UPANDE wa Jamhuri katika kesi ya uchochezi na wizi wa malighafi ya Sh. 
milioni 59 inayomkabili Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislam, Sheikh 
Ponda Issa Ponda na wenzake 49 wameiomba  Mahakama ya Hakimu Mkazi 
Kisutu Dar es Salaam imuone Ponda na wenzake wanakesi ya kujibu kwa 
sababu umeweza kujenga kesi yao.
Kesi hiyo ilikuja kwa ajili ya 
upande wa Jamhuri unaowakilishwa na wakili Mwandamizi wa Serikali 
Tumaini Kweka na Inspekta wa Polisi,  Hamisi Said na upande wa utetezi 
unaowakilishwa na Juma Nassor na Njama kuwasilisha majumuisho yao kwa 
njia ya mdomo ya kuomba mahakama iwaone washitakiwa wanakesi ya kujibu 
au la.
Kweka ambaye alitumia dakika kumi tu kuwasilisha 
majumuisho alidai upande wa Jamhuri umeweza kujenga kesi yake kupitia 
mashahidi wake 16 na vielelezo 13 walivyovileta mahakamani ambapo 
waamini kisheria vitawafanya washitakiwa wapande kizimbani kujitetea.
Wakili
 wa utetezi Nassor Juma akiwasilisha majumuisho yake, aliomba mahakama 
iwaone washitakiwa hawana kesi ya kujibu na waachiliwe huru kwa sababu 
upande wa Jamhuri umeshindwa kujenga kesi yao.
Nassor alidai 
wanachokiona katika kesi hiyo ni kuwa kuna mgogoro wa ardhi ambao 
ulitakiwa ukatatuliwa kwanza na Mahakama ya Ardhi kwa mujibu wa kifungu 
cha 167 cha Sheria ya Ardhi Na.4 ya mwaka 1999, “Sisi upande wa utetezi 
tunaiomba mahakama hii iwaachilie huru washitakiwa wote na iwaone hawana
 kesi ya kujibu kwas ababu kesi hii imefunguliwa kwa jazba na polisi na 
upande wa Jamhuri umeshindwa kuleta ushahidi ambao utaweza kuishawishi 
Mahakama iwaone washitakiwa wote wana kesi ya kujibu,” alidai wakili 
Nassor.
Hakimu Nongwa aliarisha kesi hiyo hadi Machi 4 mwaka huu,
 ambapo atakuja kutoa uamuzi wa ama kuwaona washitakiwa wana kesi ya 
kujibu au la na kuamuru Ponda na Mkadamu warudishwe rumande kwa sababu 
bado Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP), Dk Eliezer Feleshi hajaondoa hati 
yake ya kuwafungia dhamana.
Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
