Facebook Comments Box

Sunday, November 23, 2014

TAMKO LA HIZB UT-TAHRIR JUU YA YANAYOTOKEA KENYA

Kwa mara nyengine tena Waislamu nchini Kenya   wameshuhudia uvamizi wa polisi wa misikiti miinne Sakina Musa, Swafaa na Minaa Mjini Mombasa.

Kitendo hiki cha kinyama kilichopelekea
mauaji ya mwanafunzi mmoja huku vijana wapato mia mbili na hamsini kutiwa mbaroni, kilifanywa chini ya kisingizio cha kuwafurusha vijana wenye misimamo mikali. Harakati ya Hizb
ut-Tahrir Afrika Mashariki inalaani vikali kitendo hiki na twasema yafuatayo:-

Ukatili wa polisi wa Kenya umezidi sana hasa kwa Waislamu ; Huku kukiwa kuna magenge ya-nayotekeleza mauaji kama vile Baghdad boys na Mungiki ambayo wengi ya wafuasi wake ni wakristo hatujashuhudia hata kanisa moja likivamiwa na polisi kama inavyofanywa kwa Waislamu. Bali polisi katika kuendeleza maonevu kwa Waislamu, huwapachika majina radicalists na
extremists kuhalalisha unyama wao dhidi yao. Na hii ndio sura kamili ya polisi leo ndani ya nidhamu za kibepari namna
wanavyotumiwa katika kuwafanyia unyama Waislamu. Madai ya kuwa kuna Waislamu wabaya na Waislamu wazuri
‘radicalists and moderates ni njama tu kuwagawanya Waislamu.

Na hata kama kuna tofauti baina ya Waislamu kifikra na kimisimamo,basi waachiwe wenyewe Waislamu kwani Uislamu uliwawekea utaratibu maalum wa kutatua kasoro hizo. Hivyo haijakuwa halali kwa serikali kuendeleza mateso kwa Waislamu kwa kisingizio hicho. Tunakataa miito hii pamoja na vita
kupambana na ugaidi kwani vyote hivyo ni kuushambulia Uislamu na Waislamu.

Udhalilifu huu umetokamana kukosekanwa na waakilishi wa kikweli  wa mambo ya Waislamu. Hata wale baadhi ya wanasiasa wanaojitokeza ati kukashifu unyamu huo, wao hufanya hivyo kwa lengo tu la kujitafutia umaarufu wa kisiasa. Ushahidi wa haya ni kuwa hao hao ndio huwadaa raia kuwa kushiriki kwao ndani ya nidhamu za kidemokrasia ndio njia ya kuzuia dhulma juu ya Waislamu. Na ukweli ni kuwa nidhamu za kidemokrasia ndio chanzo cha balaa zote zinazoshuhudiwa na watu wote Waislamu na wasokuwa waislamu.

Madhila haya leo ni sehemu tu ya miongoni mwa mengi yanayofanyiwa Waislamu kote dunia  na hayatokoma leo hadi pale Waislamu watapoweza kufanya kazi ya kubeba ulinganizi wa Kiislamu kwa lengo la kusimamisha utawala halisi wa Kiislamu Khilafah katika moja wapo ya nchi za Kiislamu.  Utawala huo ndio
utakaohifadhi kikweli Waislamu na Wasokuwa Waislamu na kuwakinga dhidi ya shari za maadui zao.

KUMB: 04 / 1436 AH   
25th Muharram 1436 AH
18/11/2014 CE
Shabani Mwalimu
Mwakilishi kwa Vyombo Vya Habari Hizb ut-Tahrir Afrika
Mashariki



RASMI: JAJA AONDOKA YANGA: NAFASI YAKE YAPEWA MBRAZILI MWINGINE

Kiungo mkabaji raia wa Brazil Emerson De Oliveira Neves Rouqe anatarajiwa kuwasili siku ya jumanne mchana jijini Dar es salaam kwa ajili ya majaribio katika klabu ya Young Africans na endapo atafuzu moja kwa moja atajiunga na mabingwa mara 24 wa Ligi Kuu Tanzania bara.

Emerson mwenye umri wa miaka 24 ambaye kwa sasa anachezea timu ya Bonsucesso FC iliyopo ligi daraja la pili nchini kwao Brazil, msimu uliopita alikuwa akicheza soka la kulipwa nchini Poland katika timu ya Piotrkow Trybunalski FC iliyopo Ligi Daraja la pili nchini humo.

Ujio wa Emerson kuja kufanya majaribio nchini unakuja kufuatia mshambuliaji wa kimataifa kutoka nchini Brazil pia Geilson Santos "Jaja" kushindwa kurejea nchini baada ya kwenda kwao Brazil na kutoa taarifa kwamba hataweza kurejea tena nchini kutokana kukabiliwa na matatizo ya kifamilia.
Awali ilikua familia ya Jaja ije nchini katika kipindi cha mapumziko, lakini waliomba yeye Jaja ndio aende Brazil na mara baada ya kufika huko matatizo ya kifamilia aliyokutana nayo yamepelekea kushindwa kurejea nchini
 kuitumikia klabu yake na kuomba abakie kwao kwa ajili ya kutatua matatizo hayo.
Kuondoka kwa Jaja kunafanya klabu ya Young Africans kubakia na wachezaji wanne tu wa kimataifa ambao ni Mbuyu Twite, Haruna Niyonzima, Hamis Kizza na Andrey Coutinho hivyo endapo Emerson atafuzu  atakuwaa
 anakamilisha idadi ya wachezaji watano wa kimataifa.

Endapo Emerson atafuzu majaribo pamoja na vipimo atajiunga na kikosi cha kocha mbrazil Marcio Maximo katika nafasi ya kiungo mkabaji ikiwa ni sehemu ya kuboresha timu kuelekea kwenye michezo ya Ligi Kuu ya Vodacom pamoja na mashindano ya kimataifa.
Aidha kikosi cha Young African baada ya kuwa mapumzikoni kwa takribani wiki mbili, kinatarajiwa kuanza mazoezi siku ya jumatatu katika Uwanja wa shule ya sekondari Loyola kujiandaa na mchezo wa Nani Mtani Jembe
pamoja na mzunguko wa nane wa Ligi Kuu ya
Vodacom Tanzania bara.


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU