Facebook Comments Box

Saturday, January 19, 2013

ANGALIA REAL SOCIEDAD ILIPO IPA KICHAPO BARCELONA LEO




BIFU LA SINTAH NA RAYUU: HAYA NDIO MANENO MAZITO WALIOTUPIANA


Ikisemekana bifu hilo lilianza baada ya Sintah kumuandika vibaya Rayuu katika mtandao wake kama inavyoonekana hapo juu
Baada ya maneno hayo ndio ikamlazimu Rayuu nae kujibu maneno hayo katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa facebook



SAEED KUBENEA KUGOMBEA UBUNGE 2015

Mwandishi wa habari wa gazeti la Mwanahalisi Saed Kubenea, inasemekana amejipanga kugombea Ubunge Jimbo la Kibaha Mjini kupitia CHADEMA mwaka 2015. kwa hivi sasa Jimbo hilo linaongozwa na Silvestry Koka [CCM].
Saeed Kubenea ameshauriwa na Dr Slaa agombee ubunge na CHADEMA itampa sapoti katika hilo na amemuhakikishia kuwa atashinda


KAMATI YA UCHAGUZI YA TFF YA AHIRISHA UCHAGUZI


UCHAGUZI WA VIONGOZI TAFCA WAAHIRISHWA 

Kamati ya Uchaguzi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imeahirisha uchaguzi wa Chama cha Makocha wa Mpira wa Miguu Tanzania (TAFCA) uliokuwa ufanyike leo (Januari 19 mwaka huu) jijini Dar es Salaam.
Uchaguzi umeahirishwa kwa vile ulitaka kufanyika bila kuzingatia Katiba ya TAFCA Ibara ya 32(1) na Kanuni za Uchaguzi za Wanachama wa TFF Ibara ya 10(6) na 26(2), hivyo Kamati ya Uchaguzi ya TFF imeahirisha uchaguzi huo kwa vile nafasi zilizoombwa kugombewa na idadi ya waombaji uongozi haikidhi matakwa ya Katiba ya TAFCA.
Pia taratibu za kikanuni ikiwa ni pamoja na kuwaarifu waombaji uongozi ambao hawakukidhi matakwa ya Katiba ya TAFCA hazikukamilika kwa mujibu wa Kanuni za Uchaguzi za Wanachama wa TFF.
Licha ya upungufu huo, TAFCA haikuwasilisha taarifa za mchakato mzima kama ilivyoombwa na TFF. Kamati ya Uchaguzi ya TFF imeiagiza Kamati ya Uchaguzi ya TAFCA kuandaa uchaguzi mpya utakaokidhi matakwa ya Kamati ya TAFCA baada ya Uchaguzi Mkuu wa TFF.
TFF inaishauri TAFCA kutumia fursa ya Mkutano Mkuu wa leo (Januari 19 mwaka huu) kujadili mustakabali wa TAFCA kwa kuwa chama hicho kimeshindwa mara mbili kupata idadi ya wagombea wanaokidhi akidi ya Kamati ya Utendaji.
Pia TAFCA haijawahi kufanya mikutano ya Kamati ya Utendaji na Mkutano Mkuu kwa karibu miaka minne.
Boniface Wambura

Ofisa Habari

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

HII NDIO YANGA BWANA - HIVI NDIVYO ILIVYOWATANDIKA WASAUZI TAIFA LEO

 Didier Kavumbagu (kushoto) akijaribu kumtoka beki wa Black Leopards, wakati wa Mchezo huo, uliomalizika hivi punde kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Wachezaji wa Yanga, wakishangilia bao lililofungwa na Jerry Tegete.
jj
 Kikosi cha Yanga.
 Kikosi cha Black Leopards.
 Mchezaji wa Yanga, Kabange Twite (kushoto) akimiliki mpira huku akidhibitiwa na beki wa Black Leopards, Nkosiabo Xakane, wakati wa mchezo huo.
Mashabiki wa Yanga, wakishangilia bao lililofungwa na Jerry Tegete. (PICHA NA SUFIANI MAFOTO)


SIMBA YACHEZEA KICHAPO CHA 3 KWA 1

 Mabingwa wa soka Tanzania Bara,Simba wameshindwa kutamba mbele ya Wenyeji wao mara baada ya kufungwa mabao 3-1 katika mechi ya kirafiki dhidi ya timu ya Taifa ya Jeshi la Oman. mechi hiyo ilichezwa Ijumaa jioni kwenye uwanja wa Qaboos Complex jijini Muscat.
bao la simba lilifungwa katika kipindi cha pili na Haruna Moshi 'Boban' huku Mwenyekiti wa Simba,Ismail Aden Rage akiwa jukwaani pamoja na viongozi wengine wa simba, Rahma Al Kharoos na Musleh Rawahi pamoja na Kocha Talib Hilal wakiishuhudia Simba ikizama mbele ya wanajeshi hao

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjlRCm9tsdl0GuqK8TLbE1shCvEZJgJ5ZlH_m5XkhR1hTThltEl1Xt8bq8XcTQF75XYFCL6no8X9TueY_JkNVtYjykqNT-6pBUZ_PX-fKmeb_-wQHsscSKl5YQpRPaAvlNjUKfcBaSRVcQ/s1600/rAGE.JPGMwenyekiti wa Simba na Mfadhili wa safari ya Simba Rahma Al Kharoos akiangalia timu ya Simba ikipokea kichapo

TRA,,TUME YA UCHAGUZI NA JUMUIYA YA SERIKALI ZA MITAA (ALAT) WATOA MAONI YA KATIBA MPYA





 Mwenyekiti wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT) na Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Dk. Didas Masaburi akiwasilisha maoni ya Jumuiya hiyo kuhusu Katiba Mpya kwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba jijini Dar es Salaam Ijumaa, jan 18, 2013. Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa Tume Jaji Mkuu Mstaafu Augustino Ramadhani.

Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Bw. Ally saleh akiongea katika mkutano na Uongozi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) uliokutana na Tume kuwasilisha maoni yake kuhusu Katiba Mpya  katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam.


https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiqMBipiZ6xuBIr7S_HqKfhWiuqiFBoed3IEs9XBug6QoRugraXDI0Az5Ds1eGNQSGepfRtK37-qqZr9CU1TXRs9ua0wUX1VMSfErSIKhDoA3xD8p-04w6K9UDnSz8lIPc8OzlqnwMu59Q/s1600/CRC-TRA+Jaji+Warioba+na+Viongozi+wa+TRA.jpg
Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Harry Kitillya (mwenye tai nyekundu) akiongea na Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Jaji Joseph Warioba mara baada ya Mamlaka hiyo kuwasilisha maoni yake kuhusu Katiba Mpya kwa Tume katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam.

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjd_pJBymQJ4i5jeCDYb62zhaA8NubxDoPSA2TSdrA9lKa6fWm3PMmw8CVwFlBK22h8TYtK3O0_l2A54dSMrmWFnP0-F0hJaKzK9VrmQoUslqkyipIyydYZhjKBPPvWqxr7lAvVuT40p2s/s1600/CRC-TRA+Picha+ya+pamoja.jpg

 Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba wakiongozwa na Mwenyekiti wake Jaji Joseph Warioba (wa sita kutoka kushoto) katika picha ya pamoja na Viongozi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) waliongozwa na Mwenyekiti wa Bodiu ya TRA Bw. Bernard Mchomvu (wa nne kutoka kushoto) mara baada ya Mamlaka hiyo kuwasilisha maoni yake kuhusu Katiba Mpya jijini Dar es Salaam.



 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU