Facebook Comments Box

Friday, December 12, 2014

KIIZA ATUPWA NJE YANGA

Hamisi Kiiza "Diego "
Taarifa za kuaminika ambazo tumezipa hivi punde, klabu ya Yanga ipo mbioni kukatisha mkataba na mshambuliaji Hamis Kiiza raia wa Uganda.

Mmoja wa watu ambao wanashughulika na usajili wakati akiongea na mtandao huu amesema

‘’Tutakaa chini kuzungumza na Kiiza ili kuangalia namna ya kuachana kwa amani,baada ya Mliberia kufuzu vipimo vya afya hatuna jinsi lazima tuliondoe jina la Kiiza kwenye usajili wetu,kilisema chanzo hicho ‘’

Yanga inalazimika kupunguza mchezaji mmoja wa kigeni hasa baada ya mshambuliaji Kpah Sean Sherman kufuzu vipimo vya afya na kuwa mbioni kusaini mkataba na klabu hiyo.

Hivi karibuni Yanga ilimsainisha kiungo Emerson toka nchini Brazil mkataba wa mwaka mmoja, ukiachana na Kiiza wachezaji wengine wa kigeni ndani ya klabu ya Yanga ni Mbuyu Twite,Haruna Niyonzima, Kpah Sean Sherman na wabrazil Courtinho na Emerson.

Ikumbukwe Idadi ya wachezaji wa kigeni wanaotakiwa kusajiliwa na timu ni watano.


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU