Facebook Comments Box

Saturday, December 21, 2013

WAKIWA NA ASILIMIA ZAIDI YA MIA ZA USHINDI YANGA YATANDIKWA 3 KWA 1 NA MAHASIMU WAO BILA YA HURUMA



Timu ya Simba ya Msimbazi Dar es Salaam leo wameonesha kwamba wao sio wa kuchezea japo hawakupewa kabisa nafasi ya ushindi na mashabiki walio wengi. 

Simba ailionesha kuwa leo watapoteza mawazo ya mashabiki walio wengi wa Yanga pale ilipojipatia bao la kwanza kupitia kwa mshambuliaji wao kutoka Burundi ambae anaongoza kwa ufungaji wa mabao katika ligi kuu ya Vodacom Amis Tambwe.

 Tambwe baadae akaipatia timu yake bao la pili kwa mkwaju wa Penati baada ya Mshambuliaji wao mwenye chenga za maudhi Ramadhan Abdallah Singano 'MESI' kuangushwa ndani ya eneo la hatari na beki wa Yanga David Charles Luhende na mwamuzi kuamuru ipigwe penati.

Simba walipata bao la tatu kutoka kwa mchezaji wao mpya Awadh Juma baada ya kufanikiwa kumpokonya mpira kipa wa Yanga Juma Kaseja Juma aliyetaka kuurudisha mpira ndani ya box ili audake ndipo ukamgonga na mfungaji kuuwahi na kuuweka nyavuni.

Yanga walijipatia bao la kufutia machozi kupitia kwa Emanuel Okwi kwa kichwa baada ya kuwazidi ujajnja mabeki wa timu ya simba ambao leo wamestahili pongezi kubwa kwa kuwa imara tangu mwanzo.


ZITTO KABWE APOKELEWA KAMA RAISI MKOANI KIGOMA ALIPO WASILI LEO ASUBUHI TAZAMA PICHA






Zitto Kabwe akiwa katika gari la wazi mara baada ya kutua kigoma asubui ya leo ambapo amepata mapokezi ya kishindo.
 



KIBONZO: KIPANYA NA WATAFUNA NCHI



HEBU JIONEE JINSI WANAOBEBA MADAWA YA KULEVYA WANAVYO PASULIWA ILI KUYATOA

Dawa za Kulevya hazifai hakuna asiyefahamu jambo hili lakini unakuta baadhi ya watu wanayaweka maisha yao rehani na kukubali kuwa 'Punda' na kubeba mizigo hii haifai waache mara moja wote wenye tabia hii ni hatari kwa maisha yao.



Picha ya X-ray inavyoonesha tumboni madawa yaliovyo kwa mtu aliyebeba.

Athari inayoweza kupatikana yakiwa mwilini kama unavyoweza kujionea hapo juu.


Operesheni ikifanyika tayari kuyaondoa madawa hayo yaliyo sababisha kijana huyu kufariki.


Utumbo umetolewa tayari ili kuanza kuyatoa madawa hayo.


Kama uonavyo weza kujionea dawa hizo zikiwa ndani ya utumbo mpana.
Dawa zikianza kutolewa pamoja na kushafishwa kama unavyoona katika picha.




Kabla mtu hajazimeza zinakuwa hivi, sasa hebu fikiria mtu anameza kete hadi 5000 hii ni balaa kubwa sana.



 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU