Facebook Comments Box

Friday, June 21, 2013

PICHA: MBOWE NA LEMA WALIVYO JISALIMISHA POLISI JANA


MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe akitoka Polisi baada ya kuhojiwa.


MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe akiongozana na Mbunge wa Arusha mjini, Godbless Lema wakitoka Polisi baada ya kuhojiwa.
Mwenyekiti wa CHADEMA Fremaan Mbowe pamoja na mbunge wa Arusha mjini Godbless Lema jana wamejisalimisha polisi kufatia tamko la jeshi la polisi kusema kuwa linawasaka waheshimiwa hao
akingea na waandish wa habari mwenyekiti wa chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA Fremaan Mbowe alisema kuwa wao wamejisalimisha kama polisi walivyosema wanawatafuta na walipofika waliandika maelezo ambapo alisema kuwa polisi waliwaita kwa mambo mawili moja likiwa ni kwa kuwaoji kwanini walifanya mkutano pasipokuwa wa halali ambapo alisema kuwa
"jambo la kufanya mkutano pasipo kuwa halali sio kweli kwani polisi walituruhusu tukafanye mkutano katika sehemu hile lakini kinachotushangaza tumefanya wamekuja kutupiga mabomu nakusema sio wa halali na kuhusiana na ushaidi msimamo wangu upo pale pale tunao ushaidi wa kutosha na tunamjua aliyerusha bomu siku ya jumamosi lakini hatuta utaoa hadi pale Rais atakapo unda tume huru ya majaji ili wafatilie swala hili hao ndo tutawaonyesha ushaidi wetu lakini polisi hatuwezi kuwapa "hii ni kauli ya mbowe
chagonja akiongea na waandishi wa habari
kwa upande wa kamishana wa mafunzo na uperesheni ya kijeshi Paul Chagonja akiongea na waandishi yeye alisema kuwa wamekuja wamewaoji na kuwaomba ushaidi huo lakini waeshimiwa hawa hawakuwaonyesha ushirikiano
"mbowe alisema kuwa anaushaidi na hata katika vyombo vya habari ametangaza lakini nacho shangaa tulivyomuuliza hapa amesema kuwa hana ushaidi wowote na wala ajawai kutamka hivyo sasa sisi kwakuwa kasema hivyo nitakaa na makachero wangu na tutaangalia jinsi ya kufanya"alisema chagonja
Aidha alisema kuwa alimuliza mbunge wa Arusha mjini kwanini awali alikuja na kuwasifia polisi baadae akaja kuegeuka na wakati alisema kuwa awezi sema uwongo na akasema yeye anafata mwenyekiti wake anachosema.


WAKE WA MARAIS KUFANYA MKUTANO TANZANIA MWEZI UJAO


Mke wa Rais wa Marekani,Michelle Obama, 
Dar es Salaam. Rais wa zamani wa Marekani, George W. Bush na mkewe,Laura wanatarajiwa kuendesha Mkutano wa Kimataifa wa wake wa marais wa Afrika kuzungumzia nafasi ya wanawake kuinuka kimaendeleo utakaofanyika Dar es Salaam, Julai 1-2 mwaka huu.
Mkutano huo ambao ni wa kwanza kufanyika nchini, utakwenda sambamba na ziara ya Rais wa Marekani, Barack Obama pia utajumuisha maofisa wa Serikali,viongozi wa mashirika ya kiraia na wasomi wa kada mbalimbali.
Taarifa iliyotolewa na Wakfu wa George W. Bush imesema kuwa mkutano huo utakaokuwa na kauli mbiu; “Kuwekeza kwa wanawake kunaiinua Afrika” imewataja baadhi ya wazungumzaji kuwa ni pamoja na Bush mwenyewe na mkewe Laura, Mke wa Rais wa Marekani,Michelle Obama, Mke wa Waziri Mkuu wa zamani wa Uingereza,Cherie Blair na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kupambana na Ukimwi (Unaids), Michel Sidibé.
Taarifa hiyo imesema kuwa wake hao wa marais wa Afrika wanatoa mchango mkubwa wa kusukuma mbele agenda za maendeleo katika sekta za afya na elimu hivyo kukutana kwao kutatoa fursa nyingine ya kujadiliana changamoto zinazowakabili na kuweka mikakati ya pamoja.
“Wake za marais wanalo jukumu muhimu kuhusiana na uboreshwaji wa ustawi wa wanawake… wao wana nafasi kubwa ya kuinua na kuboresha sekta kama elimu,afya na maendeleo ya kiuchumi hivyo kukutana kwao ni hatua muhimu itayotoa mwanga kuhusiana na hatua zinazopaswa kufanywa kuwawezesha wanawake,”ilisema sehemu ya taarifa hiyo.
Baadhi ya wake za marais watakaohudhuria mkutano huo ni wa pamoja na Mke wa Rais wa Uganda, Janet Museveni,mke wa Rais wa Msumbiji, Maria da Luz Dai Guebuza, mke wa Rais wa Sierra Leone, Sia Nyama Koroma na mwenyeji wao Salma Kikwete.
Miongoni mwa mada zinazotarajiwa kujadiliwa wakati wa mkutano huo ni pamoja na kuwawezesha wanawake ujasiriamali kupitia mafunzo ya teknolojia,kutoa fursa na kuboresha shughuli za kilimo kwa wakulima wanawake na ukoaji wa maisha kwa kukabiliana na saratani ya ziwa


HIVI NDIVYO MIAMI HEAT WALIVYO CHUKUA UBINGWA WA NBA

Miami Heat Usiku wa jana Imefanikiwa Kutetea Ubingwa wake kwenye uwanja wa Nyumba AMERICAN AIRLINES ARENA kwa kuichapa Timu kongwe ya SAN ANTONIO SPURS kwa vikapu 95 kwa 88.

Alikuwa ni KING JAMES tena akiongoza Tim yake katika mbio hizi za mwisho za Ubingwa na kucheza katika kiwango bora sana usiku wa jana.KING JAMES aliipatia Timu yake vikapu 37 NA Rebounds 12 na kutoa assist za Kutosha kuhakikisha Ushindi unabaki nyumbani MIAMI,FLorida.Ikiwa ni kwa mara ya Pili Mfululizo MIAMI HEAT kuchukua kombe hilo baada ya mwaka Jana Kunyagua ubingwa Huo kwa Kuichapa Oklahoma City kwa game 4-2.Safari hii haikuwa Rahisi kwa HEAT kuchukua Ubingwa huo kwani Spurs walionyesha upinzani Mkubwa toka mwanzo wa Game 1,Fainali hii ilikuwa ya Piga nikupige Mpaka kufikia kufika katika Hatua ya GAME 7 ambayo ni kufa na kupona.HEAT kafanikiwa kuchukua Kombe hili baada ya ushindi wa Game 7.Wakitumia vizuri Mastar wao watatu(james,wade na bosh) Heat ilifanikiwa kupata ushindi huo.Ukiachana na Scores za King James,Wade pia alichangia Vikapu 23 NA rebounds 10,huku Bosh Akionekana kucheza Defence Nzuri Iliyo wapa shida sana Wachezaji wa SPURS.Wakizungumza na Vyombo vya Habari WADE na KING JAMES wameonekana ni watu wenye Furaha Huku wakishusha Sifa kemkem kwa wachezaji wa SPURS kwani haikuwa rahisi kwao Kuchukua Ubingwa huo kwa mara ya pili.HEAT imekuwa ni Timu ya Pili Kuchukua kombe hilo kwa mara ya pili Mfululizo kwa Miaka ya Karibu toka ichukue LA LAKERS 2009-2010.
Kwaa upande wa Spurs ambayo ndo Kwa mara ya kwanza Inapoteza Game Ya Fainali Katika Historia,Ilionekana Kuceza Vizuri kama kawaida Ila kila mtu akiwa na Mawazo na Majuto baada ya kupoteza Ushindi game 6 KATIKA hali isiyo tarajiwa,Akizungumza na Vyombo Vya habari Mmoja wa Wachezaji wakongwe wa SPURS MANU GINOBILI "Scientist" alisema bado akifumba macho anaiona GAME 6  gizanikitu ambacho wanajutia sana kupoteza mchezo Ule.Mkongwe timu Duncan katika harakati za Kutaka kuisaidia timu yake kuchukua Ubingwa Huo mara TANO akiwa na timu HIYO ziligonga mwamba jap alichangia vikapu 24 NA REBOUNDS 12.Alikuwa ni Kawhi Leornard Tena aliyekosa Mtupo Huru game 6 na kusababisha madhara kwenye timu Yake pia Game 7 ALIKOSA 3POINT ambayo ingeleta matokeo andapo angefunga na kuwaacha HEAT wakiambaa ambaa na ushindi.Tony Parker alikuwa kwenye kiwango chake lakini kazi Nzuri iliyofanywa na KING JAMES ya kumficha TONY parker asionekana kabisa kwenye game hiyo japo alipata nae Tab kidogo.DANNY GREEN aliyeonekana kung'aa zaidi game 5 Alipotea kabisa game 6 NA 7 NA KUWAACHA wakongwe wakiparangana.
HEAT imekuwa ndo timu ya Kwanza kuifunga Spurs kwenye Mchezo wa Fainali nd TIM DUNCAN,TONY PARKER,MANU GINOBILI ndo imekuwa mara yao ya kwanza Kupotea mchezo wa Fainali kwa fainali Tano walizoshiriki.Spurs Imeingia Fainali Za NBA mara TANO na imefanikiwa kuchukuwa mara NNE(1999,2003,2005,2007) na usiku wa jana kupoteza Huku HEAT IMEINGIA Fainali hizo mara mara NNE ikiwa Imechukuwa mara TATU (2006,2012,2013)Na 2011 ilipoteza Dhidi ya Dallas.

PICHA ZA MATUKIO YA GAME 7 KATI YA SPURS VS HEAT:

Tony Parker akijikuta kwenye wakati mgumu mbele ya KING JAMES Wakati akijaribu kuleta madhara.
VITA YA BOSH NA MKONGWE DUNCAN ILICHUKUWA NAFASI YAKE KAMA KAWAIDA MA'BIG HAWA WAKIKUTANA.
BOSH AKITIKISHA DEFENCE YA SPURS HUKU MONGWE MANU GINOBILI AKIHAKIKISHA ULINZI
KING JAMES LEBRON AKIFANYA YAKE MBELE YA WACHEZAJI WA SPURS KUDHIHIRISHA U'MVP WAKE.
FUNDI TONY PARKER AKIPIMANA UBAVU NA MARIO CHALMERS KUCHUKUWA BORI
MASHABIKI WA HEAT WAKISHANGILIA USHINDI WAO KWA KISHINDO IKIWA NI KWA MARA YA TATU SASA NA MARA YA PILI MFULULIZO.


MVP MARA NNE  na MVP MARA MBILI KWA SASA KING JAMES AKISUMBUA DEFENCE YA SPURS KUHAKIKISHA USHINDI UNABAKI NYUMBANI HUKU KAWHI LEORNARD AKIJARIBU KUMZUIA.



TIM "MKONGWE" DUNCAN AKIMTISHA TOTO CHRIS BOSH

TONY"FUNDI"PARKER AKIMCHAPA SHOOT MIKE MILLER.
MANU GINOBILI "SCIENTIST"AKIMPIGA FACE NORRIS COLE.


SPAIN YAIRARUA TAHITI MABAO KUMI KWA SINIA

.
.


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU