Facebook Comments Box

Wednesday, December 11, 2013

ABIRIA WA TRENI YA MWAKYEMBE WAANZA KUPITIA MADIRISHANI HEBU JIONEE KATIKA PICHA HAPA

Na Kamera ya kitongoni Blog:
 
Treni inayobeba abiria katika Jiji la Dar es Salaam maarufu kama Treni ya Mwakyembe ambayo inafanya safari zake kutoka Stesheni katikati ya Jiji hadi Ubungo - Maziwa. Imejizolea umaarufu mkubwa katika kuwasaidia abiria wengi wanaopata taabu ya usafiri katika Jiji hili.

Kadri siku zinavyozidi kwenda usafiri huu wa treni umekuwa unapendwa sana na watu walio wengi japo hauwasaidii watu wote ndani ya Jiji hili kutokana na sababu kwamba hauna foleni hivyo kuwafanya watu walio wengi kuwahi kufika nyumbani kwao ukilinganisha na usafiri mwingine wa gari ambapo umekuwa na foleni kila kukicha.

Kutokana na kupendwa huko na watu walio wengi usafiri huu sasa umeanza kuwa wa taabu sana kwa abiria kupanda pindi safari inapotaka kuanza Stesheni. 

Baadhi ya abiria wamekuwa wakipitia madirishani kama ambavyo tumezoea kuona kwenye baadhi ya mabasi ya kubeba abiria maarufu kama 'daladala' hapa Dar es Salaam kama walivyokutwa na Kamera ya Kitongoni hapo jana siku ya Jumanne tarehe 10/12/2013. 
Abiria wakiwa wamepanga foleni kabla Treni haijafika Stesheni.
Abiria huyu kama unavyomuona hapa akilipigia dirisha hesabu ili apande na kulifanya dirisha ndiyo mlango.


Baada ya kulitathmini dirisha Jamaa aliweza kupanda na kama anavyoonekana akiingia kupitia dirishani na huu sio ustaarabu kabisa.
Abiria wastaarabu wakipanda Treni hiyo kupitia mlangoni kama wanavyoonekana hapo.



MANJI KUTOGOMBEA TENA UENYEKITI YANGA: YANGA YAPATA KATIBU MKUU MPYA

Mwenyekiti wa Young Africans Yusuf Manji leo amemtambulisha rasmi Bw. Beno Njovu kuwa katibu mkuu mpya wa klabu akichukua nafasi ya Lawrence Mwalusako aliyekua kaimu katibu mkuu kwa kipindi cha mwaka mmoja.
Akiongea na waandishi wa habari makao makuu ya klabu ya Yanga, Mwenyekiti wa Yanga Bw.Yusuf Manji amesema Beno Njovu anaanza kuitumikia hiyo nafasi mpya kuanzia leo na Mwalusako atakua nae pamoja kwa kipindi cha mwezi mmoja mpaka atakapokabidhi kazi rasmi.
Aidha Manji ametangaza mkutano mkuu wa wanachama Januari 19,2013 ambapo wanachama watapata fursa ya kupitia mapato na matumizi,  na ajenda zingine mbalimbali ambazo zitajadiliwa katika mkutano huo.
Kikao cha kamati ya utendaji kilichoketi mwishoni mwa wiki kimemteua Bw.Seif Ahmed "Magari" kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano ya Kimataifa na kutokana na nafasi hiyo pia ameteuliwa kuwa mjumbe wa Kamati Kuu ya Utendaji wa klabu ya Yanga. 
Katika mkutano na wandishi wa habari makao makuu ya klabu Manji ametangaza rasmi kutogombea tena uenyekiti katika uchanguzi mkuu ujao, hili nimeliamua mwenyewe binafsi bila shinikizo na kikubwa nimefuata demokrasia.
Nina miezi saba kabla ya uchanguzi mkuu mwakani hivyo sasa ninajitahid kukamlisha shughuli zote ambazo nilianza kuzifanya ndani ya Yanga nikiwa kama mwenyekiti ili uongozi mpya utakaoingia uweze kuendeleza mipango ya kuifanya Yanga iwe klabu bora Tanzania.


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU