Facebook Comments Box

Saturday, May 11, 2013

PICHA ZA BONANZA LA VYUO VIKUU VYA MKOA WA KILIMANJARO


Mabingwa wa Netball VETA MOSHI wakiwa katika goli la Mwenge University


Mvua zilizonyesha kabla zilileta dosari na kuchelewesha mechi za Basketball





Mabingwa Kcmc kabla ya Fainali ya Mpira wa Kikapu


Vikombe vya washindi vilivyo tolewa


Washindi wa mpira wa Kikapu KCMC wakiwa na kikombe chao

Fred Maiko Leizer akiwa na kikombe cha mshindi wa kwanza
Waandaaji wa mashindano wakitoa maelezo kabla ya Fainali ya KCMC na Baptist


Kikundi cha kucheza mziki cha TIGO kikitoa burudani

Kikundi cha sarakasi cha TIGO kikitoa burudani baada ya mashindano kuisha




MSIKILIZE MRISHO MPOTO AKIMSEMA LADY JAY DEE HADHARANI

Msanii Mrisho Mpoto ambaye pia ametoa mada katika semina iliyo andaliwa na Clouds Media ambapo alimchamba Lady Jay Dee hadharani. Msikilize hapo chini
 




JESHI LA POLISI LAKANUSHA KANISA KUPIGWA BOMU

Jeshi la Polisi Mkoa wa Dar es Salaam limetoa taarifa baada ya kuwepo uvumi kuwa Kanisa la KKKT usharika wa Kunduchi Beach, lililopo Kunduchi, Dar es Salaam limelishambuliwa kwa kupuliwa kwa bomu na kurushiana risasi.

Kamanda wa Polisi Suleiman Kova amesema ukweli ni kuwa hakuna ulipuaji bomu uliofanyika katika Kanisa la KKKT Kunduchi Beach ISIPOKUWA kikosi cha Polisi kilichokuwa kinapambana na wahalifu waliokuwa karibu na Kanisa hilo kililazimika kurusha bomu la machozi ili kupambana na kuwatia mbaroni wahalifu hao.

Kova ameongeza kwa kusema waumini waliokuwepo Kanisani walishituka kwa kudhani kuwa wamevamiwa, lakini baadaye walipofahamu kinachoendelea walijitokea ili kusaidia, "Wakati askari wetu wanapambana na majambazi hayo- waumini wa kanisa hilo wamejitokeza kuwasaidia askari wetu. Naomba unisaidie kukanusha. Siyo kweli, nitazungumza na vyombo vingine vya habari kuweka sawa," amesema Kova.

---
Taarifa hii imekukuliwa kutoka ITV na Radio One Stereo.
Tusubiri taarifa iliyoahidiwa kutolewa ili kuondoa tashwishi.


NAIBU WAZIRI AINGILIA KATI UGOMVI WA JIDE NA RUGE


IKIWA ni siku moja tu tangu Naibu Waziri wa Habari  Michezo Vijana na Utamaduni Amos Makala kutangaza hadharani kulivalia njuga suala la mzozo kati ya Mkurugenzi wa wa Kampuni ya Clouds Media Group Ruge Mutahaba  na msanii nyota wa kike wa Bongo Fleva Judith ‘Wambura Lady Jaydee’  Ruge ametoa ya moyoni.
Tanzania Daima ambayo ilimpigia simu Ruge na kumuuliza ana lipi la kusema baada ya Makala kutamka kwamba atawaita wawili hao na kuzungumza nao sambamba na kuleta suluhu.
“Mimi kana nilivyosema katika tamko langu wiki iliyopita kwamba niko tayari tuitwe na watu watusikilize  pande zote mbili  hasa mlalamikaji na ukweli uweze kuwa wazi zaidi kwa sababu hadi sasa Lady Jaydee amekuwa akisema mambo mengi kiasi kwamba hata nashindwa kumuelewa”
Na siyo Waziri Makalla tu pia ikiwezekana hata kama kuna watu wengine wanataka kujitokeza ili kutuweka katika kiti moto watuulize maswali na kila mmoja wetu aote majibu mbele ya hao watu mimi niko radhi kufanya hivyo” anasema Ruge.
Wakati huohuo Ruge ameongeza kwamba  tayari ameshafuata taratibu za kisheria ikiwa ni pamoja na kumfungulia jalada la malalamiko ya kutukanwa na Lady Jaydee na taarifa hiyo amepelekewa  msanii huyo akiitwa katika vyombo vya sheria.
Lakini ninaweza kusema jambo hili linaweza kuzungumzika nje ya vyombo vya sheria kwani sisi tunaliona ni jambo dogo na la mzaha lakini lina athari kubwa katika jamii inayotuzunguka  anasema Ruge.
Mwanzoni mwa mwezi huu Lady Jaydee aliamua kuibuka na kuituhumu Clouds Media Group  kwa kutumia mitandao ya kijamii kama facebook, twitter nab log yake kwamba wana muhujumu kimuziki , kuzuia matangazo ya mgahawa wake wa Nyumbani Lounge   na kipaji chake kwa ujumba tuhuma ambazo Ruge na Clouds wanazikanusha vikali.
Mwandishi wa habari hii alijaribu kumtafuta Lady Jaydee azungumzie kuhusu kauli ya Waziri kwa kupitia simu ya mumewake Gadner Habash simu iliita bila kupokelewa.


SEMINA YA 'TWEN ZETU' YA CLOUDS MEDIA GROUP ILIVYOFANYIKA DODOMA



Mbunge wa Kigoma Kaskazini CHADEMA Ndugu Zitto Kabwe akizungumza na wasanii mabalimbali wakati akitoa mada katika semina ya kampeni maalum ya “Twen Zetu” iliyofanyika kwenye ukumbi wa African Dream mjini Dodoma leo , Kampeni hiyo inazungumzia na kuhamasisha vijana kuwa wabunifu na kutumia fursa zilizopo ili kujikwamua kimaisha lakini pia kuleta maendeleo kwa wasanii wenyewe na taifa kwa ujumla Watu mbalimbali wametoa mada katika semina hiyo ambao ni Patrick Ngowi, Zeno Ngowi Msanii Mrisho Mpoto na Ndugu Zitto Kabwe mwenyewe.
MRISHO MPOTO AKITOA MADA KATIKA SEMINA HIYO DODOMA HII LEO


Mkurugenzi wa Maendeleo na Utafiti Clouds FM Bw. Ruge Mutahaba akizungumza katika semina hiyo . Mkubwa Fella kutoka TMK akizungumza katika semina hiyoDJ Elly katikati Godzilla kushoto na Izo Busness wakiwa katika semina hiyo.Benny Kinyaiya akizungumza katika semina hiyo kulia ni Babu Tale na kushoto ni Said Bonge.Millad Ayo akizungumza Anold Kayanda akitoa mawazo yake.Ibrahim Masoud na washiriki wengine wakiwa katika semina hiyoDj fetty Afande sele akiwa na wenzie, kulia ni Shilole.
Khamis Mandi B12 akichangia Mada Gerlad Hando Shafii Dauda na Loveness Love 'Diva' wakifuatilia mada zilizokuwa zikitolewa katika semina hiyo


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU