo. Kwani huko kuna matamasha ya filamu na mziki ambayo yanakesha usiku kucha na sijasikia malalamiko. Mi nina uhakika wameanza hapo ila watakuja mpaka kwenye adhana.

Tangazo/Barua ya katibu wa mufti Zanzibar



DAR ES SALAAM MPAKA ZANZIBAR SASA KWA BARABARA


Picha(maktaba)

BAADA ya ndoto ya kuziunganisha pande mbili za katikati ya Jiji la Dar es Salaam na Kigamboni kwa daraja lenye umbali wa meta 680, Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) linaangalia uwezekano wa kujenga daraja la kihistoria zaidi litakalounganisha Dar es Salaam na Zanzibar.

Kwa sasa, uongozi wa shirika hilo upo katika mazungumzo na wataalamu mbalimbali ili kuangalia uwezekano wa kujenga daraja hilo katika bandari ya Dar es Salaam kwa upande wa Tanzania Bara na Unguja, kwa upande wa Zanzibar.

Umbali kati ya Dar es Salaam na Zanzibar ni kilometa 73.43, sawa na maili 45.62 hivyo kuwapo kwa mradi huo ni jambo linalowezekana, kwani kuna madaraja marefu zaidi duniani yanayounganisha upande mmoja wa bahari na mwingine.

Kwa sasa, daraja refu kabisa duniani ni lile la Danyang–Kunshan lililopo China ambalo lina umbali wa kilometa 165, sawa na maili 102.4. Daraja hilo lilifunguliwa Juni mwaka 2011.

Hayo yameelezwa na Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Dk Ramadhan Dau wakati alipokuwa akijibu swali la Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii, Said Mtanda ambaye alitaka kufahamu kama kuna matarajio ya kujenga daraja kubwa zaidi, ikiwezekana la kati ya Dar es Salaam na Zanzibar.

Alisema wapo katika mazungumzo na wataalamu mbalimbali ambapo mazungumzo hayo yakienda sawa, ujenzi wa daraja hilo huenda isiwe ndoto, bali ukweli.

"Hilo wazo lipo mheshimiwa na tayari tumeshaanza mazungumzo ya awali, kwa hiyo hilo wazo lipo na sisi tulilifikiria," alisema Dk Dau.

Kamati hiyo ilifanya ziara katika miradi mikubwa mitatu ya shirika hilo ambayo ni daraja la Kigamboni, ujenzi wa nyumba za Mtoni Kijichi na 'Dege Eco village' ambao una nyumba zaidi ya 7,000.

Akizungumza wakati wa kuhitimisha ziara hiyo, Mtanda alisema, kamati yake imeridhishwa na miradi hiyo ya NSSF ambayo inaendelea huku akitaka kuongezwa kwa kasi ili watanzania waanze kunufaika na miradi hiyo.

"Muangalie na hilo la ujenzi wa daraja la kutoka Dar es Salaam hadi Zanzibar na mradi wa makazi bora na salama ambao utaweza kubadili taswira ya Jiji la Dar es salaam," alisema.

Alisema kamati yake isingependa kuona changamoto zozote ambazo zinaweza kukwamisha miradi hiyo na kwamba serikali kupitia Wizara ya Ujenzi itaangalia namna ya kuunganisha miundombinu karibu na miradi hiyo.

"Lakini pia tumesikia kuwa serikali inadaiwa na mifuko ya hifadhi, tunashauri serikali kuilipa mifuko hii ili kuifanya kuwa na nguvu na kuweza kuleta maendeleo," alisisitiza Mtanda.


NDUMBARO ATEMA CHECHE

Kampuni ya Mawakili ya MALETA & NDUMBARO ADVOCATES, ambayo inawakilisha vilabu 13 vya LIGI KUU YA VODACOM TANZANIA, inapenda kutoa tamko kwa umma kama ifuatavyo:

Kampuni ya MALETA & NDUMBARO ADVOCATES, iliteuliwa na vilabu 13 vya LIGI KUU YA VODACOM TANZANIA, kwa maandishi, ili kuwawakilisha na kuwatetea katika kudai haki zao ambazo tayari SHIRIKISHO LA SOKA TANZANIA (TFF) liliamua kukata fedha za udhamini na viingilio vya mechi pasipo kuwashirikisha. 
 
Dk. Damas Daniel Ndumbaro, wakili mwandamizi, ndiye aliyekabidhiwa file hilo kwa mujibu wa utaratibu wa ofisi yetu.
Kwamba, tarehe MALETA & NDUMBARO ADVOCATES, kupitia wakili wake mwandamizi, Dk. Damas Daniel Ndumbaro, iliandika barua ya madai (Demand Notice) TFF na kuongea na waandishi wa habari.
 
Kwamba Mheshimiwa Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Mh. Juma Nkamia (MB) aliitisha mkutano kati ya TFF (ambayo iliwakilishwa na Wilfred Kidau-Mjumbe Kamati ya Utendaji, na Selestine Mwesiga, Katibu Mkuu), Bodi ya Ligi, Vilabu vya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania na Dk. Damas Daniel Ndumbaro (kama wakili wa vilabu). 
 
Mwenyekiti wa Mkutano huo, Mh. Juma Nkamia alitoa fursa kwa TFF, Bodi ya Ligi, na Wakili wa vilabu kutoa maelezo yao na hatimaye Mh. Juma Nkamia alitoa maelekezo kama ifuatavyo:
 
Jamal Malinzi sio Rais wa Nchi, na aliwaagiza wawakilishi wa TFF wafikishe ujumbe huo kwa Bw. Jamal Malinzi. Makato ya Tshs. 1000/= kwa kila tiketi ni wizi wa mchana.TFF isitishe makato ya 5% na Tshs. 1000 kwa kila tiketi mpaka watakapoongea na kukubaliana na vilabu.
 
Baadaya hapo, MALETA & NDUMBARO ADVOCATES, ilikutana na vilabu ambayo vilikuwepo siku hiyo na kukubaliana kuwa sasa tusibiri majadiliano na TFF na kwamba MALETA & NDUMBARO ADVOCATES, ikiongozwa na Dk. Ndumbaro iandae mapendekezo ili yajadiliwe na mkutano mkuu wa vilabu.
 
Kwamba tarehe 11 Oktoba 2014 TFF ilifanya mkutano wa Kamati ya Utendaji na kutoa tamko kuwa kumekuwa na taarifa za upotoshaji kuhusu kanuni za ligi kuu na kwamba Sekretariati ya TFF imefungua mashtaka dhidi ya Dk. Ndumbaro ambaye ni Mjumbe wa Bodi ya Ligi na Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya Klabu ya Simba.
 
Kwamba Kamati ya Utendaji ya TFF iliendelea kusema kuwa Kutokana na madai ya klabu kuhusu vipengele kadhaa vya Kanuni za Ligi Kuu 2014/15, Kamati ya Utendaji imepanga kukutana na viongozi wa klabu za Ligi Kuu siku ya Jumamosi, Oktoba 18 mwaka huu ili kuwasikiliza na kushauriana kuhusu changamoto za kikanuni na uendeshaji wa mashindano kwa ujumla na kwamba.
 
TFF imefanya kosa kumshitaki Dk. Ndumbaro kwa kofia ya Mjumbe wa Bodi na Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi Simba kwasababu barua toka MALETA & NDUMBARO ADVOCATES, barua za vilabu 13 na taarifa kwa vyombo vya habari ilikuwa bayana kuwa Dk. Ndumbaro anawakilisha vilabu vya ligi kuu kama wakili toka kampuni ya MALETA & NDUMBARO ADVOCATES na wala sio mwakilishi wa Bodi au Mwenyekiti wa uchaguzi wa Simba kwasababu hakukuwa na uchaguzi wa Simba.

Kwamba TFF inakiri kuwa klabu za Ligi kuu zinapaswa kukutana na TFF kujadili kasoro za Kanuni za Ligi kuu. Hapa TFF inakiri kuwa haikukutana na vilabu katika mchakato wa kutunga kanuni hizi na kwamba kanuni hizo zinakasoro. Ifahamike kwamba hayo ndio madai ambayo vilabu kupitia MALETA & NDUMBARO ADVOCATES iliyapeleka TFF kwa maandishi.

Tarehe 7 Oktoba 2014 TFF iliepeleka Mshtaka katika Kamati ya Nidhamu dhidi ya Dk. Ndumbaro. Kamati ya Nidhamu ilipanga kusikiliza Mashtaka hayo tare 09 / 10 / 2014 saa 08: oo mchana, yaani siku mbili tu baadaya ya kuwasilishwa katika kamati ya nidhamu. Mashitaka hayo yalijaa ubabaishaji na chuki binafsi dhidi ya wakili wa vilabu 13 vya Ligi Kuu.

Kwamba TFF ililazimisha kusikiliza mashtaka hayo kwa haraka na dharura ya ajabu pasipo kuwepo Dk. Ndumbaro ambaye alitoa taarifa ya maandishi kuwa atakuwa safarini Nchini Marekani kikazi, kwa barua ya tarehe 8th October 2014.

Kwamba Kamati ya Nidhamu ya TFF ilitoa maamuzi ya kumfungia Dk. Ndumbaro asijihusishe na Soka kwa kipindi cha miaka saba pasipo kutoa sababu za msingi za kufanya hivyo wala kutoa nakala ya hukumu hiyo.

Kwamba MALETA & NDUMBARO ADVOCATES kwa niaba ya vilabu vya Ligi kuu inapinga adhabu hiyo ya uonevu kwa misingi ifuatayo:-

Kamati ya nidhamu ya TFF haina mamlaka ya kisheria ya kushughulikia suala hili. (ARTICLE 2, 3,76 and 77 of TFF Disciplinary Code) Kamati ya nidhamu ya TFF ilikosea kuamua suala hili bila kutoa haki ya msingi ya kuisikiliza MALETA & NDUMBARO ADVOCATES na Dk. Damas Daniel Ndumbaro
Hakuna Chombo chochote cha TFF chenye mamlaka ya kumzuia au kumfungia Wakili wa kujitegemea kuwawakilisha wateja wake.

MALETA & NDUMBARO ADVOCATES inaandaa kesi ya madai dhidi ya TFF kwa kuizuia isifanye biashara yake halali.

MALETA & NDUMBARO ADVOCATES inapenda kuwajulisha wadau wote kuwa kupinga maamuzi ya Kamati ya Utendaji ya TFF sio kosa. Ikumbukwe kuwa JAMAL MALINZI aliwahi kupinga maamuzi ya FIFA, CAF na TFF kuhusu mabadiliko ya Katiba ya Mwaka 2013, kwa njia ya Circular Resolution, ili kuunda Kamati za Rufaa ya Uchaguzi, Kamati ya Maadili na Club Lincensing. Lakini leo Jamal Malinzi hataki kupingwa huyu ni dikteta.
 
Kwamba MALETA & NDUMBARO ADVOCATES inaandaa mashtaka dhidi ya Uongozi wa TFF, katika mambo yafuatayo:
Ubadhirifu wa US$ 200,000 fedha za TBL udhamini wa Taifa Stars
Kupinga Maamuzi ya FIFA kurejea Karume ( Haya yalikuwa mapendekezo haikuwa amri) Kufanya matumizi na manunuzi bila kibali cha kamati ya fedha ambayo ndiyo kamati ya manunuzi ya TFF kwa mujibu wa kanuni za manunuzi za TFF, manunuzi yaliyofanyika yanahusiana na Vifaa vya michezo wakati wa maboresho ya Taifa stars, Tiketi za ndege za Taifa Stars, timu ya wanawake na za vijana katika michezo yake na hotel za kambi ya timu ya Taifa ambapo hakukuwa na tenda zilizotangazwa wala ushindanishwaji wa aina yoyote jambo linaloashiria matumizi mabaya ya madaraka na fedha na kwa kuwa Rais ndiye msimamizi wa shughuli za sekretariet kikatiba jambo hili linakuwa pamoja na mengine ni suala la kimaadili kwa sheria za mpira.

Kwamba MALETA& NDUMBARO ADVOCATES inaandaa mashtaka dhidi ya Jamal Malinzi kwa Kupinga Maamuzi ya FIFA, CAF na TFF ili kufanya marekebisho ya Katiba mwaka 2013.
 
Tarehe 21 Oktoba 2014, Dk. Damas Daniel Ndumbaro alikata rufaa dhidi ya uamuzi wa Kamati ya TFF lakini mpaka sasa Kamati ya Rufaa ya Nidhamu TFF haijasema lina inakaa. Tunatarajia kuwa haraka na dharura iliyotumika katika kuamua shauri katika kamati ya nidhamu itatumika pia kuamua shauri katika rufaa. Leo ni siku ya 10 toka rufaa ikatwe lakini bado kimya wakati ilichukua siku 2 tu kusikiliza kesi ya msingi.
 
KWAHIYO Dk. Damas Daniel Ndumbaro wa MALETA & NDUMBARO ADVOCATES kwa naiba ya wateja wetu tunasema kuwa:

Tutaendelea na kuwawakilisha wateja wetu kwa uadilifu wa hali ya juu. Kwamba madai yote tuliyoyasema katika barua ya awali dhidi ya TFF ikiwemo madai yanayohusiana na Mkutano Mkuu yapo pale pale.
 
Tumekata Rufaa dhidi ya maamuzi ya kamati ya nidhamu ya TFF kuanzia tarehe 21 Okotba 2014 Tunaandaa mashtaka dhidi ya Uongozi wa TFF kwa ubadhirifu wa fedha za umma Tunaandaa mashtaka dhidi ya TFF kwa kosa la kupinga agizo la FIFA kurejea Karume.
 
Tunaandaa Mashtaka dhidi ya Jamal Malinzi kwa kosa la kupinga Maamuzi ya TFF, CAF na FIFA katika mabadiliko ya Katiba ya TFF mwaka 2013.
 
Wako 
Dk. Damas Daniel Ndumbaro (PhD)
For: Maleta & Ndumbaro Advocates
www.maletandumbaroadvocates.com

Nakala: i. Vilabu 13 vya Ligi Kuu
ii. Mh. Naibu Waziri
Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo
Maleta & Ndumbaro Advocates
www.maletandumbaroadvocates.com


BAADA YA LORI KUFELI BREAK USO KWA USO NA SIMBA MTOTO WAMI


Basi la Simba mtoto linalofanya safari zake kati ya Dar es Salaam na Tanga limegongana uso kwa uso na Lori la mizigo katikati ya Daraja la Mto Wami mkoani Pwani, Dereva wa lori hilo amefariki papo hapo na wengine kujeruhiwa.

Kitongoni blog inaendelea kutafuta taarifa zaidi za tukio hilo.

Wednesday, October 29, 2014

ROLI LA MAFUTA LAANGUKA NA KUUNGUA LOTE KIMARA KWA THOMAS

Lori la mafuta limeanguka na kuungua lote eneo la kimara kwa Thomas. Ajali hiyo imesababisha foleni kubwa kwa magari yanayo elekea kimara. Lori hilo limeanguka katika kituo cha magari yaendayo kasi. Hamna mtu alie jeruhiwa au kufa.




Tuesday, October 28, 2014

AJALI KONA YA JETI: LORI LAIANGUKIA HIACE


Kumetokea ajali mbaya mida hii maeneo ya Jeti Lumo mwisho wa lami ambapo gari kubwa la mizigo limeangua daladala iliyokuwa kituoni.


Ajali hiyo imetokea wakati gari hilo semi-trailer ikikata kona pale mwisho wa lami ambapo kontena lilianguka na kutua juu ya bodi ya daladala.


Mtoa taarifa wangu amesema hali ni mbaya na bado hajajua idadi ya vifo na majeruhi ujumla.Pia gari imepondeka sana jambo ambalo linaashiria hatari zaidi.


Kuna gari la kunyanyua makontena limeshafika pale lakini limeshindwa kutoa msaada wa uhakika kutokana na kuzidiwa uzito na kontena ambapo likijaribu kunyanyua kontena ushuka.

Hamna mtu yoyote aliepoteza maisha maana Hiace hiyo ilikuwa imepaki kusubiri muda wake wa kupakia abiria.



ABUBAKAR SALUM "SURE BOY" ACHAGULIWA MCHEZAJI BORA WA OKTOBA



Bodi ya ligi kuu soka Tanzania bara TPL Bord imemtangaza mchezaji  wa Azam FC Salum Abubakar  ‘Sure  Boy’ kuwa mchezaji bora wa mwezi oktoba katika ligi kuu soka Tanzania Bara.

Akizungumza leo Jijini Dar es Salaam kwa niaba ya Bodi ya ligi, Mkurugenzi wa Masindano wa TFF Boniface Wambura amesema mchezaji uyo amechaguliwa baada ya kuwasinda kwa vigezo wachezaji wenzake katika michezo ya mwezi  uu wa oktoba.
Mwezi  uliopita  mchezaji  wa Mbeya City Antony Matogolo aliibuka  mchezaji bora wa  mwezi  septemba na kuambulia  kitita cha shilingi milioni moja.


NAHODHA NA GOLIKIPA WA AFRIKA KUSINI AUAWA NCHINI HUMO



Nahodha na golikipa wa timu ya Taifa la Afrika kusini Senzo Meyiwa enzi za uhai wake.

Nahodha na golikipa wa timu ya Taifa la Afrika kusini Senzo Meyiwa amefariki dunia baada ya kupigwa risasi. Jeshi la polisi la nchi hiyo limesema. Tukio hilo limeripotiwa kutokea katika nyumba ya mpenzi wake iliyopo katika mji wa Vosloorus kusini mwa Johannesburg.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 aliichezea klabu ya Orlando Pirates na alicheza mechi nne zilizopita za timu yake ya taifa katika mechi za kufuzu za fainali ya mataifa ya Afrika.

Jumamosi alikuwepo katika tukio la timu yake pindi waliposonga mbele katika nusu fainali ya ligi ya Afrika kusini.
Katika maelezo yake Jeshi la polisi la afrika kusini limesema kwamba Meyiwa ameripotiwa kufariki wakati akiwasili hospitalini.

Chanzo: BBC

Sunday, October 26, 2014

SIMBA YAWASIMAMISHA KIEMBA,KISIGA NA CHANONGO

AMRI KIEMBA
Klabu ya Simba SC imewasimamisha wachezaji wake watatu kutokana na kile ninachodhaniwa wachezaji hao kuwa sehemu ya klabu hiyo kufanya vibaya, wachezaji waliosimamishwa ni viungo Amri Kiemba,Shabani Kisiga na Haruna Chanongo,hapo jana jijini Mbeya Simba ililazimishwa sare ya tano msimu huu na Prisons.
Shabaan Kisiga

Taarifa kutoka chanzo cha kuaminika ndani ya klabu hiyo kinasema pia benchi la ufundi limepewa changamoto ya kuakikisha timu hiyo inakusanya pointi tisa  kutoka kwenye michezo mitatu inafuata kama ikishindikana basi benchi Zima la ufundi nalo litapigwa chini.

Habari zaidi zikisema kuwa mshambuliaji wa kigeni Hamis Tambwe akipewa onyo kwa kuhusishwa na Simba ukawa huku Ramadhan Singano nae akipewa onyo kali pia.

 Kocha msaidizi Matola na mtoa tiba kwa vitendo Bwana Gembe wamesimamishwa kwa muda usio julikana.


PICHA: MAADHIMISHO YA GROUP LA KANDADA: TEAM ISMAIL YAFUNGWA NA TEAM DIZO MOJA

Katika maadhimisho ya Group la kandanda la Facebook kutimiza miaka minne. Ilifanyika mechi kati ya Team Ismail na Timu Dizo moja. Team Dizo iliibuka na ushindi wa magoli manne kwa moja. Team zote zilionesha soka safi na la kupendeza.

chini ni picha za bonanza hilo.

mtanange ukiendelea

Kipindi cha Pili Nassoro Binslum akiwa tayari kuanza kazi


wakati wa zawadi







wakishangilia ushindi wa taem Dizzo one





keki na kombe

mameneja wa timu mbili wakipongezana


mfungaji wa mabao matatu "hat trick" akipewa zawadi ya mpira

keki ikikatwa


Patrick Dumulinyi muanzilishi wa group la kandanda akilishwa keki



STAND UNITED WAKIINGIA UWANJANI NA TINGATINGA WAKIWA NA MBUNGE WAO

Hii ndio njia ambayo stand united waliitumia kuingia uwanjani. Mwenye shati la kitenge ni mbunge wa shinyanga mjini ambae pia ni Naibu waziri mh Masele. 

Hii inatakiwa kukemewa ni hatari.





Friday, October 24, 2014

KUELEKEA EL CLASICO ANGALIA PREVIEW HII



HATIMAYE DIAMOND ASALIMISHA SARE ZA JESHI

Kushoto ni Ney wamitego, Diamond Platnum, na Dancer wa Diamond wakiwa katika jukwaa la Fiesta hivi karibuni wakiwa wamevalia mavazi ya Jeshi.

MSANII wa muziki wa kizazi kipya, Naseeb Abdul 'Diamond', amekiri kuhojiwa na polisi baada ya kukutwa na hatia ya kuvaa mavazi yanayoaminika kuwa ni sare ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).

Hata hivyo msanii huyo alidai kwamba mavazi hayo hayakuwa sare za jeshi hilo na kwamba yeye aliyanunua alipokuwa Ujerumani ingawa baada ya kuhojiwa aliyasalimisha.

Diamond alipanda jukwaani Jumamosi iliyopita katika onyesho la Fiesta jijini Dar es Salaam akiwa na mavazi hayo jambo ambalo liliibua mjadala kwa watu walio wengi.

Diamond alikiri kupata ujumbe uliomtaka kufika Kituo cha Oysterbay, Dar es Salaam na madansa wake akiwa na nguo hizo,
"Awali Meneja wangu alishikiliwa kwa muda na mimi nikatakiwa kufika na zile nguo nikiwa na madansa wangu ambao pia walizivaa, nilifanya hivyo na kuziacha nguo baada ya taratibu zote za kisheria kukamilika," alisema.

"Nisingeweza kukaidi amri ya dola, nilifika na yale mavazi na nikahojiwa kwa saa kadhaa. Nikaeleza kwamba yalikuwa yakifanana tu na ya jeshi na hayakuwa sare rasmi za jeshi, kikubwa nilihitaji kumaliza tatizo," alisema.



Q.CHILLAH AELEZEA NANI MKALI KATI YA DIAMOND NA ALI KIBA

Msanii wa Bongo Fleva Q. Chillah

Mapya yanazidi kuibuka kuhusu ushindani wa Diamond na Ali Kiba ambapoushindani huo ulianzia katika hitimisho la tamasha la Fiesta lililofanyika katika viwanja vya Leaders Club Dar. 

Mashabiki wa wasanii hawa wawili wanavutana huku kila mmoja akisema mwenzake ana kipaji na anamfunika mwenzake. Inasemekana kuwa kuna baadhi ya mashabiki walikodiwa kwa ajili ya kumzomea Diamond wakati akitoa burudani siku ya Fiesta na hilo lilithibitishwa na Babu Tale ambaye ni meneja wa Diamond.

kwa sasa katika mziki wa Bongo Flava kumekuwa na fitina nyingi wakati mwingine wasanii kwa wasanii wanachonganishwa na mwisho wa siku unakuwa ugomvi, kwa mfano sasa hivi bifu la Ali Kiba na Diamond.

Q Chief : "Yote wanayopitia ni changamoto ambazo pengine hawakuwahi kuzania kwamba watapitia. Mimi nimepitia situation ambazo zimenijenga kuwa "sugu" na "Legendary" ndiyo maana ya kuwa mkongwe unapitia situation ambazo watu wengine wanakulazimisha ufike huko. 

Hata kama upo level fulani wanakushusha kwa kufikiria kwamba wanaweza kukushusha. Unapandishwa na watu, unapandishwa na mwenyezi Mungu, unashushwa na watu, unashushwa na mwenyezi Mungu. 

Mfano niliangalia Fiesta kwenye TV sikwenda kwa sababu nilikuwa na mambo yangu Studio, hakuna kitu kigeni nlichokiona, nimeona msanii wa marekani anafunikwa na msanii wa Tanzania ambaye ni Ali Kiba. 

Nmeona Ali Kiba ambaye amekaa kimya kwa miaka mitatu bila Airtime na watu wamemzungumzia vibaya, vizuri na nini wamemkubali tena. Ikiwa ni mtu yule yule ambaye wamemkataa na wakumuweka mtu mwingine juu. 

Hakuna kitu kisichowezekana, matokeo uliyoyaona juzi ndio matokeo yanayotokea na yataendelea kutokea. Hakuna Mungu wa hii kazi, hakunaga mfalme wa hii kazi ila kuna masultan wa Hii Kazi.



SOMA MAGAZETI YA LEO IJUMAA TAREHE 24 SEPTEMBA 2014 HAPA




 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU