Facebook Comments Box

Wednesday, September 3, 2014

MAGAZETI YA LEO: JUMATANO 03/09/2014




DR SLAA ATOA MSAADA WA MADAWATI MTAMBANI

Dr Willibrod Slaa jana amekabidhi Madawati 60 kwa Shule ya
Mvumoni Seminary iliyoko Msikiti wa Mtambani Kinondoni.
Msaada huu ni kutimiza ahadi aliyoitoa Dr. Wilbrod Slaa Katibu Mkuu wa chadema kwa niaba ya chama alipotembelea msikiti huo kutoa pole za Chama kutokana na ajali ya moto iliyoteketeza mali mbalimbali pamoja na madawati 60 ambayo yalikuwa yakitumika na wanafunzi wa kidato cha nne msikitini hapo.

msikiti wa mtambani ulipata ajali ya moto siku kadhaa zilizopita na kusababisha hasara kubwa lakini cha muhimu ilikuwa ni kuwawezesha wanafunzi wa kitado cha nne shuleni hapo ambao tayari wameanza mitihani juzi.



 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU