Facebook Comments Box

Tuesday, December 18, 2012

NDEGE KUBWA KUANZA KUTUA KIGOMA




NDEGE kubwa za abiria za kimataifa zinatarajiwa kuanza kutua Uwanja wa Ndege wa Kigoma kuanzia Desemba 15 mwaka huu baada ya uboreshaji wake kufikia hatua nzuri.
Akizungumza katika mahojiano maalumu na blog hii mjini Kigoma, Meneja wa Mamlaka ya Usafiri na Usalama wa Anga (TCAA), Godlove Hongore amesema hadi kufikia katikati ya mwezi ujao meta 1,450 za kuruka na kutua ndege zitakuwa zimekamilika kujengwa kwa kiwango cha lami kati ya meta 1,800 zinazotarajia kujengwa.
Alisema mkataba wa ujenzi wa mkandarasi wa uwanja huo unaisha Juni mwakani lakini ujenzi umeelezwa na msimamizi wa Kampuni ya Synohydro ya China kwamba unaweza kukamilika mapema zaidi ya muda uliopangwa.
Meneja wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege mkoani Kigoma, Elipid Tesha alisema mazungumzo yanaendelea vizuri ili kampuni hiyo ya Synohydro ya China iendelee na sehemu ya pili ya mradi huo katika mwaka ujao wa fedha utakaohusisha ujenzi wa njia ya kurukia ndege kufikia meta 3,000 na jengo la utawala na abiria uwanjani hapo.
Alisema tayari fedha za fidia kwa ajili ya eneo la makaburi ambalo litatumika kwa upanuzi huo, ipo na mazungumzo yanaendelea ni kuwezesha mkandarasi huyo kuendelea na sehemu hiyo ya pili ya mradi huo.
Meneja huyo wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Mkoa, alisema kukamilika kwa Awamu ya Pili ya ujenzi wa awanja huo kutaufanya Uwanja wa Ndege wa Kigoma kuwa na hadhi ya kimataifa na kuruhusu ndege kubwa zaidi ya tani 70 kutua.
Alibainisha kuwa uwanja huo ukikamilika, utakuwa kitovu cha ndege nyingi kutoka nchi za ukanda wa Maziwa Makuu na Afrika ya Kati kwenda Kusini na Kaskazini mwa Bara la Afrika na nje ya bara hilo.


KIGOMA UJIJI YATOA MWANAFUNZI BORA WA SAYANSI

SHULE ya Sekondari ya Kichangachui katika Manispaa ya Kigoma Ujiji imetoa mwanafunzi bora wa masomo ya sayansi kwa Kanda ya Magharibi katika mtihani wa majaribio (Mock Test) wa kidato cha nne uliofanyika hivi karibuni.
Akitoa taarifa kwa Balozi wa Jamhuri ya Korea nchini, Chung IL aliyefika shuleni hapo kukabidhi rasmi maabara kwa uongozi wa shule hiyo Mkuu wa Shule hiyo, Harles Lugenda alisema kuwa mafanikio hayo yametokana na kuanzishwa kwa maabara ya masomo ya sayansi katika shule hiyo.
Lugenda alimtaja mwanafunzi huyo kuwa ni Justus Ferdinand ambaye aliongoza katika masomo ya Fizikia na Kemia ambapo alisema kwamba kuwepo kwa maabara hiyo iliyoanza kufanya kazi Januari mwaka huu kumeinuka ari ya wanafunzi wa shule hiyo kusoma masomo ya sayansi na kuahidi kufanya vizuri.
Maabara hiyo imetolewa na serikali ya Jamhuri ya Watu wa Korea kupitia Shirika lake la Maendeleo (KOICA) ambapo kiasi cha Sh milioni 25 zimetumika kwa ajili ya ukarabati wa vyumba viwili vya madasara vinavyotumika kama vyumba vya maabara na vifaa vyake.
Sambamba na ujenzi wa vyumba hivyo vya maabara pia Serikali ya Korea kupitia shirika hilo inagharamia masomo ya wanafunzi wanane wanaosoma masomo ya sayansi shule hapo ambapo tayari wameshalipiwa ada kwa miaka minne ahadi watakapomaliza masomo yao ya sekondari.
Akizungumza katika makabidhiano hayo Balozi Chung IL alisema kuwa msaada huo umelenga kunaimarisha ushirikiano wa kindugu uliopo baina ya serikali hizo mbili na watu wake.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Manispa ya Kigoma Ujiji , Alfred Luanda alisema kuwa pamoja na msaada huo bado Manispaa hiyo inakabiliwa na upungufu wa maabara za sayansi na vifaa vyake katika shule zake mbalimbali na kwamba kama ipo fursa ya kupata tena msaada zaidi aliomba serikali ya Korea kuangalia uwezekano huo.


BREAKING NEWS: MTU MMOJA AUWAWA KATIKA MAJIBIZANO YA RISASI KATI YA POLISI NA MAJAMBAZI KARIAKOO LEO HII

Mtu mmoja ameuwawa mida hii katika majibizano ya risasi yaliyotokea maeneo ya Msimbazi kariakoo, mtaa wa Livingstone kati ya Polisi na majambazi waliotaka kupora fedha zilizokuwa zinapelekwa benki ya NBC.

Majambazi hao waliokuwa wamevalia nguo za kiraia inasemekana walijua fedha hizo zinapelekwa leo hivyo walijiandaa kupora na Mapolisi nao waligundua hilo mapema hali iliyofanya majambazi hao kurusha risasi hovyo na kukimbia ili kukwepa kukamatwa.

Hadi sasa ni mtu mmoja anayeripotiwa kuuwawa ila bado haijajulikana kama ni raia au jambazi wale maana pia majambazi walivaa kiraia.


AKAMATWA NA UCHAWI MAHAKAMANI KISUTU

Kijana ambae ni mganga kutoka katika mkoa wa Tanga wilaya ya Muheza eneo la Kerege amekamatwa na vifaa ambavyo vinadaiwa kuwa vya kichawi ambavyo alikuwa akiingia navyo mahakamani ili kumfanyia uganga mmoja ya watu wanaokabiliwa na kesi katika mahakama hiyo. Polisi waliweza kugundua kupitia vifaa maalumu ambavyo vimefungwa mahakamani hapo. Picha hapo juu ni mganga huyo akiwa chini ya ulinzi wa polisi

 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU