Facebook Comments Box

Thursday, April 11, 2013

UINGEREZA KUANZA KUTUMIA TEKNOLOJIA YA GOLI WEMBLEY


.
.
Timu zinazoshiriki ligi kuu ya England zinatarajiwa kukubaliana kupitisha matumizi ya teknolojia  ya mstari wa Goli maarufu kama GOAL LINE TECHNOLOGY baadaye wiki hii ambapo taarifa toka kwenye chama cha soka cha England imesema kuwa klabu hizo zimezungumzia suala la matumizi ya teknolojia hiyo na zitakutana tena siku ya alhamis ambapo agenda kuu ya mkutano huo inatarajiwa kuwa makubaliano ya kupitisha matumizi ya teknoljia hiyo kwenye michezo ya ligi kuu ya England kuanzia msimu ujao.
.
.
Kampuni ambazo zimeingia kwenye mashindano ya kuwania tenda ya ufungaji wa teknolojia hiyo kwenye viwanja vya ligi kuu ya England ni Kampuni ya HawkEye,Cairos,Goalcontrol na Goalref ambapo teknolojia hiyo itaanza kutumika kwenye mchezo wa ufunguzi wa ligi kuu ya England ambao ni mchezo wa kuwania Ngao ya jamii unaochezwa kati ya mshindi wa ligi kuu na mshindi wa kombe la Fa, tayari shirikisho la mchezo wa soka ulimwenguni FIFA limepitisha matumizi  ya Goal line Technology ambapo teknolojia hiyo itaanza kutumika kwenye michuano ya kombe la mabara.
.
.
.
.
Chama cha soka cha England tayari kimepitisha matumizi ya teknolojia hiyo kwenye uwanja wake wa Taifa wa Wembley na kimeanza kupitia mapendekezo mbalimbali toka kwenye makampuni yanayofunga mifumo ya teknolojia hiyo.


MATOKEO YA MVUA KUBWA ILIYONYESHA LEO JIJINI DAR ES SALAAM




 Haya ni matokeo ya Mvua kubwa iliyonyesha leo Jijini Dar es Salaam na eneo lililoathirika zaidi ni Mikocheni kama inavyoonekana katika picha mbalimbali hapo juu. Eneo hili ni karibu kabisa na Hospitali ya TMK, Shoppers Plaza pamoja na Mayfair Plaza miaka yote kuna tatizo hili pindi mvua kubwa inapokuwa imenyesha.



MUDA WA KUBADILI LESENI ZA ZAMANI NA KUCHUKUWA MPYA UMEONGEZWA


Mwisho wa Kubadili leseni za madereva umeongezwa mpaka April 30, 2013 badala ya march 31, 2013 ya awali. Muda huo uliongezwa baada ya kikao ambacho Polisi walikaa pamoja na Mamlaka ya mapato kujadili kutokana na matatizo ambayo yalijitokeza na kusababisha madereva kushindwa kubadili leseni hizo kwa wakati. Moja ya sababu hizo ni Mtandao kuwa chini kwa muda mwingi.

Kamanda Mohamed Mpinga amesema muda huo wa mwezi mmoja ulioongezwa unatosha na hakutakuwa na muda mwingine tena na Dereva atakayeshindwa kubadili leseni ya zamani na kuchukuwa mpya atafikishwa mahakamani mara moja kujibu shitaka atakalo kuwa amepelekwa nalo la kushindwa kubadili leseni yake kwa wakati.

Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani – SACP. Mohammed R. Mpinga (kushoto) na Mr. Salum Yusuph - Naibu Kamishna wa Kodi za ndani TRA (kulia) wakisikiliza maswali mbalimbali kutoka kwa waandishi wa habari (pichani hawapo) kuhusu mwisho wa kubadili leseni za zamani za udereva utakao kuwa mwisho wa mwezi huu 30/04/2013.






ANGALIA JINSI LORI LILIVYOPONEA CHUPUCHUPU KUTUMBUKIA MTO WAMI



Lori ambalo chupuchupu kuzama kwenye mto Wami baada ya tela kukatika, utaratibu wa kulivuta ulitumia zaidi ya saa sita zilizofanya wasafiri kutoka pande zote mbili kusubiri. 


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU