Facebook Comments Box

Thursday, February 28, 2013

WAKILI: MAHAKAMA IMUONE PONDA HANA KESI YA KUJIBU



UPANDE wa Jamhuri katika kesi ya uchochezi na wizi wa malighafi ya Sh. milioni 59 inayomkabili Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislam, Sheikh Ponda Issa Ponda na wenzake 49 wameiomba  Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam imuone Ponda na wenzake wanakesi ya kujibu kwa sababu umeweza kujenga kesi yao.

Kesi hiyo ilikuja kwa ajili ya upande wa Jamhuri unaowakilishwa na wakili Mwandamizi wa Serikali Tumaini Kweka na Inspekta wa Polisi,  Hamisi Said na upande wa utetezi unaowakilishwa na Juma Nassor na Njama kuwasilisha majumuisho yao kwa njia ya mdomo ya kuomba mahakama iwaone washitakiwa wanakesi ya kujibu au la.

Kweka ambaye alitumia dakika kumi tu kuwasilisha majumuisho alidai upande wa Jamhuri umeweza kujenga kesi yake kupitia mashahidi wake 16 na vielelezo 13 walivyovileta mahakamani ambapo waamini kisheria vitawafanya washitakiwa wapande kizimbani kujitetea.

Wakili wa utetezi Nassor Juma akiwasilisha majumuisho yake, aliomba mahakama iwaone washitakiwa hawana kesi ya kujibu na waachiliwe huru kwa sababu upande wa Jamhuri umeshindwa kujenga kesi yao.

Nassor alidai wanachokiona katika kesi hiyo ni kuwa kuna mgogoro wa ardhi ambao ulitakiwa ukatatuliwa kwanza na Mahakama ya Ardhi kwa mujibu wa kifungu cha 167 cha Sheria ya Ardhi Na.4 ya mwaka 1999, “Sisi upande wa utetezi tunaiomba mahakama hii iwaachilie huru washitakiwa wote na iwaone hawana kesi ya kujibu kwas ababu kesi hii imefunguliwa kwa jazba na polisi na upande wa Jamhuri umeshindwa kuleta ushahidi ambao utaweza kuishawishi Mahakama iwaone washitakiwa wote wana kesi ya kujibu,” alidai wakili Nassor.

Hakimu Nongwa aliarisha kesi hiyo hadi Machi 4 mwaka huu, ambapo atakuja kutoa uamuzi wa ama kuwaona washitakiwa wana kesi ya kujibu au la na kuamuru Ponda na Mkadamu warudishwe rumande kwa sababu bado Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP), Dk Eliezer Feleshi hajaondoa hati yake ya kuwafungia dhamana.



Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU