Facebook Comments Box

Friday, September 13, 2013

HILI NDIO TUKIO JINGINE LA MTU KUMWAGIWA TINDIKALI LEO UNGUJA

Ikiripotiwa ni Padri wa kanisa katoliki cheju amemwagiwa tindikali leo. 


MAHAKAMA NCHINI INDIA YAWA HUKUMU KIFO WABAKAJI WANNE

Mahakama nchini India imewahukumu wanaume wote wanne kifo baada ya kupatikana na hatia ya kumbaka na kumuua mwanamke katika basi katika mji mkuu wa India Delhi mwezi Desemba mwaka jana.
Mmoja wao aliangua kilio na kuanguka baada ya kutangazwa kwa hukumu dhidi yao .
Taarifa zinazohusiana
afya
Msichana huyo aliyekuwa na umri wa miaka 23 aliumizwa sana na baada ya wiki moja alifariki kutokana na majeraha .
Karibu miezi 9 baada ya ubakaji ulioitikisa India, jaji ametoa hukumu kwa wanaume wote wanne ambao tayari walikuwa wamepatikana na hatia ya uhalifu .
Wendesha mashtaka walikuwa wamewaombea hukumu ya kifo wakisema ingetoa ishara muhimu kwamba uhalifu wa aina hiyo hautakubalika kamwe .
Familia ya mwanamke huyo pia waliomba wanaume hao wanyongwe .
Lakini mawakili watetezi wa wanaume hao walipinga mapendekezo ya hukumu ya kifo , wakisema wateja wao hawakuwa na rekodi za uhalifu awali na kwamba wanastahili kusamehewa .
Kifo cha mwanafunzi huyo mwezi Disemba mwaka jana kilisababisha maandamano makubwa ya upinzani kote nchini India , yaliyoilazimisha serikali kubadili sheria zilizokuwepo za uhalifu wa ngono



 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU