Facebook Comments Box

Sunday, January 27, 2013

YANGA WAWAONESHA MAAFANDE WA PRISON SOKA SAFI LA KITURUKI

Jerry Tegete akichomoka kushangilia baada ya kuifungia Yanga bao la kwanza katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara dhidi ya TZ Prisons Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam jioni hii. Yanga ilishinda 3-1.

Na Mahmoud Zubeiry
YANGA SC imezidi kupaa kileleni mwa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, baada ya jioni hii kuitandika Prisons ya Mbeya mabao 3-1 katika mchezo wa ligi hiyo uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Kwa ushindi huo, Yanga imetimzia pointi 32 baada ya kucheza mechi 14, hivyo kuendelea kuongoza Ligi Kuu kwa wastani wa pointi tano, ikifuatiwa na Azam yenye pointi 27 na Simba 26.
Hadi mapumziko, timu hizo zilikuwa tayari zimefungana bao 1-1, Yanga wakitangulia kupata bao lao dakika ya 10 kabla ya Prisons kusawazisha dakika ya 17.
Bao la Yanga lilifungwa na Jerry Tegete aliyeunganisha krosi nzuri ya Simon Msuva kutoka wingi ya kulia, wakati la Prisons lilifungwa na Elias Maguri, aliyeunganisha krosi nzuri ya Misango Magai kutoka wingi ya kushoto.
Tegete akiigusa nembo ya Yanga baada ya kufunga la tatu.
Yanga walicheza vizuri dakika 15 za mwanzo na baada ya hapo, timu hizo zilianza kushambuliana kwa zamu, ingawa Watoto wa Jangwani ndio waliopoteza nafasi nzuri zaidi za kufunga.
Kipindi cha pili, Yanga walirudi na kasi nzuri kusaka ushindi na iliwachukua dakika 11 tu kupata bao la pili, lililofungwa na Mbutu Twite baada ya kutokea piga nikupige langoni mwa Prisons.
Wakati Prisons wakiwa kwenye jithada za kusaka bao la kusawazisha, walijikuta wakitandikwa bao la tatu, Tegete tena akiwainua vitini mashabiki wa Yanga, baada ya kupokea pasi nzuri ya Nurdin Bakari dakika ya 65.
Baada ya bao hilo, Yanga walianza kuonyesha vitu vya Uturuki walipoweka kambi ya wiki mbili kabla ya kuanza kwa mzunguko huu wa pili wa Ligi Kuu, wakicheza soka ya madoido pasi nyingi, uzungu na kila aina ya mbwembwe, ili mradi tu kuwaburudisha mashabiki wake.
Mapema kabla ya mchezo huo, kiungo wa Yanga, Frank Domayo alipatwa na Malaria ya ghafla na kuenguliwa kwenye kikosi cha kwanza na nafasi yake akaanza Nurdin Bakari, wakati mshambuliaji mpya wa Prisons, Emmanuel Gabriel alienguliwa kwenye kikosi cha kwanza na nafasi yake akachukua Elias Maguri, kwa sababu ya kutokuwa na leseni ya TFF ya kumruhusu kucheza Ligi Kuu. Suala la leseni ya Gabriel, dhahiri ni uzembe wa viongozi wa Prisons.
Katika mchezo wa leo, 
kikosi cha Yanga SC kilikuwa; Ally Mustafa ‘Barthez’, Mbuyu Twite/Juma Abdul dk 82, Oscar Joshua, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Kevin Yondan, Athumani Iddi ‘Chuji’, Simon Msuva, Nurdin Bakari/David Luhende dk 66, Didier Kavumbangu/Hamisi Kiiza dk 64, Jerry Tegete na Haruna Niyonzima.

TZ Prisons; David Abdallah, Aziz Sibo, Henry Mwalugala, Lugano Mwangama, Jumanne Elfadhil, Nurdin Issa, Sino Augustino, Freddy Chudu, Elias Maguri, Misango Magai/John Matei dk58 na Jeremiah Juma. 

Kiungo wa Yanga, Frank Domayo akiwa amelala katika zahanati ya Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam mida hii, baada ya kupatwa na Malaria ya ghafla. Domayo ilikuwa aanze mechi ya leo, lakini kutokana na kuugua huko ghafla, sasa nafasi yake ataanza Nurdin Bakari.

Kiungo wa Yanga, Frank Domayo akiwa amelala katika zahanati ya Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam mida hii, baada ya kupatwa na Malaria ya ghafla. Domayo ilikuwa aanze mechi ya leo, lakini kutokana na kuugua huko ghafla, sasa nafasi yake ataanza Nurdin Bakari.



UJUMBE WA SEKRETARIETI YA CCM WAWASILI SALAMA MKOANI KIGOMA LEO


 Wananchi wa Mkoa wa Kigoma leo wameupokea kwa shangwe Ujumbe wa Sekretarieti ya Chama cha Mapinduzi (CCM) uliowasili mkoani Kigoma ukitokea jijini Dar es Salaam kwa kutumia usafiri wa Treni Reli ya Kati.
Wajumbe hao ambao wanaoongozwa na Katibu Mkuu wa Chama hicho,Ndg. Abdulrahman Kinana ni pamoja na Katibu wa NEC,Itikadi na Uenezi,Nape Nnauye,Katibu NEC,Siasa na Mahusiano ya Kimataifa,Dkt. Asha-Rose Migiro na Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana CCM,Martin Shigela.
Akizungumza baada ya kuwasili Mkoani Kigoma leo, Katibu Mkuu wa CCM,Ndg. Abdulrahman Kinana alisema kuwa lengo la wao kutumia usafari huo wa Treni ni kuwadhihirishia wananchi wa Tanzania kuwa Usafiri wa Treni ni Usafiri wa uhakika na Serikali ya Chama cha Mapinduzi kupitia Wizara ya Uchukuzi, itasimamia kikamilifu usafiri huo na kuendelea kuuboresha zaidi ya ilivyo sasa na kuhakikisha safari zinaongezeka na kuwa za kila siku na si kuwa kwa wiki mara mili kama ilivyo sasa.Nao baadhi ya wakazi wa Mkoa wa Kigoma wameipongeza sana Sekretarieti hiyo kwa uamuzi wao wa kusafiri kwa kutumia Treni kutoka jijini Dar es Salaam hadi Mkoani Kigoma na kujionea hali halisi ya usafiri huo.
Ujumbe huo upo Mkoani Kigoma kwa ajili ya maadhimisho ya miaka 36 ya Chama Cha Mapinduzi.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndg. Abdulrahman Kinana akisalimiana na wanachama pamoja na wananchi wa mji wa Itigi mkoani Singida wakati Treni iliposimama kwa muda mfupi katika mji huo.


Wananchi wa Mkoa wa. kwa ajili ya maadhimisho ya miaka 36 ya Chama Cha Mapinduzi.


Wananchi wa Mkoa wa Kigoma wakiwa wamekusanyika kumsikiliza Katibu Mkuu wa CCM wakati akizungumza nao.

Wananchi wa Mkoa wa Kigoma wakielekea kuupokea Ujumbe wa Sekretarieti ya CCM wakati ukiwasili Mjini Kigoma leo.

Katibu Mkuu wa CCM,Ndg. Abdulrahman Kinana akisalimiana na wananchi wa Mji wa Kigoma waliofika kuupokea Ujumbe wa Sekretarieti ya CCM uliowasili mjini Kigoma leo kutokea jijini Dar es Salaam kwa usafiri wa Treni ya Reli ya kati.



Katibu wa NEC, Siasa na Mahusiano ya Kimataifa (CCM),Dkt. Asha-Rose Migiro akisalimiana na wananchi wa Mji wa Kigoma waliofika kuupokea Ujumbe wa Sekretarieti ya CCM uliowasili mjini Kigoma leo kutokea jijini Dar es Salaam kwa usafiri wa Treni ya Reli ya kati.


Katibu Mkuu wa CCM,Ndg. Abdulrahman Kinana akifurahia ngoma ya utamaduni ya mkoa wa Kigoma iliyokuwa ikipigwa Stesheni leo,huku Katibu wa NEC,Itikadi na Uenezi,Nape Nnauye akipiga moja ya ngoma hizo.

Katibu Mkuu wa CCM,Ndg. Abdulrahman Kinana (kulia) akipena mkono na Dereva wa Treni ya TRL,Bw. Kambi Ali (wa pili kulia) aliyewasafirisha kutoka Jijini Dar es Salaam mpaka Mjini Kigoma salama. Wengine pichani ni Katibu wa NEC, Siasa na Mahusiano ya Kimataifa (CCM),Dkt. Asha-Rose Migiro pamoja na Katibu wa NEC,Itikadi na Uenezi (CCM), Nape Nnauye.




MKAZI WA TANDIKA APIGWA RISASI KISA DENI LA TSH 100

 
Picture
MKAZI wa mtaa wa Tandika, Frank Filias (25) akiwa amelazwa katika hospitali ya wilaya Temeke wodi namba saba baada ya kupigiwa risasi na mfanyabiashara mmoja wa mbao kufuatia ugomvi wa kudaiana Shilingi ya Kitanzania 100 ya maji ambayo mama yake mzazi, Sarah Mwaikatale alidaiwa na jirani yake kuwa alishindwa kumlipa (Picha: Christopher Nyenyembe via Habari Mseto blog )



TAARIFA MPYA KUTOKA KUSINI: WALIOFARIKI WAFIKA 9, VIONGOZI WAWASILI

IDADI ya watu waliouawa katika vurugu za wilaya ya Masasi,mkoani Mtwara imeongezeka na kufikia Tisa kutoka saba walioripotiwa awali. Mmoja aliyekuwa majeruhi na kulazwa hospitali ya misheni ya Ndanda ameripotiwa kupoteza maisha yake. Ndugu wa karibu wa marehemu amemthibitishia mwandishi wa kuwa ndugu yao amefariki leo saa 9 usiku akiwa anapatiwa matibabu hospitalini.
 Mchana wa leo, mwendesha bodaboda mmoja ameuawa kwa kupigwa na vitu vinavyosadikika kuwa ni risasi za moto na kupoteza maisha papo hapo. Wananchi wamedai polisi wakiwa katika gari walimminia risasi kijana huyo aliyekuwa anaendesha pikipiki yake. Haya ni mauaji ya kwanza kutokea kwa polisi kuua watu wengi kwa risasi za moto, hali inayoitia doa Serikali. Tayari Waziri wa Mambo ya Ndani, Emanuel Nchimbi amewasili mkoani Mtwara akiambatana na Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP, Saidi Mwema, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi (JWTZ) Davis Mwamunyange. Habari zinasema kuwa viongozi hao watafaya kikao na viongozi wa Mtwara na badaye kwenda Masasi kushuhudia hali ilivyo. Hata hivyo kuna habari kuwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda atawasili kesho mjini Mtwara, kufuatia vurugu zinazoendelea ambazo zinachagizwa na kupinga gesi kupelekwa Dar es Salaam. 

MADIWANI KIGAMBONI: HAIWEZEKANI KUTUONDOA TEMEKE BILA UTARATIBU WA KISHERIA

  Tangazo la Serikali kulichukua eneo lote la Kigamboni na kuliondoa chini ya mamlaka ya Manispaa ya Temeke, limezua tafrani baada ya madiwani kutaka kuitisha kikao maalum cha kupinga hatua hiyo na tayari wameanza kukusanya saini za madiwani wanaofikia akidi ili kiitishwe kikao walichokiita kuinusuru Temeke. Tayari nusu ya kura imepatikana.

Hivi karibuni Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka alitangaza kulitwaa eneo la Kigamboni na kuongeza ukubwa wa eneo kwa kuchukua kata nyingine kwa ajili ya uanzishwaji wa jiji la kisasa la Kigamboni. Pia, alitangaza kuanzishwa kwa chombo cha Wakala wa Kuendeleza Mji wa Kigamboni (KDA) ambapo hatua hiyo inaiondoa kutoka Manispaa ya Temeke kiutawala.

Madiwani hasa kutoka Kigamboni wamesema kitendo cha Serikali kuwaondoa kibabe bila kuwashirikisha kimezidisha hofu kwa wananchi wa eneo hilo ambao tangu mradi huo uanze kuandaliwa, wamerudishwa nyuma kimaendeleo.
Tumeshtushwa sana na kauli ya waziri Profesa Tibaijuka, ni hatua ya kibabe iliyochukuliwa bila kutushirikisha sisi madiwani, haiwezekani kutuondoa manispaa ya Temeke bila kufuata utaratibu wa kisheria.
Alisema inashangaza pia kuwa Serikali imeongeza kata nyingine nne --Kisarawe 11, Kimbiji, Somangila na Pembamnazi -- na kuziingiza kwenye mradi bila kutoa taarifa kwa wananchi ili waweze kujadili na kutoa maoni yao. Kata zilizokuwa awali ni Kigamboni, Tungi, Kibada, Mjimwema na Vijibweni.
Tutalazimika kukutana haraka kuona jinsi gani tutaijibu serikali kwa maamuzi yake haya ya ukandamizaji, sisi ni wawakilishi wa wananchi kwa nini wanafanya mambo yao kwa usiri mkubwa na kisha kutupa taarifa kama vile huku hakuna mamlaka inayokubalika.
via gazeti la NIPASHE.



MAASKOFU WA MAKANISA YA PCT MTWARA WATOA TAMKO KUUNGA MKONO WANANCHI WA MTWARA

Baada ya kufuatilia kwa undani, na kwa upana kuhusu swala la gesi ambalo linaendelea kuwa ni mgongano au, ni mgogoro kati ya Serikali na wananchi wa Mkoa wa Mtwara/Lindi kuhusu ujenzi wa bomba la kusafirisha gesi kwenda kinyerezi Dar- es–Salaam, tumebaini yafuatayo:-
 1. Hakuna Sera ya gesi ambayo husababisha kupatikana Sheria baada ya kupelekwa Bungeni na kuidhinishwa bali kilichopo ni rasimu ya sera ambayo haina ushirikishwaji wa mawazo ya wananchi wa Mkoa wa Mtwara na Lindi, ambako vyanzo vya gesi hiyo ipo. 
2. Elimu kuhusu gesi na manufaa yake kwa wananchi haikutolewa ili kujua haki zao kwa madhara yatokanayo na (Uvunaji) uzalishaji wa gesi hiyo, na jinsi watakavyonufaika. Chama cha Mapinduzi katika Ilani yake ya uchaguzi ya mwaka 2010 inatamka wazi katika Ibara ya 63 kifungu cha H na K juu ya gesi ya Mnazibay Mtwara na Songo songo Kilwa, Lindi kuhusu umeme wa (240 MW) Kinyerezi na (300MW) Umeme wa Mnazi bay Mtwara. -Vifungu hivi vinafafanua: • Gesi ya Mnazi bay itakuwa kwa ajili ya Mitambo ya kuzalisha umeme ambayo itajengwa Mtwara (300MW) • Mitambo ya kuchakata gesi kujengwa Mtwara • Ujenzi wa viwanda Mtwara ili malighafi itokanayo na gesi itumike kutengeneza mbolea, plastic vikiwemo na viwanda vya Cementi 3. Gesi ya Songo songo inafafanua wazi kuwa gesi hiyo itapelekwa Kinyerezi . Dar –es –Salaam kwa madhumuni hayo hayo. • Kuendeleza viwanda mbali mbali • Kuzalisha umeme (240 MW) • Kuchakata gesi kwa kujenga mitambo Katika ahadi ya Rais wa Jahuri ya Muungano wa Tanzania alizotoa wakati wa Kampeni za uchaguzi katika hotuba yake ya tarehe 29/10/2010 alitamka wazi kuwa Mkoa wa Mtwara uwe tayari kwa maendeleo makubwa ambayo yanakuja kutokana na gesi iliyogunduliwa katika Mkoa wa Mtwara huko Mnazi bay Alimainisha/aliainisha juu ya viwanda mbalimbali vitakavyojengwa hapa mkoani vya mbolea,cement, plastic n.k na kuwataka wananchi wajiandae kupokea maendeleo hayo kwa kujenga nyumba nzuri zenye sifa kwa ajili ya wageni. Pia wawasomeshe watoto wao ili wawe na elimu ya juu na kupata ajira katika Makampuni yanayokuja. Hata baada ya uchaguzi Rais wetu alipokuja kuwashukuru wananchi wa Mkoa wa Mtwara kwa kumchagua, alitamka tena katika hotuba yake akisisitiza ahadi yake ya kujenga viwanda ambavyo vitaleta maendeleo kwa Mikoa ya Kusini na kusababisha ajira kwa wana kusini, na kuagiza kwa Meya wa Manispaa Mtwara/Mikindani kuwapa maeneo ya kujenga viwanda hivyo, kwa kile kilichoonekana kukosa maeneo ya ujenzi huo kwa makampuni hayo. Ahadi hizi alizozitoa kwa wananchi kwa ujumla wao wamezipokea na kuendelea kuzifanyia kazi. Chanzo cha Matatizo: Mara baada ya kuonekana kile walichokitarajia wananchi wa Mkoa wa Mtwara kwa kutumia gesi ya Mnazi bay kuleta maendeleo yao kuwa imeamriwa kusafirishwa kwa bomba na kupelekwa Kinyerezi Dar –Es –Salaam ili kuzalisha umeme na kuchakata gesi na mitambo hiyo iwe huko.(Mgeuko wa Ilani ya Uchaguzi, na kutozingatia ahadi zake mwenyewe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwa kinyume na kauli za usemi wake mwenyewe kwa kukitangaza kituo cha Kinyerezi kuwa ni sehemu ya mitambo ya gesi ya Mnazi bay-Mtwara na Songosongo-Lindi na kwamba bomba hilo litachukua miezi (18) mpaka kukamilika kwake, kwa matamshi haya ndiyo yaliyoleta hasira na chuki kwa wananchi wa Mtwara/Lindi kwa ujumla. Hali hii imewafanya wananchi wa Kusini kutokuwa na Imani na Serikali na viongozi wake wahusika na sakata hili la gesi kwa semi mbalimbali za viongozi hawa
-Mfano. (1) Kwa hali yoyote gesi lazima itoke Mtwara (Kwa gharama yoyote ile) kwa kukubali ama kutokubali itakwenda Kinyerezi kwa bomba 
         (2) Kuitwa wahaini wananchi wa Mkoa wa Mtwara kwa kuandamana 
             (3) Kuitwa wajinga, hawakusoma na kuwa watu wa vijiweni wasio na elimu ya gesi
     (4) Nitafanya lolote hata kama nitalaumika na Mataifa mengine lakini wapo watakaochekea yatakayotokea na kauli zinazobadilika kila kunapokucha.
      (5) Usemi wa kuigawa nchi vipande vipande Viongozi hawa hawajui kuwa chanzo kipo kwao wenyewe, kwa kutozingatia kuwa wananchi hao ambao hawana elimu kama yao wanao upeo mkubwa wa kufikiri na kutoa maamuzi kama wanavyotoa wao….
 Mfano. (1) Gesi haitoki Mtwara
             (2) Tupo tayari kufa wote kwa ajili ya gesi 
         (3) Haiwezekan mitambo ya aina zote -Kufua umeme -Kuchakata gesi -Kunufaisha viwanda vya Dar-es-Salaam kwa gesi yetu -Mikataba ya gesi ya Mnazibay kufutwa ili kuanzisha mikataba iliyo na manufaa kwa Mkoa wa Mtwara na wananchi wake. 
          (4) Kwa nini bomba la gesi kujengwa kwa muda wa miezi 18 na bara bara kwa miaka 51 ya uhuru haimalizwi kujengwa. Je kwenye gesi kuna nini nyuma yake.? Hiki ni kiini cha matatizo yote kwa wananchi wa mkoa wa Mtwara kuandamana na mikutano mbalimbali ya kuhamasisha kutokubali gesi kuondoka Mtwara Nukuu za Wananchi wa Mkoa wa Mtwara/Lindi 
1-Kung’olewa kwa Reli 
2-Kung’olewa kwa mashine za maji Newala na kupelekwa Dodoma. 
3-Kung’olewa kwa taa za kuongoza ndege uwanja wa Mtwara na kupelekwa Uwanja wa KIA Moshi 4-Kuondolewa kwa Mtwara Korido 
5-Kuwekezwa kwa bandari ya Mtwara kwa muda usiojulikana inaonyesha jinsi Serikali na viongozi wake wanavyohujumu Mikoa ya Kusini na wananchi wake kwa ujumla. -Wananchi wa Mkoa wa Mtwara na Lindi wamefikia ukomo sasa wa kutengwa kimaendeleo, kimazingira na kutendewa uonevu wa makusudi na kilio chao cha mwisho ni hiyo gesi ambayo kauli mbiu yao ni GESI HAITOKI MTWARA KWA BOMBA KWENDA KINYEREZI DAR-ES-SALAAM
. -Wananchi wote wameungana juu ya kuitetea gesi kutoka Mtwara, badala yake Serikali ifuate mikataba ya kwanza inayohusu gesi ya Mtwara pamoja na Ilani ya uchaguzi ya CCM ifuatwe na Rais atekeleze ahadi zote alizotoa hapo kwanza na afute kauli yake ya kupeleka gesi Kinyerezi, na wala Serikali isitumie nguvu katika swala zima la gesi ya Mnazibay Mtwara.

 TAMKO LA UMOJA WA MAKANISA YA KIPENTEKOSTE –P.C.T MKOA WA MTWARA P.C.T 

kwa kuzingatia mwono uliopo wa hali tete yenye mwelekeo wa kumwagika damu na kuigawa nchi vipande vipande na kuondokewa amani, yafuatayo yafanyike • Serikali isitishe mpango wake wa kuondoa gesi kutoka Mnazi bay Mtwara kwa kuisafirisha kwenda Kinyerezi Dar –es Salaam kwa bomba. • Mitambo ya kuchakata gesi ijengwe Mtwara ili gesi isafirishwe kama mazao ya gesi na mabaki yake kutumiwa katika viwanda vya mbolea na plastic. • Mitambo ya kuzalisha umeme ijengwe Mtwara na kusafirisha umeme na kuunganisha gridi ya Taifa. • Viwanda vilivyoahidiwa vya mbolea,plastic,cemet n.k vianze kujengwa sasa na isiwe propaganda tu ya kisiasa toka kwa viongozi kwa kuondoa dhana iliyotokea huko nyuma ya kuonekana Kusini ni ukanda wa vita usiendelezwe. Mfano kule Kilwa Lindi ambako ahadi ya kujenga kiwanda cha mbolea kwa gesi ya Songo songo mpaka leo hakijajengwa kwa kuwapatia nafasi ya ajira na kujiajiri kutokana na viwanda hivyo • Serikali iwe sikivu kwa kilio cha muda mrefu cha wananchi wa Mikoa ya Mtwara na Lindi ambako vyanzo vya uchumi wa gesi vipo kwa kutekeleza madai yao, kwa kuwa hawapingi kupelekwa umeme gridi ya Taifa na kuuza gesi iliyochakatwa tayari kwa kuliingizia Taifa mapato. • Serikali ikamilishe sera za gesi na mafuta na kupatikana sheria ambayo italinda mikataba yote inayofanywa na serikali juu ya gesi na kulinda wananchi wa eneo husika mikoa ya Mtwara na Lindi kwa madhara yanayotokana na gesi kwa kuwashirikisha kutoa mawazo yao. • Mazungumzo yafanyike kati ya Serikali na wananchi katika kupata ufumbuzi wa swala la gesi kwa njia ya Amani na wala isitumie nguvu zilizonazo kwani kufanya hivyo ni kuleta maafa yasiyo ya lazima kwa Taifa. • -Serikali isisikilize wabunge wadanganyifu ambao hawana makubaliano na wananchi katika majimbo yao wanayotoka, ambao huchochea mgogoro huu kwa lengo lao binafsi. • Viongozi ambao wametoa matusi kwa wananchi wafute usemi wao kwa wananchi wa Mkoa wa Mtwara ambao wamewaita wahaini kwa kuwaomba radhi bila masharti yeyote kwani semi hizo huleta chuki, uhasama, na matengano katika nchi, na kusababisha nchi isitawalike. • Serikali ya Chama Cha Mapinduzi itekeleze Ilani ya Uchaguzi ya Mwaka 2010 Ibara 63 Kifungu H na K ambavyo vipo wazi, hasa kwa kuzingatia kuwa sera zinazotekelezwa sasa na Serikali ni zile zote zilizoandikwa kwenye Ilani ya uchaguzi. • Serikali irudishe tumaini kwa wananchi wa Mikoa ya Kusini na amani inayoonekana kutoweka kwa matamshi yanayoashiria kumwagika kwa damu bila kujali kuwa nchi ilipatikana bila kuwaga damu. • Serikali iwatambue wananchi wa Mikoa ya Kusini kuwa wana haki ya kutimiziwa matakwa yao kama wananchi wa mikoa mingine kwa kupata maendeleo kutokana na vyanzo vya uchumi vilivyopo katika maeneo yao. -Sisi viongozi wa dini tunamwomba Mungu awape hekima viongozi wetu wa Serikali kwa sababu wamepewa dhamana na Mungu kuliongoza Taifa.
-Ukamilifu wao wenye haki utawaongoza, bali ukaidi wao wenye fitina utawaangamiza Methali 11:3 -Asiyemcha Mungu humpoteza jirani yake kwa kinywa chake, bali wenye haki watapona kwa maarifa. Methali 11:9
 Imesainiwa na BISHOP C. CHILUMBA MWENYEKITI MKOA PAMOJA
                  NA:- PASTOR SELEKWA KATIBU PCT- MKOA WA MTWARA

 Nakala: • Mwenyekiti PCT Taifa-Dar –es –Salaam
             • Maaskofu na Wachungaji wote wa PCT Mkoa wa Mtwara. 


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU